Mdunguaji wa Goma

RIWAYA; MDUNGUAJI WA GOMA.

NA; BAHATI K MWAMBA.

SIMU; 0758573660.

SEHEMU YA TATU.



Wakati yeye akidhani ni yeye mwenye akili za kukagua mazingira kabla ya kazi, alijidanganya.

Kulikuwa na mtu mwingine nae alikuwa na kazi kama yake na, yeye alipenda kukagua mazingira kabla ya kazi na, jioni hiyo na yeye alikuwa anaenda kwenye jengo la mauzo kuweka mambo yake sawa.

Wote wawili walijikuta wakianza kazi kabla ya siku iliotakiwa. Walianza mtafutano kabla ya wakati.

Mtu huyo alikuwa ni mtaalamu wa mapigano na kuruka viunzi. Kujikunja na kujikunjua kwa kasi, kulifanya apachikwe jina la Kiuno cha nyoka, badala ya jina lake Said Magabe.

Jengo la mauzo lilijuta kuwafahamu viumbe wale kwa siku hiyo.

Moto ukawaka!



****

Jengo la mauzo lilikuwa katikati ya mji, ambapo kulikuwa na changanyikeni nyingi ya watu. Magari ya abiria na binafsi, yalipishana kwa mwendo was taratibu sana, kwa sababu ya wingi wa watu na shughuli zao.

Watu nao walikuwa wanapishana na magari hayo kwa umakini wa kawaida, kwa kuwa walijua wingi wao, uliwafanya madereva wawe makini kupita kiasi.

Miongoni mwa watu waliokuwa wakipishana na magari, alikuwa ni Miguu ya Kuku ambae macho yake yalikuwa makini kutazama lango la jengo alilokuwa anaelekea.

Alimtizama kila mtu aliyekuwa anaingia na kutoka kwenye jengo lile lenye urefu wa ghorofa nane. Miguu yake miembamba iliyofichwa na kanzu yake, ilizidi kulisogelea jengo lile bila kujali kuzongwazongwa na watu, waliokuwa na haraka zao.

Miguu yake ilimfikisha kwenye mlango wa vioo, ambao ulikuwa na kibao kilichoandikwa; ‘Push’.
Haraka haraka alitupia macho yake kila pande ya jengo lile na, alifanikiwa kuona njia upande wake wa mashariki. Njia ile ilikuwa inapitisha magari kuelekea mwenye maegesho, ambayo yalikuwa chini ya jengo lile. Kulikuwa na walinzi wawili wa kampuni fulani, ambao walilinda njia hiyo huku mmoja akiwa na kalamu na karatasi za risiti na, mwenzake akiwa na bunduki aina ya pumpaction 2p. Bunduki aina ya gobole, japo iliundwa kisasa zaidi na kupewa jina hilo.

Aliachana nao.

Mkono wake wa kulia ukataka kuusukuma mlango ule, lakini kuna mtu mwingine aliuvuta kwa ndani, ili apate nafasi ya kutoka ndani ya jengo lile lilosifika kwa uuzaji wa simu za aina zote; kwa bei ya jumla ama rejareja.

Alipishana na mtu yule ambae yalikuwa anatoka, na yeye akiingia.
Alipokelewa na hewa safi ilioletwa na viyoyozi, huku akishuhudia idadi kubwa ya watu ambao walikuwa wakichagua simu, kwenye maduka sita yaliokuwa pale ground.

Alivuta hatua zake taratibu akiwa kama ni mtu ambae anachagua duka la kufuata, lakini lengo lake lilikuwa ni kuona upande ambao ulikuwa na kambarau, ama mlango wa ngazi za kuelekea kwenye ghorofa za juu.

Macho yake yaliokuwa yanazurura mithili ya pimbi kwenye vilima vya mawe, yalifanikiwa kuona sehemu ya kambarau na sehemu ya ngazi za kawaida. Haraka haraka alipiga hatua na kuelekea ilipokuwa kambarau, alibonyeza kitufe cha kuruhusu kuingia, aliingia na kubonyeza kitufe namba nane.

Kambarau ilianza kupanda juu kuelekea mwisho wa jengo na muda wote Miguu ya kuku alikuwa makini na saa yake mkononi. Hadi anafika ghorofa ya mwisho, alikuwa amehesabu sekunde arobaini na tano tu na, hiyo ilikuwa ni kwa sababu haikusimama kuchukua ama kushusha mtu, alikuwa ni peke yake aliyeiongoza kuelekea mwisho wa jengo.

Alitoka na kuelekea upande wa ngazi, alichungulia chini na hakuona mtu, alichungulia upande wa juu na kuona ngazi zilikuwa zinaelekea juu, alizifuata.

Alitumia dakika moja kutokea juu ya jengo. Huko aliishia kuona mji wa Dar as laam kwa uzuri wake. Aliona majengo marefu yalivyolipendezesha jiji, aliona kwa mbali bahari ikiwa imebeba meli kubwa na ndogo, huku matanga ya mashua za wavuvi yakionekana kwa mbali, mithili ya nyota angani.

Miguu ya Kuku hakupanda huko juu kushangaa uzuri wa jiji la Dar es laam, bali alipanda huko juu kufanya vitu viwili.

Alitaka kujua ukubwa wa jengo lile kwa kusoma vipimo vya mzunguko wa huko juu na vipimo vile alivihesabu kwa hatua za miguu yake. Alipohakikisha amehesabu vema upana na urefu wa paa la jengo lile, alitulia na kuanza kupiga hesabu zake. Hesabu alizokuwa akipiga, ni upana wa kila ofisi ndani ya lile jengo na ilihitaji hatua zake ngapi,ili kuhama kibaraza kimoja kwenda kingine. Alipomaliza kukadiria, akabaki na kazi moja tu; kuhakikisha anatembelea moja ya ofisi zilizoko kwenye lile jengo na alichagua kutembelea ofisi itakayokuwa kwenye ghorofa ya nne, kwa kuwa alitakiwa kuchukua mzigo ghorofa ya tano.

Lakini kabla hajaenda kuitembelea ofisi hiyo, alitakiwa kumaliza jambo la pili ambalo lilikuwa limmfanya afike kule juu.

Kwa kuwa alijua lile jengo lilikuwa mtaa gani, alihitaji kuona mtaa wa pili ambao kulikuwa na makao makuu ya jeshi la polisi. Kupanda kule juu, kulimfanya autazame vema mtaa ule na aliangazia zaidi kwenye makao makuu ya jeshi la polisi.

Alitumia dakika tatu na sekunde kadhaa kutazama majengo ya makao makuu ya jeshi la polisi, kisha alitizama barabara zilizokuwa zinapitika kirahisi kutokea kwenye mtaa ule, kuelekea maeneo ya makao makuu ya jeshi. Wakati alipokuwa anatizama, bahati nzuri aliona kuna gari moja lilikuwa inatoka karibu na jengo la mauzo, kuelekea mtaa ambao kulikuwa na makao makuu ya jeshi. Alianza kuhesabu dakika za mwendo wa lile gari, hadi kufika mtaa uliokuwa na ofisi za jeshi la polisi.

Wakati macho yake yakiwa kwenye lile gari ambalo lilikuwa linatembea taratibu kwa sababu ya msongamano wa watu, huku akiwa amelikadiria mshale wa kasi wa lile gari, kuwa kwenye namba ishirini; Mara nyuma yake alisikia vishindo vya mtu, ambae ni kama alitua kutoka angani.

Masikio yake yanauwezo wa kutofautisha vishindo vya viumbe hai zaidi ya thelathini, hivyo hakupata shaka kujua vishindo vya kiumbe kilichodondoka nyuma yake.

Taratibu alielekeza macho yake juu, kuona kama kulikuwa na ndege ama helikopita yoyote iliyopita juu.

Ajabu hakuona wala kusikia kelele za miungurumo yoyote kutokea juu.

“Kiumbe gani anaepaa na kutua kwa vishindo vya binaadamu!” Aliwaza huku akianza kugeuka taratibu bila kuwa haraka yoyote.

Naam, macho yake yalikutana na binadamu akimtizama bila kupepesa macho. Binadamu ambae alikuwa ni mrefu na mpana wa mwili, huku akionekana kutozingatia mazoezi kwa sababu, nyama za mikono yake na kifua chake, havikuonekana kupitia kashkashi yoyote ya mazoezi.

Binadamu yule alikuwa ametota maji mwili mzima, huku mgongoni mwake akiwa amebeba kibegi, ambacho kilionekana kuwa na mzigo wa gram chini ya mia sita.

Macho ya Miguu ya Kuku yalimtizama mtu yule kwa umakini, kisha aliamua kutazama nyuma ya mtu yule na, hapo aliweza kuona tank la maji. Tank lile lilikuwa la Lita elfu moja.

“Ina maana mtu huyu katoka kwenye hilo simtank!?” Alijiuliza huku akishangaa peke yake.

Wakati akiendelea kumtazama, kwa haraka haraka alijaribu kupiga hesabu za dakika alizokaa kule juu, ambapo ilikuwa ni zaidi ya dakika saba na, muda wote huo ilimaanisha huyo mtu alikuwa ndani ya hilo tank.

“Inashangaza!” Alijisemea tena huku mara hii akigeuza shingo yake na kuitizama ile gari, ambayo ilikuwa inakaribia kufika usawa wa makao makuu ya jeshi la polisi. Aliondoa macho yake huko na kuitizama saa yake, ambapo aligundua imetumia dakika tano pekee, ikiwa kwenye mwendo wa kawaida sana.

Alirudi kumtizama yule bwana ambae muda wote alikuwa hajasema lolote zaidi ya kumwangalia tu.

“Pole na kazi fundi” Miguu ya Kuku alimwambia yule bwana.

“Wewe ni mhusika hapa?” aliuliza mtu yule kwa sauti ya kukwaruza.

“Napunga tu upepo bwana fundi” Miguu ya Kuku alijibu.

Bwana yule hakujibu kitu, alipiga hatua zake na kuelekea kwenye ngazi na kushuka chini.

Miondoko na macho ya yule mtu, yalimtisha Miguu ya Kuku, pia yalimpa tahadhari kubwa.

“Huyu sio mtu wa kawaida. Dakika saba ndani ya maji!” Alijiwazia huku akirudi kutazama kule kwenye ofisi za polisi.

Alianza kupiga hesabu zake kuhusu mwendo kasi wa magari ya jeshi la polisi, kuwahi kwenye jengo la mauzo baada ya tafrani kutokea.
“Kama mshale wa mwendo uko kwenye namba ishirini na, ametumia dakika tano, basi polisi kwenye mwendo wa dharura watatumia dakika moja na sekunde thelathini, wakiwa kwenye namba hamsini. Sekunde thelathini ni zile kona mbili tatu.” Aliwaza huku bado macho yake yakitizama barabara zilizotoka kwenye kituo cha polisi, kuelekea kwenye jengo la mauzo.

“Lakini polisi wetu huwa wanatumia dakika kumi hadi kumi na tano, kujiandaa kabla hawajaanza safari ya dharura. Dakika hizo hutumia kuitana, kubeba silaha na kupeana majukumu. Hivyo ili wafike kwenye hili jengo, inawahitaji watumie dakika ishirini pekee, japo hata kwa miguu wanaweza kufika ndani ya dakika nane na wakikimbia ni dakika tano. Lakini wakisikia risasi ni lazima waje na bunduki na magari.” Aliwaza tena huku alianza kuondoka na kuelekea chini, akiwa na nia ya kutumia ngazi kushuka chini.
Alitaka atumie ngazi ili ajue muda atakaotumia endapo itamlazimu kuzitumia.

Alipofika ghorofa ya saba, aligundua ofisi za kule juu wakati huo zilikuwa zimefungwa, hivyo kupelekea kuwe na ukimya wa kutisha.

Wakati anakaribia kufika ghorofa ya sita, masikio yake yalisikia vishindo vya mtu mwingine akipanda ngazi na, alipojaribu kusikiliza, aligundua mtu yule alikuwa anapanda ngazi kwa kasi kubwa na upandaji haukuwa wa kawaida.

Haraka na yeye aliziruka ngazi na kudondokea kwenye kibaraza cha ghorofa ya sita, kisha alichumpa na kwenda kujibanza kwenye korido ya moja ya ofisi zilizokuwa pale, kisha alitulia.

Vitendo vyake vilichukua sekunde mbili tu, kukamilisha mpango wake.

Sekunde tano baadae, alishuhudia mtu akipita kwa kasi kubwa, kuelekea ghorofa za juu. Mtu yule alikuwa ni yule aliemuona akiwa ametota maji.

“Baboon!” Alijisemea kivivu.

Akili yake ilimpa tahadhari, mwili wake nao ukakubali kuipokea tahadhari. Sekunde mbili baadae, kisu kilikuwa mkononi mwake na kwa kasi ya ajabu, aliichana kanzu yake katikati ya miguu, kisha akajifunga na kumfanya aonekane kama amevaa vazi la wahindi, jamii ya uddhu.

Lakini yeye pale alikuwa ametengeneza suruali kwa ajili ya dharura aliohitaji kukabiliana nayo.

Alirejesha kisu chake sehemu alipokitoa, kisha aliingiza mkono wa kushoto kwenye mfuko wa kanzu yake na alipoutoa, ilikuwa umeshika kifuko cha karanga kavu. Alikipasua kifuko kile, kisha alitoa karanga chache na kuzitupia mdomoni na, zilizosalia mkononi alizihesabu kwa idadi.

Zilikuwa karanga sita pekee, karanga zile alizitia kwenye mfuko wake wa kulia kisha akakitupa kifuko cha karanga, kikiwa na karanga zake, huku yeye akisalia na zile karanga sita mfukoni na zile za mdomoni akizimeza baada ya kuzitafuna.

Akapiga hatua ndefu kuelekea kwenye kibaraza cha ile ghorofa ya sita, ili apande ngazi kuelekea juu akutane na yule mbabe ambae alikuwa ameelekea huko.

Akili yake ilimwambia mbabe yule alikuwa amerudi kule juu kumuua, hilo hakutaka mbabe yule wa kukaa ndani ya maji, alifurahie.

Wakati mguu wake unakanyaga kwenye kibaraza, huku mkono wake ukijiandaa kudaka chuma cha kujishikiza ili kupanda ngazi, macho yake yalishuhudia kivulia kikija kwa kasi pale alipo.

Hakuzubaa.
Haraka nae alijivuta nyuma hatua moja, huku akimshuhudia yule jamaa akitua chini kama mzimu, baada ya kuruka kutokea kwenye kibaraza cha ghorofa ya saba, ikiwa na maana alitumia zile bomba kuserereka, kisha kujiachia na kutua ghorofa ya sita.

Macho ya Miguu ya Kuku yaliushuhudia mwili mkubwa, ukifanya maajabu.

Walitazamana bila kusemeshana.

Mchapo ukapangwa.

Wakati wao wakidhani walikuwa peke yao kwenye ofisi zilizokuwa ghorofa ya sita, walikosea. Kulikuwa na kiumbe mwingine ambae alikuwa kwenye lile jengo muda mrefu kabla yao, na alikuwa palepale kwenye ghorofa ya sita akiwa amejibanza akiwachora.

Huyu alikuwa ni Tembe za chai, mbabe wa babe.

Kumekuchwa jengo la Mauzo
.
.
.
.
Endelea kuwa nami
 
RIWAYA; MDUNGUAJI WA GOMA.

NA; BAHATI K MWAMBA.

SIMU; 0758573660.

SEHEMU YA TATU.



Wakati yeye akidhani ni yeye mwenye akili za kukagua mazingira kabla ya kazi, alijidanganya.

Kulikuwa na mtu mwingine nae alikuwa na kazi kama yake na, yeye alipenda kukagua mazingira kabla ya kazi na, jioni hiyo na yeye alikuwa anaenda kwenye jengo la mauzo kuweka mambo yake sawa.

Wote wawili walijikuta wakianza kazi kabla ya siku iliotakiwa. Walianza mtafutano kabla ya wakati.

Mtu huyo alikuwa ni mtaalamu wa mapigano na kuruka viunzi. Kujikunja na kujikunjua kwa kasi, kulifanya apachikwe jina la Kiuno cha nyoka, badala ya jina lake Said Magabe.

Jengo la mauzo lilijuta kuwafahamu viumbe wale kwa siku hiyo.

Moto ukawaka!



****

Jengo la mauzo lilikuwa katikati ya mji, ambapo kulikuwa na changanyikeni nyingi ya watu. Magari ya abiria na binafsi, yalipishana kwa mwendo was taratibu sana, kwa sababu ya wingi wa watu na shughuli zao.

Watu nao walikuwa wanapishana na magari hayo kwa umakini wa kawaida, kwa kuwa walijua wingi wao, uliwafanya madereva wawe makini kupita kiasi.

Miongoni mwa watu waliokuwa wakipishana na magari, alikuwa ni Miguu ya Kuku ambae macho yake yalikuwa makini kutazama lango la jengo alilokuwa anaelekea.

Alimtizama kila mtu aliyekuwa anaingia na kutoka kwenye jengo lile lenye urefu wa ghorofa nane. Miguu yake miembamba iliyofichwa na kanzu yake, ilizidi kulisogelea jengo lile bila kujali kuzongwazongwa na watu, waliokuwa na haraka zao.

Miguu yake ilimfikisha kwenye mlango wa vioo, ambao ulikuwa na kibao kilichoandikwa; ‘Push’.
Haraka haraka alitupia macho yake kila pande ya jengo lile na, alifanikiwa kuona njia upande wake wa mashariki. Njia ile ilikuwa inapitisha magari kuelekea mwenye maegesho, ambayo yalikuwa chini ya jengo lile. Kulikuwa na walinzi wawili wa kampuni fulani, ambao walilinda njia hiyo huku mmoja akiwa na kalamu na karatasi za risiti na, mwenzake akiwa na bunduki aina ya pumpaction 2p. Bunduki aina ya gobole, japo iliundwa kisasa zaidi na kupewa jina hilo.

Aliachana nao.

Mkono wake wa kulia ukataka kuusukuma mlango ule, lakini kuna mtu mwingine aliuvuta kwa ndani, ili apate nafasi ya kutoka ndani ya jengo lile lilosifika kwa uuzaji wa simu za aina zote; kwa bei ya jumla ama rejareja.

Alipishana na mtu yule ambae yalikuwa anatoka, na yeye akiingia.
Alipokelewa na hewa safi ilioletwa na viyoyozi, huku akishuhudia idadi kubwa ya watu ambao walikuwa wakichagua simu, kwenye maduka sita yaliokuwa pale ground.

Alivuta hatua zake taratibu akiwa kama ni mtu ambae anachagua duka la kufuata, lakini lengo lake lilikuwa ni kuona upande ambao ulikuwa na kambarau, ama mlango wa ngazi za kuelekea kwenye ghorofa za juu.

Macho yake yaliokuwa yanazurura mithili ya pimbi kwenye vilima vya mawe, yalifanikiwa kuona sehemu ya kambarau na sehemu ya ngazi za kawaida. Haraka haraka alipiga hatua na kuelekea ilipokuwa kambarau, alibonyeza kitufe cha kuruhusu kuingia, aliingia na kubonyeza kitufe namba nane.

Kambarau ilianza kupanda juu kuelekea mwisho wa jengo na muda wote Miguu ya kuku alikuwa makini na saa yake mkononi. Hadi anafika ghorofa ya mwisho, alikuwa amehesabu sekunde arobaini na tano tu na, hiyo ilikuwa ni kwa sababu haikusimama kuchukua ama kushusha mtu, alikuwa ni peke yake aliyeiongoza kuelekea mwisho wa jengo.

Alitoka na kuelekea upande wa ngazi, alichungulia chini na hakuona mtu, alichungulia upande wa juu na kuona ngazi zilikuwa zinaelekea juu, alizifuata.

Alitumia dakika moja kutokea juu ya jengo. Huko aliishia kuona mji wa Dar as laam kwa uzuri wake. Aliona majengo marefu yalivyolipendezesha jiji, aliona kwa mbali bahari ikiwa imebeba meli kubwa na ndogo, huku matanga ya mashua za wavuvi yakionekana kwa mbali, mithili ya nyota angani.

Miguu ya Kuku hakupanda huko juu kushangaa uzuri wa jiji la Dar es laam, bali alipanda huko juu kufanya vitu viwili.

Alitaka kujua ukubwa wa jengo lile kwa kusoma vipimo vya mzunguko wa huko juu na vipimo vile alivihesabu kwa hatua za miguu yake. Alipohakikisha amehesabu vema upana na urefu wa paa la jengo lile, alitulia na kuanza kupiga hesabu zake. Hesabu alizokuwa akipiga, ni upana wa kila ofisi ndani ya lile jengo na ilihitaji hatua zake ngapi,ili kuhama kibaraza kimoja kwenda kingine. Alipomaliza kukadiria, akabaki na kazi moja tu; kuhakikisha anatembelea moja ya ofisi zilizoko kwenye lile jengo na alichagua kutembelea ofisi itakayokuwa kwenye ghorofa ya nne, kwa kuwa alitakiwa kuchukua mzigo ghorofa ya tano.

Lakini kabla hajaenda kuitembelea ofisi hiyo, alitakiwa kumaliza jambo la pili ambalo lilikuwa limmfanya afike kule juu.

Kwa kuwa alijua lile jengo lilikuwa mtaa gani, alihitaji kuona mtaa wa pili ambao kulikuwa na makao makuu ya jeshi la polisi. Kupanda kule juu, kulimfanya autazame vema mtaa ule na aliangazia zaidi kwenye makao makuu ya jeshi la polisi.

Alitumia dakika tatu na sekunde kadhaa kutazama majengo ya makao makuu ya jeshi la polisi, kisha alitizama barabara zilizokuwa zinapitika kirahisi kutokea kwenye mtaa ule, kuelekea maeneo ya makao makuu ya jeshi. Wakati alipokuwa anatizama, bahati nzuri aliona kuna gari moja lilikuwa inatoka karibu na jengo la mauzo, kuelekea mtaa ambao kulikuwa na makao makuu ya jeshi. Alianza kuhesabu dakika za mwendo wa lile gari, hadi kufika mtaa uliokuwa na ofisi za jeshi la polisi.

Wakati macho yake yakiwa kwenye lile gari ambalo lilikuwa linatembea taratibu kwa sababu ya msongamano wa watu, huku akiwa amelikadiria mshale wa kasi wa lile gari, kuwa kwenye namba ishirini; Mara nyuma yake alisikia vishindo vya mtu, ambae ni kama alitua kutoka angani.

Masikio yake yanauwezo wa kutofautisha vishindo vya viumbe hai zaidi ya thelathini, hivyo hakupata shaka kujua vishindo vya kiumbe kilichodondoka nyuma yake.

Taratibu alielekeza macho yake juu, kuona kama kulikuwa na ndege ama helikopita yoyote iliyopita juu.

Ajabu hakuona wala kusikia kelele za miungurumo yoyote kutokea juu.

“Kiumbe gani anaepaa na kutua kwa vishindo vya binaadamu!” Aliwaza huku akianza kugeuka taratibu bila kuwa haraka yoyote.

Naam, macho yake yalikutana na binadamu akimtizama bila kupepesa macho. Binadamu ambae alikuwa ni mrefu na mpana wa mwili, huku akionekana kutozingatia mazoezi kwa sababu, nyama za mikono yake na kifua chake, havikuonekana kupitia kashkashi yoyote ya mazoezi.

Binadamu yule alikuwa ametota maji mwili mzima, huku mgongoni mwake akiwa amebeba kibegi, ambacho kilionekana kuwa na mzigo wa gram chini ya mia sita.

Macho ya Miguu ya Kuku yalimtizama mtu yule kwa umakini, kisha aliamua kutazama nyuma ya mtu yule na, hapo aliweza kuona tank la maji. Tank lile lilikuwa la Lita elfu moja.

“Ina maana mtu huyu katoka kwenye hilo simtank!?” Alijiuliza huku akishangaa peke yake.

Wakati akiendelea kumtazama, kwa haraka haraka alijaribu kupiga hesabu za dakika alizokaa kule juu, ambapo ilikuwa ni zaidi ya dakika saba na, muda wote huo ilimaanisha huyo mtu alikuwa ndani ya hilo tank.

“Inashangaza!” Alijisemea tena huku mara hii akigeuza shingo yake na kuitizama ile gari, ambayo ilikuwa inakaribia kufika usawa wa makao makuu ya jeshi la polisi. Aliondoa macho yake huko na kuitizama saa yake, ambapo aligundua imetumia dakika tano pekee, ikiwa kwenye mwendo wa kawaida sana.

Alirudi kumtizama yule bwana ambae muda wote alikuwa hajasema lolote zaidi ya kumwangalia tu.

“Pole na kazi fundi” Miguu ya Kuku alimwambia yule bwana.

“Wewe ni mhusika hapa?” aliuliza mtu yule kwa sauti ya kukwaruza.

“Napunga tu upepo bwana fundi” Miguu ya Kuku alijibu.

Bwana yule hakujibu kitu, alipiga hatua zake na kuelekea kwenye ngazi na kushuka chini.

Miondoko na macho ya yule mtu, yalimtisha Miguu ya Kuku, pia yalimpa tahadhari kubwa.

“Huyu sio mtu wa kawaida. Dakika saba ndani ya maji!” Alijiwazia huku akirudi kutazama kule kwenye ofisi za polisi.

Alianza kupiga hesabu zake kuhusu mwendo kasi wa magari ya jeshi la polisi, kuwahi kwenye jengo la mauzo baada ya tafrani kutokea.
“Kama mshale wa mwendo uko kwenye namba ishirini na, ametumia dakika tano, basi polisi kwenye mwendo wa dharura watatumia dakika moja na sekunde thelathini, wakiwa kwenye namba hamsini. Sekunde thelathini ni zile kona mbili tatu.” Aliwaza huku bado macho yake yakitizama barabara zilizotoka kwenye kituo cha polisi, kuelekea kwenye jengo la mauzo.

“Lakini polisi wetu huwa wanatumia dakika kumi hadi kumi na tano, kujiandaa kabla hawajaanza safari ya dharura. Dakika hizo hutumia kuitana, kubeba silaha na kupeana majukumu. Hivyo ili wafike kwenye hili jengo, inawahitaji watumie dakika ishirini pekee, japo hata kwa miguu wanaweza kufika ndani ya dakika nane na wakikimbia ni dakika tano. Lakini wakisikia risasi ni lazima waje na bunduki na magari.” Aliwaza tena huku alianza kuondoka na kuelekea chini, akiwa na nia ya kutumia ngazi kushuka chini.
Alitaka atumie ngazi ili ajue muda atakaotumia endapo itamlazimu kuzitumia.

Alipofika ghorofa ya saba, aligundua ofisi za kule juu wakati huo zilikuwa zimefungwa, hivyo kupelekea kuwe na ukimya wa kutisha.

Wakati anakaribia kufika ghorofa ya sita, masikio yake yalisikia vishindo vya mtu mwingine akipanda ngazi na, alipojaribu kusikiliza, aligundua mtu yule alikuwa anapanda ngazi kwa kasi kubwa na upandaji haukuwa wa kawaida.

Haraka na yeye aliziruka ngazi na kudondokea kwenye kibaraza cha ghorofa ya sita, kisha alichumpa na kwenda kujibanza kwenye korido ya moja ya ofisi zilizokuwa pale, kisha alitulia.

Vitendo vyake vilichukua sekunde mbili tu, kukamilisha mpango wake.

Sekunde tano baadae, alishuhudia mtu akipita kwa kasi kubwa, kuelekea ghorofa za juu. Mtu yule alikuwa ni yule aliemuona akiwa ametota maji.

“Baboon!” Alijisemea kivivu.

Akili yake ilimpa tahadhari, mwili wake nao ukakubali kuipokea tahadhari. Sekunde mbili baadae, kisu kilikuwa mkononi mwake na kwa kasi ya ajabu, aliichana kanzu yake katikati ya miguu, kisha akajifunga na kumfanya aonekane kama amevaa vazi la wahindi, jamii ya uddhu.

Lakini yeye pale alikuwa ametengeneza suruali kwa ajili ya dharura aliohitaji kukabiliana nayo.

Alirejesha kisu chake sehemu alipokitoa, kisha aliingiza mkono wa kushoto kwenye mfuko wa kanzu yake na alipoutoa, ilikuwa umeshika kifuko cha karanga kavu. Alikipasua kifuko kile, kisha alitoa karanga chache na kuzitupia mdomoni na, zilizosalia mkononi alizihesabu kwa idadi.

Zilikuwa karanga sita pekee, karanga zile alizitia kwenye mfuko wake wa kulia kisha akakitupa kifuko cha karanga, kikiwa na karanga zake, huku yeye akisalia na zile karanga sita mfukoni na zile za mdomoni akizimeza baada ya kuzitafuna.

Akapiga hatua ndefu kuelekea kwenye kibaraza cha ile ghorofa ya sita, ili apande ngazi kuelekea juu akutane na yule mbabe ambae alikuwa ameelekea huko.

Akili yake ilimwambia mbabe yule alikuwa amerudi kule juu kumuua, hilo hakutaka mbabe yule wa kukaa ndani ya maji, alifurahie.

Wakati mguu wake unakanyaga kwenye kibaraza, huku mkono wake ukijiandaa kudaka chuma cha kujishikiza ili kupanda ngazi, macho yake yalishuhudia kivulia kikija kwa kasi pale alipo.

Hakuzubaa.
Haraka nae alijivuta nyuma hatua moja, huku akimshuhudia yule jamaa akitua chini kama mzimu, baada ya kuruka kutokea kwenye kibaraza cha ghorofa ya saba, ikiwa na maana alitumia zile bomba kuserereka, kisha kujiachia na kutua ghorofa ya sita.

Macho ya Miguu ya Kuku yaliushuhudia mwili mkubwa, ukifanya maajabu.

Walitazamana bila kusemeshana.

Mchapo ukapangwa.

Wakati wao wakidhani walikuwa peke yao kwenye ofisi zilizokuwa ghorofa ya sita, walikosea. Kulikuwa na kiumbe mwingine ambae alikuwa kwenye lile jengo muda mrefu kabla yao, na alikuwa palepale kwenye ghorofa ya sita akiwa amejibanza akiwachora.

Huyu alikuwa ni Tembe za chai, mbabe wa babe.

Kumekuchwa jengo la Mauzo
.
.
.
.
Endelea kuwa nami
Shukran mkuu
 
RIWAYA; MDUNGUAJI WA GOMA.

NA; BAHATI K MWAMBA.

SIMU; 0758573660.


SEHEMU YA NNE.


Macho ya Miguu ya Kuku yaliushuhudia mwili mkubwa, ukifanya maajabu.

Walitazamana bila kusemeshana.

Mchapo ukapangwa.

Wakati wao wakidhani walikuwa peke yao kwenye ofisi zilizokuwa ghorofa ya sita, walikosea. Kulikuwa na kiumbe mwingine ambae alikuwa kwenye lile jengo muda mrefu kabla yao, na alikuwa palepale kwenye ghorofa ya sita akiwa amejibanza akiwachora.

Huyu alikuwa ni Tembe za chai, mbabe wa babe.

Kumekuchwa jengo la Mauzo.

*****

Miguu ya Kuku alirudi nyuma huku mkono wake wa kulia ukiingia kwenye mfuko wake, alipoutoa ulikuwa na karanga moja na, aliitupia mdomoni na kuitafuna huku mfukoni zikisalia tano.

Kiuno cha nyoka baada ya kuona mwenzake anaingiza mkono mfukoni, alidhani anataka kutoa silaha. Haraka alipiga hatua ndefu na kuachia konde maridhawa, lililoenda kutua kwenye bega la kushoto la miguu ya Kuku, baada ya harakati za kukwepa kuzaa matunda hasi.
Konde lile lilimsukuma nyuma hatua kadhaa na kabla hajajipanga, alijikuta akichezea mateke mawili ya mbavu yaliompeleka chini bila kupenda.

Miguu ya Kuku hakufanya haraka kusimama, alimtizama kiuno cha nyoka ambae alikuwa ananesanesa kama Bruce Lee. Alitizama namna alivyokuwa anachanganya miguu yake kwa kasi, huku macho yake yakimtizama bila kupepesa.

Akilini mwake aliafiki kukutana na mtu wa kazi; mnene lakini uzito nyoya.

Alijinyanyua chini kivivu, huku akiingiza tena mkono wake mfukoni na kutoa karanga nyingine na, kuitupia mdomoni. Mfukoni mwake zilisalia nne.

Alinyanyuka huku akiendelea kumshuhudia Kiuno cha nyoka akizidi kurusha miguu yake, mithili ya mcheza dansi za ritungu na zeze.
Aliitafuna karanga huku akijipanga kumkabili adui yake mwenye wepesi wa nyoya. Kwake kuhesabu karanga sita na kuzitia mfukoni, kisha kula moja moja, kulikuwa na maana kubwa sana na kila mara, huo ndio ulikuwa mtindo wake awapo mapambanoni.

Aliitazama tena miguu ya adui yake, kisha akawa kama anahama kutoka kushoto,kwenda kulia, lakini katikati ya safari yake, alirudi haraka upande wa kushoto na, jitu nene uzito nyoya likajaa kwenye hila za mchapo, kisha likaishia kutandikwa konde kali kwenye mbavu zake za kulia na, wakati linageuka ili kujihami, likakutana na konde maridadi kwenye paji la uso kisha, likaachwa litatarike mithili ya mpiga debe alieona bus la Udart, stendi ya Ubungo.

Wakati kiuno cha nyoka anapambana na nyotanyota zilizomzonga usoni, mwenzake aliutumia muda huo kuchukua karanga ya tatu na kuirushia mdomoni, huku mfukoni zikisalia tatu.

Kwa kawaida wakati anapobakiza idadi ya vipande vitatu mfukoni, huwa kinachofuata ni ama adui yake akimbie ama asimame auawe. Lakini anapobakiza vipande vinne au zaidi, hasi adui yake humuacha mzima hata kama atakuwa amemchakaza namna gani.

Sasa kitendo cha yeye kula karanga tatu na kubakiza tatu, ilikuwa ni ama zake ama za kiuno cha nyoka.

Lakini wakati na yeye akijiapiza kumchakaza kiuno cha nyoka, nae mtu mnene uzito nyoya, alikuwa anajiapiza kulipiza mipigo miwili alioipata kutoka kwa hasimu wake.

Mchoro ukachorwa upya na mwenye akili ndiye mshindi.

Mtu mnene aliruka juu na kujikunjua kwa kasi huku, akitanguliza teke mithili ya Van dame, lakini alijikuta akitua chini bila kumpata aliyemkusudia na badala yake alijikuta anatandikwa tena teke la mgongo, lilompeleka chini kifudifudi.
Mtu mnene hakutaka kukawia chini, haraka alijipindua mithili ya mruka viunzi vya Agon, kisha alisimama wima huku akiweka aina nyingine ya kata, ili apambane na mtu mrefu mwenye miguu miembamba mithili ya flamingo.

Wakati yeye akijipanga ili aelewe anapigwaje kirahisi, mwenzake yeye alikuwa anachukua karanga ya nne na kuitupia mdomoni, huku zikisalia mbili mfukoni mwake.

Ni kwa kuwa hakujua ile ilimaanisha nini na, laiti angelijua, basi angetafuta njia nyingine ya kukabiliana na Miguu ya Kuku na si kwa mpambano wa kombati.

Mpambano ulianza tena na katika sekunde kumi za kupashana jab, tayari Miguu ya kuku alikuwa ameenda chini mara mbili, huku pua yake ikianza kutoa damu.

Alizifuta kwa kutumia kiganja cha mkono wake wa kushoto, huku mkono wa kulia ukichukua karanga ya tano na kuitupia mdomoni, mfukoni alibaki na karanga moja pekee na hakutaka iishe bila kufanya alilokusudia na hakutaka iwe mara ya kwanza, kumaliza karanga zote sita, bila kumshinda adui yake.

Miguu ya kuku alipanga pigo linaitwa Capoeira, huku akimshuhudia mtu mnene akiwa ameweka kata za Taekwondo.

Kwa aina za mapigano walizokuwa wamezichora, ilimaanisha wa Taekwondo anatumia mikono, huku wa Capoeira akitumia miguu, kupiga na kupangua misumari ya mwenzake.

Mchezo ukaanza!

Bonge uzito nyoya alianza kushambulia kwa kasi, huku akiwa na nia ya kumaliza mchezo haraka, lakini kila alivyokuwa anaweka ngumi, alikuwa anakutana na hewa. Kila akipiga, alikutana na sehemu tupu; kasi yake ilikuwa ni sawa na kazi bure mbele ya miguu ya Kuku.

Kibao kikageuka, miguu myembamba ilianza kuchapa jitu nene. Kila kiuno cha nyoka alipojaribu kukwepa, aliishia kulambwa makofi ya miguu, huku akipigwa ngumi za sindikiza mwana alale.

Upanguaji wake haukumsaidia na alipangua hadi mikono ikaelemewa, huku akili yake ikishindwa kukubali kasi ya miguu ya Kuku, ambae alikuwa ananesa kulia, anachapa kushoto, yaani ni kama anatema mate kulia, anafukia kushoto.

Miguu ya Kuku alibadili aina ya mapigano, sasa alitaka kumwangusha chini mtu mnene, ilibidi atulie kidogo huku akimalizia kutupa karanga ya mwisho mdomoni, huku akimshuhudia Kiuno cha nyoka akihema kama mbwa koko, aliyekoswa ukoko kwa Mama ntilie.
Alijipanga mtindo wa kumwangusha mtu chini. Mtindo maarufu kwa jina la Hapkido, kisha akatisha kama anaenda kumfuata na ghafla alijiachia chini, huku akitanguliza goti la kushoto chini, kisha aliserereka mithili ya wafungaji wa La liga Hispania, kisha akatanua mikono yake na kwenda kukidaka kiuno cha mtu mnene lakini uzito nyoya. Alipohakikisha amefanikiwa kuondoa nguvu za miguu, akamzungusha kwa ufundi mkubwa bila kujali uzito wa mwili wake, kisha akambwaga chini kama pipa la lami. Hakumkawiza, alimnyanyua tena kama mtu anyanyue kiroba cha mkaa, kisha akambwaga tena huku akiwa bado amekikumbatia kiuno cha nyoka na kumsikia akilia kama kahaba aliesahau pedi kwenye daladala. Akamwinua tena na kumpeleka chini kwa mara ya tatu na lengo lake likiwa linaelekea kutimia, alitaka kumuua kwa kizunguzungu, huku akiwa ameharibu mfumo wa chakula na hewa. Ina maana kama angelimpeleka chini mara tano na kumwachia, basi Kiuno cha nyoka angeliishia kutapika kama Kuku wa mdondo huku uhai ukiagana na mwili.

Wakati anamuinua na kumzungusha ili ampeleke chini kwa mara ya nne, macho yake makali yaliona kivuli cha mtu kikiwa kimejibanza kwenye korido moja wapo ndani ya ofisi zile za ghorofa ya sita na, kivuli kile kilichumpa haraka na kuwapisha waangushane wenyewe, lakini haikuwa hivyo na; badala yake Miguu ya Kuku alimwachia kiuno mwenzake,kisha akamsukuma na teke zito lilomsukuma hadi kwa yule mtu aliyekuwa amejibanza kwenye kona, ambapo walipamiana na kwenda chini kama magunia ya ulezi wa kuumua pombe ya gongo.

Wakati wao wakipamiana na kupiga mweleka, Miguu ya Kuku yeye alikuwa anaruka sarakasi na kuwafuata huku macho yake yakimulika mithili ya kurunzi, za taa nyekundu.
Kiuno cha nyoka licha ya kizunguzungu na kujisikia vibaya tumboni, lakini hakutaka kufa kizembe na baada ya kupamiana na mtu mwingine, haraka alimchapa konde la uchungu mtu yule, kisha akajitoa mwilini mwake na kuangukia pembeni huku akitweta kwa kwikwi zisizo na mfano.

Wakati akiwaza cha kufanya, alimshuhudia miguu ya Kuku akimfuata kwa kasi, kama mmakonde aliyechapwa mshale wa kichwa na wakati huo huo, yule mtu waliepamiana, nae akimfuata kwa jaziba kwa nia ya kumlipiza konde alilomchapa.
“Hata! Siwezi kufa kizembe na hawa mahayawani” Alijiwazia huku mkono wake wa kushoto ukielekea haraka miguuni mwake na, ulipotoka ulikuwa umeshika kitu mfano wa yai la mjusi na kwa wepesi mkubwa, alikirusha chini huku yeye akijinyanyua na kujirusha upande mwingine.

Miguu ya Kuku hakuwa mgeni na aina ile ya mabomu, baada ya kuona likiwa mkononi mwa hasimu wake, haraka alijirusha nyuma kwa kasi huku akimshudia yule mvamizi wa tatu, nae akijirusha chini kwa kasi huku akitoa sauti ya hamaniko, mithili ya kahaba wa Buza aliyefumaniwa na mume wa mzaramo wa Kibada.


Wakati wao wanajirusha kukwepa lile bomu dogo aina ya handalert, ni wakati huo huo bomu lilipotua chini na kulipuka huku likipasua vioo vya milango na, baada ya hapo ving'ora vya tahadhari vikaanza kurindima, baada ya vifaa maalumu kunasa hatari ya moto.

Koki za maji zilianza kutoa maji kwa fujo ili kukabiliana na hatari ile.

Nani abaki wakati taharuki imeanza kutanda ndani ya jengo la mauzo?

Hakuna aliyetaka kubaki, kila mtu alianza kutafuta namna ya kujitoa kule ghorofani bila mwenzake kumfuata.

Kiuno cha nyoka, mtaalamu wa kuruka viunzi, ndiye alieanza kuchomoka kama mshale wa mmang'ati, kisha miguu ya Kuku nae alianza kushuka kwa kasi, lakini kasi yake haikuwa kubwa kama ya kiuno cha nyoka ambae alikuwa anaserereka na kutua mithili ya vampire.

Wakati wao wakitumia ngazi kushuka, Tembe za chai yeye alikuwa anaita kambarau ili imshushe chini haraka, awahi kuwaona wale jamaa kisha na yeye afuate yeyote ambae angeona anafaaa.

Alipofika chini na kuungana na watu wengine kukimbia kutoka nje, tayari wenzake walikuwa wameshafika nje kabisa, walikuwa haraka kuliko kambarau na ndicho alichokitaka.

Yeye alitaka awe wa mwisho ili awasake mmoja mmoja kwa kadri alivyoweza.
Lakini kwa kuwa hakujua watu wa aina gani anaowafuata na laiti angelijua, hizo nguvu angelikwenda kuzitumia kujiandaa kwa ajili ya kuchukua mzigo, ghorofa ya tano.

Lakini kwa kuwa ninge huja baada ya kutokea, alijikuta akiunga mfukuzano wa wababe wale aliotoka kuwashuhudia muda mfupi uliopita.

Moto ukawaka kwenye mitaa ya Lumumba na Posta.

Vita ya watu watatu, ikawa zaidi ya vita vya Waryenchoka na waryenchali Tarime, Mara
.
.

.
.
ENDELEA KUWA NAMI.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom