KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,181
- 17,174
Hivi huyu ni mtu gani asiyekuwa na sura watu wakaona angalao sura yake?Kwa hali hii ya sintofahamu inayoendelea, huyu mtu hadi sasa ni mzima?, Je ameuawa?
Kwa kweli roho yangu inaumia sana yaani imekuwa baridi mno juu ya tukio hili la kutekwa na kutoonekana kwa huyu jamaa!.
What is going on kwa huyu kijana, Je ameuliwa?
Hata CHADEMA hawana kabisa picha yoyote inayomwonyesha, au kuna siri gani hasa inayozuia asionekane. Hata gazeti moja hakuna lililo na picha yake? Ndugu zake waliopotelewa na mtoto wao hawataki sura yake ionekane, labda kuna mtu ambaye anaweza kujua alipo?
Hili pekee ndilo linalonishangaza tokea nilipoanza kusikia habari za kutekwa kwake.