Mdahalo: Tuwapime Magufuli na Lowassa

Mdahalo: Tuwapime Magufuli na Lowassa

Mjadala huu ni wa elimu na viwanda. Mambo ya sura hayapo. Jadili mada

Kwani kuna ilani ya chama chochote iliyokua ikisema , tanzania kutakua na mgao wa umeme kwa kipindi kisichojukana?
Nasema nitawapima na kuwachagua kwa sura zao, sitaki elimi wala viwanda, atae tokea vizuri kwenye picha, atapata kura yangu.
 
Hatupepesi macho hapo LOWASA anamwacha mbali Magufuli!

MAGUFULI - Anavyosema viwanda hakuna serikali inayojengwa viwanda karne hii ila inavutia uwekezaji binafsi sasa mwekezaji kama anaona fursa yenyewe inamlipa ndipo huwekeza. Sera zetu toka enzi za Mkapa ziko wazi juu ya uwekezaji hivyo lugha ya viwanda kila mkoa ni ya kutafutia kura tu. Kumbuka kuwa hv sasa serikali inakusanya kodi toka wawekezaji na si kujenga viwanda.

LOWASSA - Anavyonadi elimu bure kuanzia chekechea hadi chuo kikuu inawezekana kwa kuwa hapo kinachofanyika ni kuziba mianya ya utoroshaji wa kodi ambao hulitia hasara taifa. Kupunguza baraza la mawaziri na naibu waziri na kupunguza ununuzi wa magari ya kifahari.

Okay!! Viwanda ni kutafuta kura tu kwa sababu ya vijana wengi hawana ajira, nimekusoma kidogo mkuu
 
Hivi jiulize...leo hii hatuna wasomi wa kufanya kazi viwandani?jiulize..tatizo kubwa la vijana leo ni ajira inayotatuliwa kwa viwanda.

Kwa wewe unavyofkiria hao wasomi walioko mtaani ni wakemia wangap ambao anaweza fanya kwenye vwanda zaidi ya 60 kaka??
 
Hujui unachosema...hivi hukusikia vijana wenye degree 800 walijitokeza kwenye interview ya uhamiaji kupata wafanyakazi kama 50 hivi?tatizo kubwa letu leo sio wasomi wa kuwaajiri bali ajira za wasomi hao, viwanda ndio jibu kwa sasa.
Hii unayoisema hapo inaitwa Poor mind. Elimu bora Sio kumaliza chuo na kupata vyeti kisha unazurura kutafuta kazi. Halafu mtu anakuja anasema atajenga viwanda(ofisi) vingi ili wapate ajira!!
Huko ni kutumia Uti wa mgongo kifikiria badala ya kutumia ubongo.
Issue ni Elimu, Elimu, Elimu tu.
 
Swali la great thinkers linajibiwa na light thinkers ..lost urgument

Integrity first others comes next, we need good Governance i.e considering 7pillars of good Governance. its so simple to say education or industrialization.

1. Legitimacy
2. Participation
3. Responsible stewardship:
4. Ethical conduct: includes respect, honesty, openness, integrity, trustworthiness
and fairness in all interactions
5. Transparency: requires timely access by electors, shareholders, members and
other key stakeholders to low-cost, relevant, reliable information about finances,
and management of resources,
6. Predictability:
7. Accountability
 
unamaanisha watanzania wakipata elimu yenyewe yenyewe yenye ujazo wa kutosha, utapeli utaongezeka duniani??
hahahahahahahha baba kenya mtanzania akikamatwaga kwa kosa hatakiwagi kutowa maelezo ila sikuwa na maana hiyooooooooo!
 
Wabongo taabu tupu, hawajui serikali ya JK imetengeneza wataalamu wa kutosha, madegree holder n zaidi ya 1M (lets say laki 5 wako vzr kichwan wengine mburura)
Kazi limekuwa suala gumu sana kwa ss na hali itakuwa mbaya zaidi baadae, elimu ilipofikia inatakiwa kuboreshwa tu na maboresho n muendelezo hayataisha, so kama nchi kipambaule kiwe viwanda ili kusababisha nchi isonge mbele haraka zaidi
Kwa nchi ilipofikia inahitaji mchachaka wa maendeleo, anayeweza hiyo kazi n magufuli EL hawez mchakachaka, akitukimbiza itakuwa anafukia mashimo vzr ila wenzake wale vzr
 
Mchango wangu....
Tayari tuna wasomi na wajasiria mali ambao wanaweza kuanzisha viwanda wakiwezeshwa kama anavyosema Magufuli.. Mazingira ya viwanda yapo.. Angalia machungwa na machenza yanavyoozea mashambani kule Muheza na kwingineko..inahitaji kipaumbele na mtaji kuyasindika kutoa juice au kuyaweka ndani ya mabox yahiharibike. Ni sera Inawezekana!

Binafsi nafikiri magufuli kipao mbele chake king'ekuwa viwanda vidogo vidogo ing'eleta sound good kwa wasikilizaji.
 
Mkuu acha ushabiki. Tuambie kuhusu Elimu na Viwanda. Mambo ya vyama na ushabiki weka pembeni

Waache ma light thinkers waogelee mkuu make wao chochote poa tu kanyaga twende
 
Umeme hakuna, hivo viwanda vinaendeshwaje, ndo haya haya ya kilimo cha umwagiliaji wa ubuyu....
"Education is the most powerful weapon wich you can use to change the world" Nelson mandela
 
Elimu kwanza,viwanda vinajengwa na nan kama si wasomi?
Viwanda vinaendeshwa na nan kama si wasomi?
...tayari huyu mwenye sera ya viwanda anatudanganya tu,hivi umeme wakuendesha viwanda uko wp?...halafu anatuambia atavifufua viwanda..nan aliviua?.....30%ya watz ndio wanaonufaika na Umeme kwa nini iko hivyo na tuna zaidi ya nusu karne toka tupate Uhuru?......tatizo hapa n Elimu Elimu Elimu na tafadhali tusidanganyane....Sera ya viwanda tz itasubiri mapinduzi katika Elimu.
 
Ukweli ni kwamba gongo itabaki kua gongo2 hata ubadilishe Chupa haiwezi kua juice, kwahiyo ccm ni ileile walijisemea wenyewe na hapo hata asimame nani bado hakutakua na jipya, na mjue mwaka huu wanachi tumechoka subilini kufungasha mizigo mana tunaweka selekali mpya
 
Wabongo taabu tupu, hawajui serikali ya JK imetengeneza wataalamu wa kutosha, madegree holder n zaidi ya 1M (lets say laki 5 wako vzr kichwan wengine mburura)
Kazi limekuwa suala gumu sana kwa ss na hali itakuwa mbaya zaidi baadae, elimu ilipofikia inatakiwa kuboreshwa tu na maboresho n muendelezo hayataisha, so kama nchi kipambaule kiwe viwanda ili kusababisha nchi isonge mbele haraka zaidi
Kwa nchi ilipofikia inahitaji mchachaka wa maendeleo, anayeweza hiyo kazi n magufuli EL hawez mchakachaka, akitukimbiza itakuwa anafukia mashimo vzr ila wenzake wale vzr

Wapuuzi tu hawa, wao wanahisi ili kiwanda kifanye kazi kinahitaji wataalamu 200 wenye masters kumbe hata wataalamu 5 wanatosha kurun kiwanda. Alafu hii nchi hivi bado tunaongelea mpaka leo tunaongelea watanzania hawajasoma? sentensi ambayo Mwl. Nyerere alikuwa akiisema miaka 40 iliyopita ndo bado tunaisema leo kweli? hivi wasomi tulionao sahivi ndani na walioko nje bado tunakosa wataalamu kama 100 wa kurun viwanda hata 10 tu vipya? any way, inferiority complex bado ni tatizo kubwa sana kwasbabu amabye hajasoma analalamika hana elimu lakini kibaya zaidi hata waliosoma nao hawajiamini kama kweli ni wasomi, na ndo maana wengi hawaaminiki kwasababu hawajiamini hata wao wenyewe
 
Hujui unachosema...hivi hukusikia vijana wenye degree 800 walijitokeza kwenye interview ya uhamiaji kupata wafanyakazi kama 50 hivi?tatizo kubwa letu leo sio wasomi wa kuwaajiri bali ajira za wasomi hao, viwanda ndio jibu kwa sasa.

Usichanganye haya mawili, WASOMI na WALIOHITIMU
 
Binafsi nafikiri magufuli kipao mbele chake king'ekuwa viwanda vidogo vidogo ing'eleta sound good kwa wasikilizaji.
.. Si suala la ku sound good kwa wasikilizaji.. Ni suala la maendeleo na practicality.. Viwanda vidogo huchochea kuzaliwa kwa viwanda vikubwa.. Vilevile tutathimini kwa nini vwanda vingine vilikufa.. ili tudhibiti hali hio!
 
Viwanda ni kimbilio lao ili wazidi kutusomba si wazee wa push up ! Wazee wa nguvu elimu kidogo ila elimu ni kila kitu wekeza ktk elimu raha utaiona huwezi kuwaelekeza watu muda mwingi kama wanaelimu watakuelewa tu!
 
Ndio maana ukaambiwa 1. Elimu, 2. Elimu na 3. Elimu

Maana ya elimu ni kuelimika na kuelimika hakuna shule inayofundisha kuelimika, tatizo la watanzania wengi kwa sahivi si elimu bali kuelimika ..na hili linaletwa na kutokujiamini
 
ELIMU, ELIMU NA ELIMU; Elimu Alpha & Omega

Kuna sababu gani kujenga viwanda then uanze kuhangaika kutafuta skilled manpower ya kuendesha viwanda vyenyewe nchi za nje!! hizi shule za kayumba; kila mtu analalamika tumeua elimu; tumeua elimu! Kujenga viwanda hapa nyumbani kisha ukagenisha ajira ni upuuzi, vijana wetu wanabaki kuwa manamba kama tunavyoona kule Arusha Sunflag na A to Z kwa sababu they are not skilled;; again sio deal!!

Bora kurestore elimu, tukatengeneza skilled manpower base; tukapata wataalamu wetu wenyewe wa kuviendesha at the top level then tukaanza kujenga viwanda, na kujenga viwanda has to be a gradual proccess au staggered; sio nostalgic mayhem driven by cheap political expediency ya kurudisha viwanda tu kama tulivyokuwa navyo 70's na 80s', ni lazima kuweka vipaumbele tunajenga viwanda gani kwanza; huwezi kujenga viwanda vya kusindika mkonge wakati mkonge wenyewe huna!


Priority wise; I give Ed Lowassa 101/100


Lowassa kipao mbele chake namba moja Elimu, namba mbili Elimu na namba tatu elimu.

Magufuli yeye kipao mbele chake Viwanda, Viwanda Tanzania nzima.

Wote hao juu wanaomba kazi kwetu, sisi ndio mabosi wao. Wametuambia watatufanyia hayo tukiwapa ridhaa ya kutuongoza.

Sasa tujadili yupi kati ya hao atakaye weza kutuvusha. Je Elimu itawezekana? Viwanda vitawezekana?

Nondo zenu zitasaidia sana kutushawishi sisi ambao bado atujaamua tumpigie kura nani.

Karibuni kwa mjadala wa maslai mapana ya Tanzania yetu. Mungu ibariki Tanzania, Ibariki Africa


 
Back
Top Bottom