Rais Magufuli aliikuta dola 1 sawa na Tsh 2208 akaiacha dola 1 sawa na Tsh 2315 sawa na ongezeko la Tshs 107

Mwande na Mndewa

JF-Expert Member
Feb 26, 2021
950
2,866
Leo dola 1 sawa na tzs 2500 sawa na tofauti ya tshs 292 toka Hayati Rais Magufuli alivyoondoka (2500 - 2208 = 292) hii inasababishwa na kinachoendelea duniani juu ya dola,hivi sasa mataifa kama China yameanza kutumia pesa yao, Urusi vivyo hivyo na tumesikia habari ya brics(China, Urusi, India, Brazil, South Africa) kukubaliana kutumia sarafu moja, pengine ni mpango wa kuondoa nguvu ya dola duniani, lakini tusijifungie kwenye boksi la mawazo ya sababu hizo tu, twende kwenye sababu za kiuchumi,

Ku-import(kununua vitu vingi kuliko ku-export(kuuza) hili kwenye sababu za kiuchumi ni tatizo namba moja lakini, shida kubwa tumekosa ubunifu kabisa nashauri yafuatayo;-

1. Serikali lazima iwekeze kwenye madini iwe na migodi yake yenyewe.

Yaani watanzania tuchimbe na kuuza dhahabu, gesi, chuma nk Lakini kufanikisha hili ni lazima iwekeze kwenye utafiti wa kutosha nasisitiza utafiti wa kutosha, hii itasaidia kuingiza fedha nyingi za kigeni kwenye nchi yetu hasa uuzaji wa dhahabu.

2. Serikali iboreshe bandari ya Dar es salaam, tusiiuze bali tuwekeze wenyewe kwa kununua vifaa vya kisasa na kufanya kazi 24hrs lakini pia itengenezwe bandari kavu kubwa kabisa Morogoro ili mizigo inapotoka bandarini ipelekwe Morogoro wahusika wa mikoa ya kanda ya ziwa kati na nje ya nchi watachukua mizigo hapo. Hii itaongeza ufanisi wa bandari na kuwavutia wateja zaidi.

3. Serikali ni lazima iwekeze kwenye kilimo na viwanda ili kupunguza uagizaji wa bidhaa nje ya nchi, kwanza kutoa ruzuku kwenye pembejeo zakilimo na kuandaa mazingira wezeshi kwa wazawa kufungua viwanda vya bidhaa zinazozalisha kwa wingi nchini mfano mkonge, pamba, alizeti, chikichi na karafuu, tukifanya hivyo tutaongeza uzalishaji, tutapata fedha nyingi za kigeni na tutaongeza mzunguko wa biashara na fedha nchini.

Tuzungumzie matumizi ya dola kwenye manunuzi ya bidhaa kutoka nje ya nchi importation na sio manunuzi ya ndani ni sawa kuzuia matumizi ya dola kwa manunuzi na malipo ndani ya nchi lakini huwezi kufanya manunuzi ya nje kwa kutumia Tsh, mfanyabiashara akitoka Tanzania kwenda Uturuki kununua nguo atakwenda na dola kwakua ndio pesa unayoweza kuibadili na kupata fedha nchi yoyote duniani kwa urahisi, matumizi ya dola hayaepukiki.

Tuzungumzie reserve yetu ya taifa ukifuatilia data za BOT utaona, hifadhi ya fedha za kigeni Tanzania kwa sasa na baadae inapaswa itosheleze miezi mitano mpaka sita,

Tuzungumzie bibi, babu, Mama na dada wanaovaa nguo, hizo nguo zinatoka China nk
tunahitaji dola kuzinunua na kuzileta hapa Tanzania ili bibi, babu, Mama, Baba, Mimi na wewe tuzinunue na tuzivae.

Tuzungumzie bibi, babu, Mama, Baba, Mimi na wewe tukiumwa tunatumia dawa lakini hatuna viwanda vingi vya dawa, zinaagizwa nje Ili bibi, babu, baba, mama, Mimi na wewe tuzipate ni lazima ziagizwe nje kwa dola.

Tuzungumzie kilimo, bibi, babu, baba, Mama, Mimi na wewe tunahitaji mahindi Ili tupate mahindi tunahitaji mbolea, mbolea zinaagizwa nje ya nchi kwa kutumia dola.

Tuzungumzie usafiri sio? Bibi, babu, baba,Mama,Mimi na wewe Magari, pikipiki nk yanatumia mafuta lakini hatuchimbi mafuta,serikali inatumia fedha nyingi sana (dola) kuagiza mafuta ili bibi, babu, baba, Mama, Mimi na wewe tupande gari kwenda sokoni kununua mahitaji uliyoorodhesha, nadhani nimetumia lugha rahisi kuona thamani ya tshs yetu mbele ya dola.

Nimalizie kihesabu; ina tafsiri ya kuwa, tunatumia sana vitu vya nje kuliko wao kutaka vya kwetu, sijui ni kweli au rasilimali zetu tumezikalia ama sisi ni wajinga,labda tutaamka akija Magufuli mwingine, ila ningekuwa na maamuzi basi biashara zote za kuagiza vitu nje na kuingiza nchini ningezipiga chini na kuwapa kipaumbele wale wote wanaofanya biashara ya kupeleka vitu nje.

Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854

- Bachelor of business administration in International business.

- Master of Leadership and Management.

Recent Publications;-
Assessment on the Effects of Micro-financing on Poverty Reduction.
 
Kabla hujalaumu wala kusifia...
Twende na homework moja...
Wakati Magufuli anaingia Euro ilikuwa kiasi gani kulinganisha na dollars?
Na Leo iko kiasi gani?
Pound?
Rand??

Kabla hatujaanza sema mzalendo wetu alikuwa shujaa mtalalam wa sarafu dunia nzima...hebu tufanye a little bit of research...
Tusije mwishoni kusema kabla ya Magufuli kuingia..bei ya Dhahabu soko la dunia ilikuwa hivi na sasa iko hivi...

Ignorance is bliss
 
Kabla hujalaumu wala kusifia...
Twende na homework moja...
Wakati Magufuli anaingia Euro ilikuwa kiasi gani kulinganisha na dollars?
Na Leo iko kiasi gani?
Pound?
Rand??

Kabla hatujaanza sema mzalendo wetu alikuwa shujaa mtalalam wa sarafu dunia nzima...hebu tufanye a little bit of research...
Tusije mwishoni kusema kabla ya Magufuli kuingia..bei ya Dhahabu soko la dunia ilikuwa hivi na sasa iko hivi...

Ignorance is bliss
Neno
 
Leo dola 1 sawa na tzs 2500 sawa na tofauti ya tshs 292 toka Hayati Rais Magufuli alivyoondoka (2500 - 2208 = 292) hii inasababishwa na kinachoendelea duniani juu ya dola,hivi sasa mataifa kama China yameanza kutumia pesa yao, Urusi
Je umefanya utafiti kwenye mataifa mengine dola imesimama palepale kwa viwango vya miaka ya 80 haijapanda!
 
Kabla hujalaumu wala kusifia...
Twende na homework moja...
Wakati Magufuli anaingia Euro ilikuwa kiasi gani kulinganisha na dollars?
Na Leo iko kiasi gani?
Pound?
Rand??

Kabla hatujaanza sema mzalendo wetu alikuwa shujaa mtalalam wa sarafu dunia nzima...hebu tufanye a little bit of research...
Tusije mwishoni kusema kabla ya Magufuli kuingia..bei ya Dhahabu soko la dunia ilikuwa hivi na sasa iko hivi...

Ignorance is bliss
Yaani wewe hutamani kabisa anatajwa Magufuli katika mema. Kama hamjajifunza kwenye haya ya Bandari ambayo yameshusha kabisa heshima ya nchi basi mnatafuta anguko kuu.

Hata kina Lissu wamekwishamjua mzalendo wa kweli na sasa wanamhubiri majukwaani.

Siasa ni sayansi, bado mnayo nafasi ya kujisahihisha na kwenda kutubu Chato
 
Leo dola 1 sawa na tzs 2500 sawa na tofauti ya tshs 292 toka Hayati Rais Magufuli alivyoondoka (2500 - 2208 = 292) hii inasababishwa na kinachoendelea duniani juu ya dola,hivi sasa mataifa kama China yameanza kutumia pesa yao, Urusi
Asante kwa maelezo mazuri. Hiyo paper yako ni ya mwaka gani, iko kwenye journal ipi, volume namba ngapi, na pages namba zipi , boss.
 
Yaani wewe hutamani kabisa anatajwa Magufuli katika mema. Kama hamjajifunza kwenye haya ya Bandari ambayo yameshusha kabisa heshima ya nchi basi mnatafuta anguko kuu.

Hata kina Lissu wamekwishamjua mzalendo wa kweli na sasa wanamhubiri majukwaani.

Siasa ni sayansi, bado mnayo nafasi ya kujisahihisha na kwenda kutubu Chato
Acha utani bwashee. Kwa hiyo huyo Mbowe ndiye unamuita mzalendo wa kweli?
 
Mzalendo muhimu kuwa kiongozi. Sasa hivi tuwewapa nchi watu wa nje.hawana uchungu wowote na Tanganyika. Akili zao ni kuuza kila kitu. Hawashugulishi ubongo.
Tanganyika haipo, wacheni kujitoa akili, na hakuna kiongozi yeyote tangu Nyerere aliyewahi kuongoza Tanganyika ni Tanzania tu,

Mpaka hapo mtakapoidai Tanganyika na kurudishwa ndio utawazulia watu uongo.
 
Mkuu hariri kwanza andiko lako lina aya za kujirudia rudia sana.

Vitu vingi umegusia vya kitaalamu ila umegusa juu juu sana, hujaeleza unachotaka kueleza.
Anachoeleza ni kwamba Magufuli ni bora kuliko Samia kwa sababu dola ilikuwa rahisi kwa 292 shilingi. Anachosahau ni kwamba wakati wa Kikwete kuja kwa Magu, nayo ilikuwa pungufu kwa 690 shilingi. Mkapa kuja kwa Kikwete pungufu kwa 460, Mwinyi, Nyerere ilikuwa ni chini kabisa.
 
Leo dola 1 sawa na tzs 2500 sawa na tofauti ya tshs 292 toka Hayati Rais Magufuli alivyoondoka (2500 - 2208 = 292) hii inasababishwa na kinachoendelea duniani juu ya dola,hivi sasa mataifa kama China yameanza kutumia pesa yao, Urusi vivyo hivyo na tumesikia habari ya brics(China, Urusi, India, Brazil, South Africa) kukubaliana kutumia sarafu moja, pengine
Mkuu uzi umeshiba nyama za kutosha hongera kwa muda wako,
Nakushauri tafuta mbunge mmoja kilaza ambae ni domo zege pale bungeni umsaidie kummezeshe huu uzi akafunguke, hakika atafungua macho ya walio wengi ktk kadamnasi nae atapata point 3 siku ya kikao cha bunge:
 
Tanganyika haipo, wacheni kujitoa akili, na hakuna kiongozi yeyote tangu nyerere aliyewahi kuongoza Tanganyika ni tanzania tu,
mpaka hapo mtakapoidai Tanganyika na kurudishwa ndio utawazulia watu uongo
Ipo mioyoni kwetu. Kuna watu wana uchungu na mali za Tanganyika.
 
Leo dola 1 sawa na tzs 2500 sawa na tofauti ya tshs 292 toka Hayati Rais Magufuli alivyoondoka (2500 - 2208 = 292) hii ina
0755078854

- Bachelor of business administration in International business.

- Master of Leadership and Management.

Recent Publications;-
Assessment on the Effects of Micro-financing on Poverty Reduction.
Ndugu yangu Chakubanga napenda kukupa taarifa rasmi kwamba Hifadhi ya Dola nchini ipo chini sana kuliko wakati wowote tangu mwaka 1981. Asant.
 
Back
Top Bottom