Mdahalo ITV Bila Profesa Lipumba Na Wengine, Kwanini?

Jamani Maggid alikuwa na hoja katika jambo hili. Binafsi ningependa na wagombea wengine wawepo katika mdahalo huo.
Shida inayonipata na kuleta tofauti kwangu na Maggid ni ile ile. Uandishi wa upande mmoja.

Maggid alitakiwa kabla hajaleta mada yake hapa awe amewasiliana na waandaaji wa mdahalo huo na kuwauliza kwa nini unaitwa mdahalo wakati anayekwenda katika mdahalo huo ni mtu mmoja?

Mdahalo huu haukuwapo wa ghafla. Ulitangazwa kwa siku zaidi ya tatu nadhani. Na ilijulikana ni mtu mmoja atakayekuwepo wala haikuwa siri. Na yawezekana kuna sababu za mantiki kwa nini ni mmoja tu aliyeweza kuonekana au kuthibisha kushiriki na wengine wasishiriki. Maggid kama mwandishi msomi alitakiwa kuwatafuta waandaaji na kuwauliza kabla ya kuja na maandishi yake yasiyotenda haki. Kama Maggid ni mwandishi msomi anajua wazi uandishi wa jinsi hii haukubaliki kitaaluma.

Namshauri Maggid arudi kwanza na kuwatafuta waandaaji, awaulize maswali, then, aje hapa na malalamiko yake with evidence of what he has collected kutoka kwa waandaaji then tu-discuss. Bila hivyo, attacks zote anazopata hapa ni size yake.

Kwanza I doubt hata kama aliusikiliza manake anasema kwenye blog yake kuwa alikuwa njiani kwenda Iringa na alikutana na mlezi wake JK pale Mikumi jamaa pamoja na kuwa ni mgombea lakini Maggid akawekwa kabdo na 'msafara wa mgombea' sasa sijui msafara wa mgombea Slaa naye anaweza kukuweka kando na wewe kutoka kupiga picha.

Yaani pale umejishusha kweli, eti JK alikushangaa uliposimama porini kwenye wanyama wakali ili kumpiga picha. Kweli mapenzi ni makali hayaaa
 
Maggid bwana! Hukusikia kuwa kila mgombea urais angepewa muda wake? Unajua Jmosi ijayo itakuwa ni nafasi ya nani? Je unajua ITV wakati wanatangaza kuwepo kwa kipindi hicho walitumia lugha gani? Walisema mdahalo au Dr. Slaa kujibu maswali live? Maggid umekuwaje siku hizi?
 
Mod Peleka hii mada kwenye Jukwaa la lugha, maana kumbe tunataka kujua ni nini mahojiano na ni nini mdahalo, kule kwenye Jukwaa la Lugha ndo kuna wataalamu wa Kiswahili haswaa. hii issue siyo ya kisiasa itakaaje kwenye jukwaa la siasa?
 
...Nadhani, inawezekana ni utaratibu waliyojiwekea ITV! Na vilevile, nadhani walikosea kuuita "mdahalo"..Inawezekana hayakuwa makosa ya makusudi na inawezekana ilikuwa kutokana na kubanwa kwa baadhi ya wagombea, kama Prof. Lipumba! Hata hivyo, tunaweza kutosheka kwamba ITV wameanzisha mwendo...tunaweza kuwa na "Mdahalo wa Taifa" kwa kuwashirikisha akina Prof. Lipumba, Dr. Slaa, na wengine ili tupate "flavour" ya kweli ya uchambuzi, upembuzi, na uchanganuzi makini wa hoja na mantiki ya mdahalo. Siku mbili, tatu, na au nne zinatosha kabla ya Oktoba 31, 2010. ITV ifanywe kweli tuone ushupavu wa hoja zilizokwenda shule....INAWEZEKANA, ITV ITIMIZE WAJIBU WAKE!!!
 
...Nadhani, inawezekana ni utaratibu waliyojiwekea ITV! Na vilevile, nadhani walikosea kuuita "mdahalo"..Inawezekana hayakuwa makosa ya makusudi na inawezekana ilikuwa kutokana na kubanwa kwa baadhi ya wagombea, kama Prof. Lipumba! Hata hivyo, tunaweza kutosheka kwamba ITV wameanzisha mwendo...tunaweza kuwa na "Mdahalo wa Taifa" kwa kuwashirikisha akina Prof. Lipumba, Dr. Slaa, na wengine ili tupate "flavour" ya kweli ya uchambuzi, upembuzi, na uchanganuzi makini wa hoja na mantiki ya mdahalo. Siku mbili, tatu, na au nne zinatosha kabla ya Oktoba 31, 2010. ITV ifanywe kweli tuone ushupavu wa hoja zilizokwenda shule....INAWEZEKANA, ITV ITIMIZE WAJIBU WAKE!!!


Bwana Maligwa,
Umenena, na nashukuru umenielewa. Naamini waandaaji hawajachelewa kutukusanyia wagombea Urais zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja kwenye mdahalo halisia. Katika wakati huu ni vema tukawekana sawa juu ya nini maana ya mdahalo, mahojiano na mazungumzo. Narudia, tulichokiona jana si mdahalo kwa maana ya mdahalo tunayoifahamu wengi. Yawezekana mahojiano au PR tu, kutangaza sera za chama husika. Binafsi sina tatizo na ujumbe alioutoa Dr Slaa, isipokuwa, ingekuwa na maana zaidi kama angekutanishwa na hoja kinzani kutoka kwa wagombea wengine. Isifike mahali, hii tunayoiiita sasa midahalo ikawa ni midahalo inayotokana na mikutano ya ndani ya vyama- Pale ambapo, mgombea anakutana na tabasamu za wapambe na washabiki wa chama chake wakiwa wameshika bendera na hata matarumbeta. Watamshangilia kila anapomaliza sentesi. Inahusu mambo muhimu kwa taifa letu. Kama Lipumba atahojiwa Ijumaa akiwa peke yake, basi, set up ya mahojiano irekebishwe, na usiitwe mdahalo. Ni mtazamo wangu tu.
 
binafsi nimefaidika sana na mdahalo/maeleza/mahojiano, whatver you decide to call it. nimefurahi sana kuona at last TZ tunapata wagombea wenye uwezo wa hali ya juu wa kuchanganua issues of national interest. for once hatujasikia tu mambo ya kujenga barabara, sijui shule, zahanati, as if those are the only issues!!! Nachukua nafasi hii kushukuru vyombo vya habari na waandaji wa mdahalo.
God Bless TZ.
 
Ndugu Zangu,
Jana tumesikiliza mdahalo, au labda mazungumzo au mahojiano kati ya Dr Slaa ( CHADEMA) na Rosemary Mwakitwange. Mahojiano yaliyoruhusu wengine kuchangia kwa njia ya simu pia.
Tunawapongeza walioshiriki kufanya jitihada zile. Ilitoa fursa kwa sisi wapiga kura kumsikiliza Dr Slaa. Hata hivyo, pungufu kubwa kabisa lililoonekana ni namna waandaaji walivyoandaa mdahalo wa upande mmoja bila kuwashirikisha wagombea wengine wa Urais waliopitishwa na NEC. Maana, ni vema pia tukatofautisha maana ya mdahalo na mahojiano. Kama yale ya jana yalikuwa ni mahojiano tu, hakuna tatizo kwa mgombea mmoja tu kuhojiwa. Lakini kama unaitwa mdahalo, basi, tujadili maana ya mdahalo.

Kama ni mdahalo, basi, ingekuwa ni vema na busara kwa wagombea wengine wa Urais kushiriki. Bila shaka, wagombea wengine nao wana haki za msingi za kupewa nafasi ya kuelezea sera zao na kujibu maswali ya wapiga kura. Hata kama chama tawala, CCM kimeweka wazi kuwa mgombea wao hatashiriki mdahalo, lakini hatujasikia vyama vingine vitoa misimamo kama hiyo.

Wengi wetu tungependa kuona wagombea wengine wa Urais nao wakialikwa, hivyo basi, kupewa fursa ya kuelezea sera za vyama vyao na kuulizwa maswali. Kungetoa fursa ya wagombea hao kushindana kwa hoja pia. Labda kama kuna maelezo ya kuwa wagombea hao walialikwa lakini hawakuitikia mwaliko wa kwenda studioni. Au kuwa gharama za muda wa kurusha hewani mdahalo ziligharamiwa na chama cha mgombea aliyefika kwenye mdahalo/mahojiano. Kama sivyo, basi, waandaaji watakuwa hawakuwatendea haki wagombea na wapiga kura kwa ujumla wao.

Maana, tukianza sasa kujenga tabia ya kubagua wagombea itakuwa ni jambo la hatari sana. Ikumbukwe, tangu Uchaguzi Mkuu wa 1995, tulianza kujenga misingi mizuri ya wagombea kupewa fursa sawa. Kwenye uchaguzi wa mwaka 1995 wagombea wote wa Urais walialikwa kwenye mdahalo uliofanyika kwenye iliyokuwa Kilimanjaro Hotel. Kama inavyoonekana pichani, kulikuwa na Profesa Lipumba, Augustino Mrema, Benjamin Mkapa na Bwana Cheyo. Historia ni mwalimu mzuri. Tujifunze.

Maggid,
Iringa, Jumapili, Oktoba, 24, 2010

call it whatever....mdahalo/majadiliano/mazungunzo............fikra zako zingekuwa na some sense kama ungezileta kabla..............but this is very "reactive" observation..............hii kitu ilijulikana kuwepo some days ago na ulikuwa kimya...............

Anyhow...........waandaaji/ muandaaji nilimsikia vizuri akisema.......leo tutazungumzia mambo kadhaa yaliyopo katika Chadema Manifesto..............na hata mjumbe mmoja alipouliza suala la mgombea binafsi yule dada alimjibu/katisha kuwa hilo jambo halipo ktk Chadema manifesto......pamoja na kuwa Dr Slaa alijibu...........

sidhani kama ingekuwa fair kuuita mdahalo..........kumleta Lipumba or whoever kujadili Manifesto za Chadema pekee.............
 
Maggid,

Ngoja tuangalie upande wa pili, jee kuna lolote ulilojifunza kutoka wenye mdahalo/mahojiano ya jana? Na jee unaweza kusema nini kuhusu mgombea Dr. Slaa? Mwisho, jee unaonaje wazo la CCM kuwanyima wagombea wake kushiriki kwenye midahalo?

Natanguliza shukrani...
 
......................... Maggid kama mwandishi msomi alitakiwa kuwatafuta waandaaji na kuwauliza kabla ya kuja na maandishi yake yasiyotenda haki. Kama Maggid ni mwandishi msomi anajua wazi uandishi wa jinsi hii haukubaliki kitaaluma.......................

Nimependa jinsi ulivyoiweka kwa kutumia neno "kama"............I'm serious
 
Bwana Maligwa,
Umenena, na nashukuru umenielewa. Naamini waandaaji hawajachelewa kutukusanyia wagombea Urais zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja kwenye mdahalo halisia. Katika wakati huu ni vema tukawekana sawa juu ya nini maana ya mdahalo, mahojiano na mazungumzo. Narudia, tulichokiona jana si mdahalo kwa maana ya mdahalo tunayoifahamu wengi. Yawezekana mahojiano au PR tu, kutangaza sera za chama husika. Binafsi sina tatizo na ujumbe alioutoa Dr Slaa, isipokuwa, ingekuwa na maana zaidi kama angekutanishwa na hoja kinzani kutoka kwa wagombea wengine. Isifike mahali, hii tunayoiiita sasa midahalo ikawa ni midahalo inayotokana na mikutano ya ndani ya vyama- Pale ambapo, mgombea anakutana na tabasamu za wapambe na washabiki wa chama chake wakiwa wameshika bendera na hata matarumbeta. Watamshangilia kila anapomaliza sentesi. Inahusu mambo muhimu kwa taifa letu. Kama Lipumba atahojiwa Ijumaa akiwa peke yake, basi, set up ya mahojiano irekebishwe, na usiitwe mdahalo. Ni mtazamo wangu tu.

Maggid

Ita mahojiano hayo kwa jina unalotaka wewe lkn wa TZ tunachotaka ni kusikia sera za wagombea no matter kama watakuja kwa makundi au mmoja mmoja!

By the way why "rafikiyo" tena akiwa ndiye Rais aliyepo madarakani kakataa midahalo na kufanya labda kuwa ndiye Rais wa kwanza incumbent hapa duniani kufanya hivyo?
 
Mipango iliyopo ni kuwaalika pia wagombea wa vyama vingine nao wafanya kama Dr Slaa. mwanzoni mpango ulikuwa ni kuandaa mdahalo wa wagombea wote na CCM walipokataa, ikaonekana si vema kuwaleta wapinzani peke yao kwa sababu watakuwa wakishambuliana wao kwa wao. Ndipo likaja wazo la kumweka kila mgombea peke yake. Wiki ijayo kuna mipango ya kuwaleta wagombea zaidi ingawa kuna tetesi kuwa mipango hii imeshaanza kuhujumiwa. Kwa taarifa yeny ITV imeshaanza kutiw a miskusuko kutokana na kipindi kile cha jana
 
... Lakini kama unaitwa mdahalo, basi, tujadili maana ya mdahalo.
... Kama ni mdahalo, basi, ingekuwa ni vema na busara kwa wagombea wengine wa Urais kushiriki.
,... lakini hatujasikia vyama vingine vitoa misimamo kama hiyo.
Labda kama kuna maelezo ya kuwa wagombea hao walialikwa lakini hawakuitikia mwaliko wa kwenda studioni.
Au kuwa gharama za muda wa kurusha hewani mdahalo ziligharamiwa na chama cha mgombea aliyefika kwenye mdahalo/mahojiano.
Kama sivyo, basi, waandaaji watakuwa hawakuwatendea haki wagombea na wapiga kura kwa ujumla wao.
Mkuu naona habari yako ina presumption nyingi sana, ni vyema ungepata majibu ya maswali yote hayo kwanza kabla ya kuconclude. Lakini cha ajabu pamoja na kutokuwa na majibu ya maswali hayo, naona umeshafikia conclusion hii:
Maana, tukianza sasa kujenga tabia ya kubagua wagombea itakuwa ni jambo la hatari sana.
 
Maggid
Nilikuwa nasoma sana makala zako siku za nyuma na nilikuwa shabiki wako mkubwa. Lakini siku za hivi karibuni nimegundua unaweka masilahi binafsi mbele kuliko ya nchi na nashawishika kuamini kwamba unatumika kwa manufaa ya watu wengine. Kufuatia ilo nimeamua kutosoma jambo lolote kutoka kwako manake naona kama huna jipya tena.
Kuhusu huu mdahalo, sote tunafahamu mhusika mkuu aliyepaswa kuwako katika mdahalo ni JK lakini yeye binafsi na chama chake hawataki kufika kwenye usahili, ili wajieleze na waeleweke kwa wananchi wengi, badala yake wameamua kujitenga na jamii. Kukosekana kwa wagombea wengine sio hoja kubwa na ata kama wangefika wote na mhusika mkuu kutokuwapo sidhani kama ingesaidia kitu. Isitoshe kusema wagombea wakuu wa uchaguzi ni kati ya Slaa na Kikwete walobaki hawana ushawishi mkubwa, lakini sio kwamba hawana umaana. Ushauri wangu labda uwaulize ccm wakupe sababu za msingi kukataaa midahalo.
 
Ni kweli hii ya kumuita Mgombea mmoja ina busara yake, kwa sababu hebu just imagine JK hashiriki mdahalo, halafu Slaa na Lipumba peke yao ndo wanashiriki, matokeo yake wanararuana wenyewe kwa wenyewe kwa hoja kali kabisa, ukizingatia Lipumba has Nothing to loose, inaweza ikamuumiza Slaa wakati mpinzani wake mkubwa yaani Jk akiua tembo kwa ubua tu.

Kwa Hiyo mdahalo wenye tija kwa sasa, ni wa Wagombea wawili wenye nguvu sana, ambao ni Slaa na Kikwete, au wote watatu wawepo, kinyume chake mdahalo hakuna tija, bora ahojiwe mmoja mmoja ili kila mmoja amwage sera zake,wananchi tuchambue wenyewe
 
Ndugu Zangu,
Jana tumesikiliza mdahalo, au labda mazungumzo au mahojiano kati ya Dr Slaa ( CHADEMA) na Rosemary Mwakitwange. Mahojiano yaliyoruhusu wengine kuchangia kwa njia ya simu pia.
Tunawapongeza walioshiriki kufanya jitihada zile. Ilitoa fursa kwa sisi wapiga kura kumsikiliza Dr Slaa. Hata hivyo, pungufu kubwa kabisa lililoonekana ni namna waandaaji walivyoandaa mdahalo wa upande mmoja bila kuwashirikisha wagombea wengine wa Urais waliopitishwa na NEC. Maana, ni vema pia tukatofautisha maana ya mdahalo na mahojiano. Kama yale ya jana yalikuwa ni mahojiano tu, hakuna tatizo kwa mgombea mmoja tu kuhojiwa. Lakini kama unaitwa mdahalo, basi, tujadili maana ya mdahalo.

Kama ni mdahalo, basi, ingekuwa ni vema na busara kwa wagombea wengine wa Urais kushiriki. Bila shaka, wagombea wengine nao wana haki za msingi za kupewa nafasi ya kuelezea sera zao na kujibu maswali ya wapiga kura. Hata kama chama tawala, CCM kimeweka wazi kuwa mgombea wao hatashiriki mdahalo, lakini hatujasikia vyama vingine vitoa misimamo kama hiyo.

Wengi wetu tungependa kuona wagombea wengine wa Urais nao wakialikwa, hivyo basi, kupewa fursa ya kuelezea sera za vyama vyao na kuulizwa maswali. Kungetoa fursa ya wagombea hao kushindana kwa hoja pia. Labda kama kuna maelezo ya kuwa wagombea hao walialikwa lakini hawakuitikia mwaliko wa kwenda studioni. Au kuwa gharama za muda wa kurusha hewani mdahalo ziligharamiwa na chama cha mgombea aliyefika kwenye mdahalo/mahojiano. Kama sivyo, basi, waandaaji watakuwa hawakuwatendea haki wagombea na wapiga kura kwa ujumla wao.

Maana, tukianza sasa kujenga tabia ya kubagua wagombea itakuwa ni jambo la hatari sana. Ikumbukwe, tangu Uchaguzi Mkuu wa 1995, tulianza kujenga misingi mizuri ya wagombea kupewa fursa sawa. Kwenye uchaguzi wa mwaka 1995 wagombea wote wa Urais walialikwa kwenye mdahalo uliofanyika kwenye iliyokuwa Kilimanjaro Hotel. Kama inavyoonekana pichani, kulikuwa na Profesa Lipumba, Augustino Mrema, Benjamin Mkapa na Bwana Cheyo. Historia ni mwalimu mzuri. Tujifunze.

Maggid,
Iringa, Jumapili, Oktoba, 24, 2010

You can call it whatever you wish, lakini bottom line imefikiwa.
 
Ningekuona mtu wa maana kama ungelilia JK awepo naye lakini husemi chochote juu ya hilo.

Mchumia tumbo hajifichi.
 
Maggid,

Ngoja tuangalie upande wa pili, jee kuna lolote ulilojifunza kutoka wenye mdahalo/mahojiano ya jana? Na jee unaweza kusema nini kuhusu mgombea Dr. Slaa? Mwisho, jee unaonaje wazo la CCM kuwanyima wagombea wake kushiriki kwenye midahalo?

Natanguliza shukrani...

Rufiji,

Naamini kabisa, kuwa mahojiano ya jana yamememsaidia Dr Slaa. Lakini, yangemsaidia zaidi kama angepambanishwa na wengine au hata kuulizwa maswali magumu juu ya mitazamo yake na sera za CHADEMA. Na sera ni itikadi, suala la itikadi halikuguswa kabisa. Waandaaji walitakuwa kuwa makini zaidi. Huwezi kuliita chungwa embe halafu ukatarajia watu wote wakubali hilo. Ndio msingi wa mimi kudadisi.

Tunakokwenda tuwe na taasisi huru ya habari itakayokuwa na jukumu la kupanga idadi ya midahalo ya kitaifa kwa wagombea wa nafasi za juu ( Urais) au hata wabunge. Ipange tarehe za midahalo mapema mara kampeni zinapoanza.

Naamini midahalo ni jambo jema. Naamini katika neno huru, fikra huru. Huenda CCM wameamua kutoshiriki midahalo kwa sababu za kimkakati. Kama ni hivyo, huo ni mkakati wa kimakosa. Tunakokwenda CCM wataihitaji midahalo, kuna watakaowashangaa.

Binafsi sina ugomvi na Dr Slaa au mgombea mwingine yeyote wa nafasi ya Urais au Ubunge. Wengine mtabidi muizoee tu staili yangu ya kuandika fikra zangu kwa uhuru. Katika niandikiayo, sijawahi kuficha jina langu na sina sababu ya kufanya hivyo. Najitambua kuwa ni mwanadamu, si malaika. Ninakosea pia, siogopi kuyaona yakiwekwa hadharani yale yaliyo na mapungufu katika maandiko yangu, fikra zangu.

Naamini Dr Slaa ni mwanasiasa mahiri. Nilitambulishwa kwa mara ya kwanza kwa Dr Slaa na ndugu yangu Zitto Kabwe, Julai 2004 pale ofisi za CHADEMA Kinondoni. Sikuwa na mazungumzo marefu na Dr Slaa, lakini first impression yangu ilikuwa ni mtu msikivu na mnyenyekevu. Ni kiongozi mwenye mvuto. Kwa mtazamo wangu, changamoto kubwa anayokabiliana nayo Dr Slaa ni CHADEMA yenyewe. Hili nitalifafanua siku za usoni, nikilifafanua sasa nahofia kuna watakaonijia juu kama moshi wa kifuu. Ni wale wasionifahamu. Wale ambao, ukiandika fikra zako, basi, wanakimbilia kukutafutia kabati lako; CHADEMA, CCM, CUF, Udini na mengineyo. Au la kawaida siku hizi; " Jamaa kanunuliwa na mafisadi". Ni wale waliolisahau kabati muhimu sana; KABATI la TANZANIA. Kwamba, hawajaisha, wale wenye kutanguliza maslahi ya Tanzania KWANZA, hata kama watalazimika kutembea kwa miguu kilomita hamsini.
 
Maggid
Nilikuwa nasoma sana makala zako siku za nyuma na nilikuwa shabiki wako mkubwa. Lakini siku za hivi karibuni nimegundua unaweka masilahi binafsi mbele kuliko ya nchi na nashawishika kuamini kwamba unatumika kwa manufaa ya watu wengine. Kufuatia ilo nimeamua kutosoma jambo lolote kutoka kwako manake naona kama huna jipya tena.
Kuhusu huu mdahalo, sote tunafahamu mhusika mkuu aliyepaswa kuwako katika mdahalo ni JK lakini yeye binafsi na chama chake hawataki kufika kwenye usahili, ili wajieleze na waeleweke kwa wananchi wengi, badala yake wameamua kujitenga na jamii. Kukosekana kwa wagombea wengine sio hoja kubwa na ata kama wangefika wote na mhusika mkuu kutokuwapo sidhani kama ingesaidia kitu. Isitoshe kusema wagombea wakuu wa uchaguzi ni kati ya Slaa na Kikwete walobaki hawana ushawishi mkubwa, lakini sio kwamba hawana umaana. Ushauri wangu labda uwaulize ccm wakupe sababu za msingi kukataaa midahalo.

Miye nilishamshtukia siku nyingiiiii kwamba fani ya uandishi si fani yake kakurupuka na kuivamia tu lakini hana uwezo nayo kabisa maana huishia kujikanyagakanyaga tu na msomaji kushindwa kabisa kuelewa alikuwa anataka kusema nini.
 
Rufiji,

Naamini kabisa, kuwa mahojiano ya jana yamememsaidia Dr Slaa. Lakini, yangemsaidia zaidi kama angepambanishwa na wengine au hata kuulizwa maswali magumu juu ya mitazamo yake na sera za CHADEMA. Na sera ni itikadi, suala la itikadi halikuguswa kabisa. Waandaaji walitakuwa kuwa makini zaidi. Huwezi kuliita chungwa embe halafu ukatarajia watu wote wakubali hilo. Ndio msingi wa mimi kudadisi.

Tunakokwenda tuwe na taasisi huru ya habari itakayokuwa na jukumu la kupanga idadi ya midahalo ya kitaifa kwa wagombea wa nafasi za juu ( Urais) au hata wabunge. Ipange tarehe za midahalo mapema mara kampeni zinapoanza.

Naamini midahalo ni jambo jema. Naamini katika neno huru, fikra huru. Huenda CCM wameamua kutoshiriki midahalo kwa sababu za kimkakati. Kama ni hivyo, huo ni mkakati wa kimakosa. Tunakokwenda CCM wataihitaji midahalo, kuna watakaowashangaa.

Binafsi sina ugomvi na Dr Slaa au mgombea mwingine yeyote wa nafasi ya Urais au Ubunge. Wengine mtabidi muizoee tu staili yangu ya kuandika fikra zangu kwa uhuru. Katika niandikiayo, sijawahi kuficha jina langu na sina sababu ya kufanya hivyo.

Naamini Dr Slaa ni mwanasiasa mahiri. Nilitambulishwa kwa mara ya kwanza kwa Dr Slaa na ndugu yangu Zitto Kabwe, Julai 2004 pale ofisi za CHADEMA Kinondoni. Sikuwa na mazungumzo marefu na Dr Slaa, lakini first impression yangu ilikuwa ni mtu msikivu na mnyenyekevu. Ni kiongozi mwenye mvuto. Kwa mtazamo wangu, changamoto kubwa anayokabiliana nayo Dr Slaa ni CHADEMA yenyewe. Hili nitalifafanua siku za usoni, nikilifafanua sasa nahofia kuna watakaonijia juu kama moshi wa kifuu. Ni wale wasionifahamu. Wale ambao, ukiandika fikra zako, basi, wanakimbilia kukutafutia kabati lako; CHADEMA, CCM, CUF, Udini na mengineyo. Au la kawaida siku hizi; " Jamaa kanunuliwa na mafisadi". Ni wale waliolisahau kabati muhimu sana; KABATI la TANZANIA. Kwamba, hawajaisha, wale wenye kutanguliza maslahi ya Tanzania KWANZA, hata kama watalazimika kutembea kwa miguu kilomita hamsini.


Majid Mjengwa aka Maggid

Mtoto wa Kinondoni Biafra.

Na U-scandinavia wako wote lakini MASJID AL NUR bado inakutawala, unaangalia huyu jamaa anasujudu Ijumaa kama mimi au Jumapili kama Baba mkwe.
 
Back
Top Bottom