Mdahalo: Hakuna wakati katika historia ambapo Zanzibar haikuitegemea Bara

Tangu historia ya kale Visiwa vya Zanzibar zimeishi na kufanikiwa kwa kutegemea bara (eneo la mwambao wa Afrika ya Mashariki) na hata maeneo ya ndani ya Afrika. Kufanikiwa kokote kule kunakotajwa kuhusu Zanzibar kumetokana daima na mahusiano yake ya karibu na bara. Bila Bara Zanzibar haiwezi kufanikiwa hata leo hii. Lakini zaidi mafanikio yake ya huko nyuma yalitokana sana na Zanzibar kuwa na ukuu wa kutawala maeneo ya bara. Haijawahi kufanikiwa bila kuwa na nguvu ya kiutawala au kisiasa huko bara. Hili linaonekana hata leo hii katika MUungano wetu ambapo Zanzibar bado wanaonekana kuwa na maamuzi mengi kuhusiana na bara na wanafanikiwa zaidi kwa mgongo wa bara na sasa wapo wanaotaka izidi kufanikiwa kwa kile wanachokiita "kuondolewa kero za Muungano".

Hata Muungano ukivunjika bado Zanzibar itajikuta inaitegemea bara kwa namna nyingi zaidi - kiuchumi, ongezeko lake la watu, kiusalama n.k Hii ni kweli isiyopingika.

Kubali au kataa.
Nakubali in one way na kukataa in another.

Nadhani zenji imekuwa ikiitegemea na kunufaika na bara kutokana na ukweli kuwa Sultan under "Zanzibar Sultanete",alikuwa akimiliki maeneo makubwa ya mwambao wa pwani ya afrika mashariki.Kwahiyo utegemezi hata wa kiuchumi,kisiasa na kiutawala ulikuwepo na bado upo ndo maana kulikuwepo na mapinduzi nk,ambapo wanamapinduzi hao waliwategemea wabara.

Binafsi naamini tunategemeana,na nina amini pia tutaendelea kufanya hivyo hata kama muungano ukivunjika leo.Ni siasa tu lakini hatuwezi kuacha kutegemeana.

Kwa kumalizia,just kwa wasomaji,ungetuwekea hayo mafanikio yaliyoonekana kuwa yamepatikana kutokana na utegemezi huo,hilo lingesaidia zaidi badala tu ya kuwa vague kusema "mafanikio yao mengi yalitegemea bara"
 
Tunajua Tv ya mwanzo tena ya rangi Zanzibar ilipata msaada kutoka bara ,reli ya mwanzo Afrika mashariki msaada ulitoka bara hata umeme uliokuwa ukiwaka katika redius ya kilomita tano ulitoka Tanganyika(Eneo ambalo hata huko Uingereza walikuwa hawajawahi kueneza umeme kwa eneo lenye ukubwa huo)

Wazee wengine maradhi matupu !
 
Mzalendokimathi, bado hujajibu swali la mada.
Historia unayosema haina mashiko kwasababu kama jina halikuwepo ardhi na watu walikuwepo.

Kwa dunia ya leo kuongelea habari za biashara za utumwa ni kupotoka. Sasa hivi dunia ipo katika enzi nyingine na historia ya karafuu au mane mane haina nafasi. Karafuu zinatengenezwa maabara FYI.

Jiulize, katika globalisation na modern tech ZNZ inaweza kusimama bila bara! hapo ndipo swali lilipo.J
Jikite kwenye mada, nasi tunajikusanya kutoa dozi
 
Mzalendokimathi, bado hujajibu swali la mada.
Historia unayosema haina mashiko kwasababu kama jina halikuwepo ardhi na watu walikuwepo.

Kwa dunia ya leo kuongelea habari za biashara za utumwa ni kupotoka. Sasa hivi dunia ipo katika enzi nyingine na historia ya karafuu au mane mane haina nafasi. Karafuu zinatengenezwa maabara FYI.

Jiulize, katika globalisation na modern tech ZNZ inaweza kusimama bila bara! hapo ndipo swali lilipo.J
Jikite kwenye mada, nasi tunajikusanya kutoa dozi
ZNZ inaweza kabisa kusimama bila Bara. Kwa nini mnafikira hawawezi? sii ndio yaleyale ya mkoloni jamani. ZnZ wanaweza kabisa kusimama pekee tena wanaweza kuwa tishio kubwa sana la bara. hadi leo hii watalii wanokuja nchini huja kwa ajili ya zanzibar zaidi ya Kilimanjaro...

Tuache unafiki wanaweza sana kusimama pekee isipokuwa sisi ndio sidhani kama tunaweza kusimama bila ZnZ kwa sababu hizi kero za Muungano ndizo hutumiwa sana wakati wa harakati za kisiasa bara..Kuna wakti hufikiria hakuna kero za muungano isipokuwa kero hizi ni mpango wa kutuweka wabara pamoja nyuma ya Utaifa wetu ktk mgogoro wa muungano. Let ZnZ go!
 
Kuvuka yale maji kuja bara mbona ni kazi rahisi...ngoja uvunjike ndio tutajua janja ya jusi kuota jua.
 
sizungumzii mapenzi ya Zanzibar kuungana na bara; ninachosema ni kuwa Wazanzibar wanaweza kwenda nje ya Muungano (na inapaswa kuwa hivyo mapema zaidi) lakini ni wao wanaojidanganya kudhania kuwa wanaweza kuishi na kufanikiwa bila bara. Sisi bara tunaweza kuishi na kufanikiwa bila Zanzibar wao hawawezi.
 
sizungumzii mapenzi ya Zanzibar kuungana na bara; ninachosema ni kuwa Wazanzibar wanaweza kwenda nje ya Muungano (na inapaswa kuwa hivyo mapema zaidi) lakini ni wao wanaojidanganya kudhania kuwa wanaweza kuishi na kufanikiwa bila bara. Sisi bara tunaweza kuishi na kufanikiwa bila Zanzibar wao hawawezi.
Hapana wanaweza sana mkuu wangu kwa sababu walikuwepo kabla a muungano na ombaomba kama sisi. Kutegemea siku zote inatokana na kutegemeana. Unalima na kuuza mazao yako unategemea lazima kuwepo na mnunuzi huwezi kusema muuzaji au mnunuzi anamtegemea mmoja wapo wote wanategemeana. Mume kwa mke. mimea, ardhi kwa mvua na kadhalika. Bara pasipo Zanzibar hatuna nchi tutaanza Alif kwa ujiti na pengine itafuatia Wasukuma kutaka kujitenga nao kwa dhahabu yao. Afrika kwa ujumla wake hatuwezi kuendelea pasipo UMOJA WETU. naamini kabisa ktk Pan Africanism ndio njia pekee ya Afrika kujikwamua zaidi ya hapo sisi wote maskini ombaomba na tutaendelea kuwa omba omba sema tu tofauti itakuwa mmoja anavaa suti mwingine kanzu.
 
ZNZ inaweza kabisa kusimama bila Bara. Tuache unafiki wanaweza sana kusimama pekee isipokuwa sisi ndio sidhani kama tunaweza kusimama bila ZnZ.
Duh Mkuu Mkandara...! Yaani pamoja na hatari zote za mawimbi, dhoruba na upepo mkali, hawatulii kwao...wanaaga na kuvuka bahari kuja bara kwa sababu bila wao hatuwezi kusimama! Kumbe wanatupenda kiasi hicho...sisi watu milioni arobaini wa bara hatuwezi kusimama bila watu milioni moja wa Zenji!
Let ZnZ go!
Mbona hapa sasa unajicontradict mwenyewe Mkuu...yaani kama tunawategemea kiasi hicho, how do we let them go? Nadhani all they need to do ni kutu''abandon", si wamechoka kutulea wabara tusioweza hata kusimama peke yetu? What the hell is stopping them au yawezekana you are wrong na ni wao ndio wanaoogopa kusimama peke yao?
 
Duh Mkuu Mkandara...! Yaani pamoja na hatari zote za mawimbi, dhoruba na upepo mkali, hawatulii kwao...wanaaga na kuvuka bahari kuja bahari kuja bara kwa sababu bila wao hatuwezi kusimama! Kumbe wanatupenda kiasi hicho...sisi watu milioni arobaini wa bara hatuwezi kusimama bila watu milioni moja wa Zenji!

Mbona hapa sasa unajicontradict mwenyewe Mkuu...yaani kama tunawategemea kiasi hicho, how do we let them go? Nadhani all they need to do ni kutu''abandon", si wamechoka kutulea wabara tusioweza hata kusimama peke yetu? What the hell is stopping them au yawezekana you are wrong na ni wao ndio wananogopa kusimama peke yao?
@Mag3, siku zote ukimsikia mtu akisema fulani hawezi kuishi bila mimi basi jua ya kwamba yeye ndiye mwenye matatizo. hakuna binadamu anayemtegemea mwenzake isipokuwa tunategemeana. Nyerere mwenyewe alisema Znz kuwepo pale itamletea matatizo na kama angekuwa na uwezo angevisogeza visiwa hivyo mbali baharini tusiwe karibu vile maana ni tatizo. Matatizo hayajaishi leo hii tunakaribia miaka 50 lkn analaumiwa kwa kusema vile tu. Na pengine nikwambie tu ya kwamba wale ndege uwaonao mgongoni mwa Nyati humtegemea Nyati na Nyati huwategemea kudondoa kupe mwilini mwake..

Sisi ni millioni 40 karibu 50 ina maana demand yetu kubwa zaidi ya wao..na maadam sisi maskini kukidhi demand tena nimekosea, inatakiwa niseme sisi sote hatuna demand ila imevuka mipaka na kuwa hii ni dhiki ya uhaba wa kila kitu. Hivyo kuwezesha utawala kuondoa dhiki kwa watu millioni 40 ni vigumu zaidi ya millioni moja. Na amini maneno yangu wakiuza matunda na Karafuu pekee inaweza kuwatoa uhaba wa chakula Wazanzibar kuliko sisi tunaotegemea gasi ilomilikiwa na wageni.

Let ZnZ go inatokana na kujiamini kwangu ya kwamba hawatuhitaji ila tunahitajiana. Na ili na sisi tujifunze kutokuwa na jeuri na ubishi wa maskini jeuri wa kusodoana. Sisi wote ni ombaomba hakuna mwenye nafuu, hivyo haiwezekani kuwa wao wanatutegemea kwa bakuli analoombea JK.. Acha na wao watembeze bakuli lao watapata mlo wa siku maana nyote hamtaki Africa moja.
 
Hadi leo hatujaona kampeni ya kutaka kuvunja Muungano ikianza... hakuna aliyejitokeza kusema Wazanzibar walioko kwenye serikali au utumishi wa MUungano waachie ngazi
 
sizungumzii mapenzi ya Zanzibar kuungana na bara; ninachosema ni kuwa Wazanzibar wanaweza kwenda nje ya Muungano (na inapaswa kuwa hivyo mapema zaidi) lakini ni wao wanaojidanganya kudhania kuwa wanaweza kuishi na kufanikiwa bila bara. Sisi bara tunaweza kuishi na kufanikiwa bila Zanzibar wao hawawezi.
Mkuu orodhesha basi hayo mafanikio na how wameyapata kwasababu ya bara?Itasaidia hapa kwenye mjadala.Lasivyo itakuwa ni ubishi,huyu anasema yes na huyu anasema no bila hata kutaja sababu ama kuweka facts za why yes or why no.
 
Mkandara, Tunajua kabisa wao wanaweza kusimama bila Tanganyika. Waliwahi kufanya hivyo siku za nyuma.
Nini hasa kinawazuia wao kuondoka katika muungano ikiwa wanadai kwa dhati kabisa hauwasaidii, ni udikteta na 'ushetani wa Nyerere' n.k

Pili, kwanini wanataka serikali 3, mkataba, na si kuvunja muungano endapo wanaweza kusimama wenyewe.
Tatu, nini wanachokitaka ndani ya serikali 3 au mkataba ambacho unadhani wanakihitaji ili kutusaidia na ambacho hawataki kusema.
 
Mkandara, Tunajua kabisa wao wanaweza kusimama bila Tanganyika. Waliwahi kufanya hivyo siku za nyuma.
Nini hasa kinawazuia wao kuondoka katika muungano ikiwa wanadai kwa dhati kabisa hauwasaidii, ni udikteta na 'ushetani wa Nyerere' n.k

Pili, kwanini wanataka serikali 3, mkataba, na si kuvunja muungano endapo wanaweza kusimama wenyewe.
Tatu, nini wanachokitaka ndani ya serikali 3 au mkataba ambacho unadhani wanakihitaji ili kutusaidia na ambacho hawataki kusema.
Nguruvi3, Hakuna kiongozi hata mmoja Zanzibar anataka kuvunja muungano - hakuna. Na hakuna kiongozi yeyote Zanzibar anataka leo serikali tatu maana wanajua utata wa serikali tatu, hii ilikuwa sera ya Chadema na CUF waliingia mkenge wakati wanaongoza Upinzani na wanachama wengi bara. Sio leo hii wanaotaka Jumuiya tu ni CUF sio serikali tatu..

Lakini baada ya fikra za hawa Hizbu kukolea vichwani mwa watu ndio unaona hizi habari za kujitenga na umoja wa Wazanzibar, wasichokifahamu ni kwamba CCM ilitumia mbinu ya muafaka ili wapate kurudi madarakani. Hakuna kitu umoja wa Wazanzibar kwa sababu hawana hata moja wanalokubaliana isipokuwa kutazama maslahi ya Zanzibar.. Jambo ambalo sii kosa kabisa na kwa uhakika maslahi ya Zanzibar ni hizi kelele za ku dai kuvunja muungano zinawapa nafasi zaidi na zaidi. Kila wanapodai tunaongeza dau na viongozi wake wanaongezwa vyeo na nafasi.. Kidali pooh!
 
Mkandara,
Nakubaliana nawe kuwa wanachofanya ZNZ ni kutishia ili matakwa yao yaongezeke.
Imefika mahali hakuna sababu ya kuwabembeleza. Tumejitahidi Pan Africanism unfortunate we have wrong partner.

Msimamo wangu ni kuwa tuidai Tanganyika, si kwa kutaka serikali 3 au mkataba bali kuuvunja kabisa.
Kuuvunja kwasababu hatuwezi kubeba mbelo iliyojaa samadi tukijidanganya tunalea.

Hapa ilipofika wenyewe wanasema wamefungua pandora box. Hakuna kitakachofanyika ambacho hatutahoji.
Tutafanya kila kitu tit for tat

LET ZNZ GO ASAP! IF POSSIBLE DEC 31 2012.
 
Tangu historia ya kale Visiwa vya Zanzibar zimeishi na kufanikiwa kwa kutegemea bara (eneo la mwambao wa Afrika ya Mashariki) na hata maeneo ya ndani ya Afrika. Kufanikiwa kokote kule kunakotajwa kuhusu Zanzibar kumetokana daima na mahusiano yake ya karibu na bara. Bila Bara Zanzibar haiwezi kufanikiwa hata leo hii. Lakini zaidi mafanikio yake ya huko nyuma yalitokana sana na Zanzibar kuwa na ukuu wa kutawala maeneo ya bara. Haijawahi kufanikiwa bila kuwa na nguvu ya kiutawala au kisiasa huko bara. Hili linaonekana hata leo hii katika MUungano wetu ambapo Zanzibar bado wanaonekana kuwa na maamuzi mengi kuhusiana na bara na wanafanikiwa zaidi kwa mgongo wa bara na sasa wapo wanaotaka izidi kufanikiwa kwa kile wanachokiita "kuondolewa kero za Muungano".

Hata Muungano ukivunjika bado Zanzibar itajikuta inaitegemea bara kwa namna nyingi zaidi - kiuchumi, ongezeko lake la watu, kiusalama n.k Hii ni kweli isiyopingika.

Kubali au kataa.

Nyani Linapotaka kupazwa miti yote huteleza
 
sizungumzii mapenzi ya Zanzibar kuungana na bara; ninachosema ni kuwa Wazanzibar wanaweza kwenda nje ya Muungano (na inapaswa kuwa hivyo mapema zaidi) lakini ni wao wanaojidanganya kudhania kuwa wanaweza kuishi na kufanikiwa bila bara. Sisi bara tunaweza kuishi na kufanikiwa bila Zanzibar wao hawawezi.

Mwana kijiji tafadhali wafadhilaka wapunda mnyoge mnyoge lakini haki yake mpeni Uliza serekali ya Tanganyika ilipofika mahali ikawa haina pesa za kulipa deni katika Bank ya Dunia kama sikosei au kulikuwa na deni manatakiwa mlilipe kwa waki ule mkawa hamna pesa za kulipa ,Kambarageakamuomba Mzee Aboud jumbe ampe pesa zile ili alipe wakati huo Juma Duni alikuwa waziri wafedha au ni katibu akazitowa zile pesa mkapewa na yeye Juma Duni alibainisha hilo, zile pesa hadi hii leo serekali yako imeshindwa kuzirejesha tafuta makala ya Juma Duni yenye habari hiyo,isitoshe kabla ya vita vya vyenu vya Uganda Zanzibar ilinunuwa kwa pesa taslimu vifaa vya kileo kwa wakati ule kutoka Urusi fatilieni hilo Ubalozi wa Usrusi mliokuwa hamjuwi nikiwa kijana mdogo nimeona kwa macho yangu vile vifaa vikipitishwa kupelekwa welezo kila alfajiri silaha zile ndizo zilizo fanya leo hii muwe wasemaji na wenyenye majivuna Mungu awarehemu Baba zetu na ndugu zetu waliopoteza maisha yao kwa kwa vita visivyo wahusu hatima yake leo sisi ndugu zao tunaona machungu ya ukombozi wao na laiti kama sio Mzee Aboud kunganisha ASP mgeufyata kwani kabla ya hapo mlikuwa silolote si chochote kwenye mamuzi ya Zanzibar na huo Udugu mnaousema kuwa sisi ni Ndugu Bara na Zanzibar yes ndio Udugu wetu mkubwa umefanya na Waisilamu wa zanzibar kuowana na waisilamu wa bara na hata kama pasingekuwapo na Huo Mungano bado still tungekuwa ni ndugu kwani Dini yetu ndio tuwekea udugu huo na sio Mungano ni matokezeo tu ,leo mnawanyanyasa waisilamu wa bara kama mnavyo wanyanya waisilamu wa zanzibar halafu kiungo hicho hicho kilichounganisha zanzibar na bara mnajisifia kuwa eti ni Ndugu
 
nijuavyo mimi katika karne ya 13 Zanzibar iliwa ni Empire na ikiitwa Zenji Empire, hapajatokea empire nyingine yoyote ndani ya africa yote,,sasa wakati huo hata neno tangnyika hakuna, halikuwepo na wala hathubutu mtu kujinasibu kuwa ilikuwepo tanganyika,, tanganyika katika historia ilizaliwa baada ya Berlin conference ambapo kama mataifa mengine ya afrika yaligaiwa mipaka na wazungu ili yatawaliwe na tanganyika ikaangukia ndani ya mikono ya wajerumaji chini ya Germany East Africa Company pamoja na kenya mnamo mwana 1890,,,,na kwa wakati huo Zanzibar ni dola kubwa kushinda madola yoyote africa na wala africa nzima kwa maana ya bara hakukuwa na nchi isipokuwa Egypt nyengine zote zilikuwa ni kingship or kingdoms ndogo ndogo zilizoongozwa na makabila hata neno tangnyika lilitolewa na wajerumani baada ya kuripoti serikali yao tanga manake hadi dar salama wakati huo ilikuwa sehemu ya Zanzibar na pwani yote hadi kilwa sasa ukisema hakuna muda Zanzibar haikuwahi kutegemea bara itakuwa unachekesha na wala hujui usemalo. tanganyika haiwezi kuifikia Zanzibar hata kwa asilimia 10 kama hufahamu waulize wazee wa zamani wakitangnyika wanajua hivyo,,manake historia ya tanganyika baada ya uhuru nyerere aliipiga marufuku ili watangyika wasijue asili yao wapi na badala yake wakawa wanasomeshwa ya kupigania uhuru nyerere, kinyengetile basi.
Zanzibar pato lake kubwa lilikuwa Ivory na slaves, vyote kutoka bara.
Ondokeni haraka nchini kwetu hatuwataki!!!
 
Zanzibar hawatakaa wajue umuhimu wa muungano kwao mpaka siku muungano utakapovunjika bse haitakuwa zanzibar tena bali pemba na unguja
wanajiita wazanzibar bse wako ndani ya muungano nje ya muungano hakuna kitu kama zenji

Hata Singapore walifikiriwa hawataweza kuishi bila kivuli cha Malaysia.

Link Singapore Seen Overtaking Malaysia 45 Years After Lee's Tears - Bloomberg

Seychelles inamtegemea nani? Cape verde inamtegemea nani?

Miafrika tuko wavivu kufikiri. Hata wakiitegemea Bara(Tanganyika) kuna ubaya wowote?

Kwani bara(Tanganyika) inamtegemea nani sasa hivi?

Kwa nini inategemea wengine?

Hata US anakwenda kila kipembe duniani kudondosha mabomu,kumsaka Kony, Kugawa vyandarua, anategemea kukopa China.
Ndio maana ya utandawazi.

Kila nchi inategemea nyengine?

Hata China anapotoa 20 bilion kwa Afrika basi naye anategemea kuvuna maliasili kutoka Afrika pia. Ipo nchi inayojitosheleza duniani?

Mwanakijiji wamekufanya nini hawa wagunya?
 
Mksndara said:
ZNZ inaweza kabisa kusimama bila Bara. Kwa nini mnafikira hawawezi? sii ndio yaleyale ya mkoloni jamani. ZnZ wanaweza kabisa kusimama pekee tena wanaweza kuwa tishio kubwa sana la bara. hadi leo hii watalii wanokuja nchini huja kwa ajili ya zanzibar zaidi ya Kilimanjaro

Mkandara,

..Ikiwa watagundua mafuta au gesi basi hawatatutegemea. vinginevyo nakuhakikishia watatafuta kila namna waendelee kuwa pamoja na Tanganyika.

..kuhusu utalii, mapato ya Tanganyika ktk sekta ya utalii ni around shilingi trilion 1.4, wakati Zanzibar wanaingiza around bilion 163.

..kukumbusha tu, katika bajeti hii ya juzi ofisi ya makamu wa raisi imetengewa kitita cha shilingi bilion 32 mahsusi kwa ajili ya Zanzibar. kabla ya hapo ZNZ waligoma kulipa sh bilion 40+ ambalo lilikuwa deni la tanesco.
 
Back
Top Bottom