Mdada anapokunjia ndita ampendaye atarajie nini?
...Anatakiwa aulizwe mpenzi ni aje leo mbona umeninunia? labda anaweza kufunguka kwa mpenziwe, na akagundua tatizo lilikuwepo ni dogo sana....Mwanamke kudeka ndani ya mapenzi muhimu.
BAK hivi na mwanaume anayekunja ndita huwa ni nini?
Sasa huyo mdada anakunja ndita wakati gani? na hiyo tabia hiyo huwa anamfanyia mpenzi wake tu? na ameanza lini hiyo tabia au ni kawaida yake?
Swahiba wa mdada wadai naye kashikwa pabaya
Ila hizo ni hadaa zake aonekane kama hajapenda sana
Khofu yake akionekana kafa pengine asije kufa kikwelikweli
Hana imani na kijana kama naye anampenda kiuthabiti
Mdada anapokunjia ndita ampendaye atarajie nini?
na nyie wanaume wake / wapenzi wenu wanapowakunjia ndita hebu mjishushe mtafakari mlipokosea mrekebishe maisha yaishe.......
n wewe dada ndita za nini? kama kakukosea si umwambie, na akirudia makosa si umweleze? kama hajirekebishi si uanze?
Inabidi naye aulizwe kulikoni leo? mbona una kisirani hivyo?.....sikulala vizuri usiku wote nilikuwa macho nawaza mafisadi wanavyoimaliza nchi lol!
BADILI TABIA ni sahihi kuomba msamaha kwa kosa ambalo hata hulijui?
Yupo huyu mdada kweli anapendeza sanaaaaaa
Yupo huyu kijana kweli anampenda huyu mdada lol..
Penzi lao laelekea kuwaka na halina kizima moto lakini,
Upo mushkeli katika dimbwi la mahaba yao tarajiwa..
Mdada anapokunjia ndita ampendaye atarajie nini?
Sijui ana deko lipi huyu mdada badala ya kicheko
Kila amwonapo njemba wake huanza kukuda ndita!
Jambo aulizwapo huanza kujibu mazogo bila lengo
Kijana ameghafilika hajui anapendwa au anavumiliwa tu
Mdada anapokunjia ndita ampendaye atarajie nini?
Swahiba wa mdada wadai naye kashikwa pabaya
Ila hizo ni hadaa zake aonekane kama hajapenda sana
Khofu yake akionekana kafa pengine asije kufa kikwelikweli
Hana imani na kijana kama naye anampenda kiuthabiti
Mdada anapokunjia ndita ampendaye atarajie nini?
Njemba sasa imetosheka na udhia sasa yawasha mataa
Mdada kaghafirika hajui la kufanya kwani ndita siyo utu
Kibuti chanukia nami kuwasuluhisha nimeghairi kabisa
Waswahili husema wagombanapo ndugu chukua kapu ukavune
Mdada anapokunjia ndita ampendaye atarajie nini?
Mwanamke mjinga atavunja ndoa kwa mikono yke yeye mwenyewe.
Best inabidi wanawake tupige kura kung'oa mafisadi, manake kumbe wanaathiri ndoa hivi eeh? Tunabembeleza ham'bembelezeki
Exactly Rutashubanyuma chukua kapu ukavune. Hakuna cha kusuluhisha hapo mdada hana raha mapenzini ndio maana anakunja ndita, mkaka shurti atafute sababu ya kukunjiwa ndita. Kama hawapeani raha ya nini kujitia karaha? Uamuzi wanao wenyewe