MCs, Wapiga Picha, Make-up artists n.k na matumizi ya Picha zetu

Feyanga

JF-Expert Member
Jun 27, 2007
223
89
Wakuu, Habari za muda huu?

Leo nakuja kwenu na hii mada ama sijui niite tabia ama vipi. Yaani kumekuwa ni kawaida sasa ya makundi haya: Wapiga picha, watu wa make up, ma-MC, mafundi nguo etc. Yaani wao wanakupa huduma na unalipia na bado wataku-post kwenye Mitandao ya Kijamii (Social Media) kila sehemu.

Kama alikuwa mpiga picha basi utajikuta kila mahali, au kama alikuwa MC wako basi naye atapost picha za sherehe nzima kwa jinsi alivyopiga picha yeye au kuchukua video. Inafika wageni waalikwa mnajikuta huko mitandaoni. Kama alikushonea nguo vivyo hivyo, kama alikupaka makeup naye ni yale yale.

Na kuna wale umenunua nguo, kiatu etc basi kwa kuwa anakujua, siku ukivaa tu hicho kitu labda ukapost bila hata kuwatag. Watakuja hapo “asante kwa kutuchagua” “asante kuturuhusu tukuhudumie” au watachukua picha wakapost kwao na maneno kibao. Je, kama mwenyewe nilikuwa sitaki watu wajue nimenunua kwenu?

Ni nadra kukutana na wanaokuuliza/muuliza mwenye tukio lake kabla hawajapost.

Kwa kweli hii tabia inakera sana, bora hata pangekuwa na makubalino au punguzo la bei katika huduma zao. Mkubaliane kabisa kwamba atatumia picha zako kutafutia wateja hivyo mkubaliane bei kabisa. Sio nakulipa kila kitu halafu mara paaa! picha zimejaa mtandaoni au ukiamka siku inayofuata unakuta familia nzima mpo mtandaoni.

HOJA YANGU:
Jamani hii ni sawa?

Ulinzi wa data upo wapi? Hivi watu wanajua kwamba wana haki juu ya picha/taarifa zao? Hivi wenye matukio wanajua kwamba wanaweza kataa kupostiwa, wanajua ni haki yao kuruhusu au kukataa? Na hao wanaoposti wanajua ni kosa bila ridhaa ya mhusika?

Nini maoni yako?
 
Wakuu, Habari za muda huu?

Leo nakuja kwenu na hii mada ama sijui niite tabia ama vipi. Yaani kumekuwa ni kawaida sasa ya makundi haya: Wapiga picha, watu wa make up, ma-MC, mafundi nguo etc. Yaani wao wanakupa huduma na unalipia na bado wataku-post kwenye Mitandao ya Kijamii (Social Media) kila sehemu.

Kama alikuwa mpiga picha basi utajikuta kila mahali, au kama alikuwa MC wako basi naye atapost picha za sherehe nzima kwa jinsi alivyopiga picha yeye au kuchukua video. Inafika wageni waalikwa mnajikuta huko mitandaoni. Kama alikushonea nguo vivyo hivyo, kama alikupaka makeup naye ni yale yale.

Na kuna wale umenunua nguo, kiatu etc basi kwa kuwa anakujua, siku ukivaa tu hicho kitu labda ukapost bila hata kuwatag. Watakuja hapo “asante kwa kutuchagua” “asante kuturuhusu tukuhudumie” au watachukua picha wakapost kwao na maneno kibao. Je, kama mwenyewe nilikuwa sitaki watu wajue nimenunua kwenu?

Ni nadra kukutana na wanaokuuliza/muuliza mwenye tukio lake kabla hawajapost.

Kwa kweli hii tabia inakera sana, bora hata pangekuwa na makubalino au punguzo la bei katika huduma zao. Mkubaliane kabisa kwamba atatumia picha zako kutafutia wateja hivyo mkubaliane bei kabisa. Sio nakulipa kila kitu halafu mara paaa! picha zimejaa mtandaoni au ukiamka siku inayofuata unakuta familia nzima mpo mtandaoni.

HOJA YANGU:
Jamani hii ni sawa?

Ulinzi wa data upo wapi? Hivi watu wanajua kwamba wana haki juu ya picha/taarifa zao? Hivi wenye matukio wanajua kwamba wanaweza kataa kupostiwa, wanajua ni haki yao kuruhusu au kukataa? Na hao wanaoposti wanajua ni kosa bila ridhaa ya mhusika?

Nini maoni yako?
Ni makosa kama wanafanya hivyo bila kibali cha mhusika mkuu, kwa mhusika unatakiwa kwanza kuwa na mkataba na hao wote wa yale ambayo mnakubaliana kuyafanya likiwemo la kutumia picha zako kwa shughuli ambazo ni binafsi hata kama ni harusi au hata kama ni mshona suti,suti bega lazima akuombe tena kwa maandishi,pia ndio maana haitakiwi mpiga picha wa shughuli yako aweke alama yake kwenye picha zako. Tatizo ni kuwa tunayafanya haya mambo kienyeji sana kunakuwa hakuna hati yoyote ya makubaliano au ya nini kinatakiwa kifanywe ,wewe ukishalipa pesa tu basi mambo kwisha kwa watu makini unatakiwa kuwa na mkataba wa chcohote unachofanya na mteja wako yaani mshereheshaji,mwandaaji,mpiga picha n.k kwenye mktaba mnakubaliana yapi yafanywe na yapi hayatakiwa kufanywa bila idhini yako au idhini yake.
 
Japo wengi wanafanya kwa lengo la the so called kutangaza biashara na kutafuta wateja, kiuhalisia sio sawa ni heri kuwe na makubaliano kabla kuliko kupost bila ruhusa na mkisema mpelekane vyombo vya sheria, watoa huduma wataangukia pua.. Nchi za wenzetu wanafanya hivyo ila huku Kibongobongo tunachukulia poa

Ni madini/elimu nzuri sana mkuu umetoa, kuna rights na obligations ambazo pande zote mbili zinatakuwa kuzifanya na kuzipata...Mkataba wa makubaliano ni muhimu sana, kwa maana kila mmoja wetu anahitaji faragha(privacy) sio wote wanapenda kupostiwa
 
Ni makosa kama wanafanya hivyo bila kibali cha mhusika mkuu, kwa mhusika unatakiwa kwanza kuwa na mkataba na hao wote wa yale ambayo mnakubaliana kuyafanya likiwemo la kutumia picha zako kwa shughuli ambazo ni binafsi hata kama ni harusi au hata kama ni mshona suti,suti bega lazima akuombe tena kwa maandishi,pia ndio maana haitakiwi mpiga picha wa shughuli yako aweke alama yake kwenye picha zako. Tatizo ni kuwa tunayafanya haya mambo kienyeji sana kunakuwa hakuna hati yoyote ya makubaliano au ya nini kinatakiwa kifanywe ,wewe ukishalipa pesa tu basi mambo kwisha kwa watu makini unatakiwa kuwa na mkataba wa chcohote unachofanya na mteja wako yaani mshereheshaji,mwandaaji,mpiga picha n.k kwenye mktaba mnakubaliana yapi yafanywe na yapi hayatakiwa kufanywa bila idhini yako au idhini yake.
Asante mkuu, wengi hatujui haya.
 
Hahaha ungejua wengi wanaomba kupostiwa..yaani maharusi wanamuombaa photographer awape picha za fasta fasta mbili tatu kwa ajili ya kumrushia MC ili azipost.
Hawa haina shida mkuu, kwa wale wanaotaka wenyewe. 😂😂😂 ati Mc awapost
 
Japo wengi wanafanya kwa lengo la the so called kutangaza biashara na kutafuta wateja, kiuhalisia sio sawa ni heri kuwe na makubaliano kabla kuliko kupost bila ruhusa na mkisema mpelekane vyombo vya sheria, watoa huduma wataangukia pua.. Nchi za wenzetu wanafanya hivyo ila huku Kibongobongo tunachukulia poa

Ni madini/elimu nzuri sana mkuu umetoa, kuna rights na obligations ambazo pande zote mbili zinatakuwa kuzifanya na kuzipata...Mkataba wa makubaliano ni muhimu sana, kwa maana kila mmoja wetu anahitaji faragha(privacy) sio wote wanapenda kupostiwa
Shukrani sana. Makubaliano ni muhimu. Pia kutokana hiyo watu kutokujua ama wengine wanapenda hivyo. Ni hakika kuna ambao wanajikuta tu wameshapostiwa na hata kama hataki anakaa tu kimya sababu hajui haki yake ni ipi.
 
Kuna wateja ukiwafanyia makeup pasipo kuwarusha mtandaoni wanakasirika hatari..ingawa ni uungwana kuulizana kwanza.
Kuwarusha😂😂😂😂 na siku hizi watu wa makeup wengi wanafanya kazi na wapiga picha. Tena kuna ile Before n after😂😂😂 mara paaaa watu mtandaoni wanakujadili ulivyovadilika ehh🙌🏿🙌🏿
 
Asante mkuu, wengi hatujui haya.
Mkuu nadhani unakumbuka kuna picha iliwekwa mitandaoni ya mchezaji wa Simba ambayo wako pamoja na mke wake,picha ile haikustahili kuwekwa mitandaoni kwani ilionyesha mke wake ni mtu mzima kuliko mume lakini kumbe ulikuwa ni upotoshaji tu ama wa makusudi au kwa kutokujua,ile picha ilileta taharuki na usumbufu kwa wandnoa hao,laiti kama kungekuwa na makubaliano fulani ili picha isngewekwa mitandaoni, hadi sasa sielewi lengo la aliyeiweka ile picha mtandaoni, tatizo pia hawa wenye visimu wanakuwa na vihere here sana wakipiga tu hao wamerusha ,hilo ni kosa ndio maana kwenye harusi au matukio mengine kunakuwa na tangazo kabisa kuwa hairuhusiwi kupiga picha iwe kwa simu au kifaa kingine kwa mtu ambaye hahusiki wengine huenda mbali zaidi hadi kutoruhusu kuingia na simu ukumbini, hizi simu zimeharibu sana maisha wengine hupiga hadi selfie kwenye majeneza wakiaga marehemu!
 
Wakuu, Habari za muda huu?

Leo nakuja kwenu na hii mada ama sijui niite tabia ama vipi. Yaani kumekuwa ni kawaida sasa ya makundi haya: Wapiga picha, watu wa make up, ma-MC, mafundi nguo etc. Yaani wao wanakupa huduma na unalipia na bado wataku-post kwenye Mitandao ya Kijamii (Social Media) kila sehemu.

Kama alikuwa mpiga picha basi utajikuta kila mahali, au kama alikuwa MC wako basi naye atapost picha za sherehe nzima kwa jinsi alivyopiga picha yeye au kuchukua video. Inafika wageni waalikwa mnajikuta huko mitandaoni. Kama alikushonea nguo vivyo hivyo, kama alikupaka makeup naye ni yale yale.

Na kuna wale umenunua nguo, kiatu etc basi kwa kuwa anakujua, siku ukivaa tu hicho kitu labda ukapost bila hata kuwatag. Watakuja hapo “asante kwa kutuchagua” “asante kuturuhusu tukuhudumie” au watachukua picha wakapost kwao na maneno kibao. Je, kama mwenyewe nilikuwa sitaki watu wajue nimenunua kwenu?

Ni nadra kukutana na wanaokuuliza/muuliza mwenye tukio lake kabla hawajapost.

Kwa kweli hii tabia inakera sana, bora hata pangekuwa na makubalino au punguzo la bei katika huduma zao. Mkubaliane kabisa kwamba atatumia picha zako kutafutia wateja hivyo mkubaliane bei kabisa. Sio nakulipa kila kitu halafu mara paaa! picha zimejaa mtandaoni au ukiamka siku inayofuata unakuta familia nzima mpo mtandaoni.

HOJA YANGU:
Jamani hii ni sawa?

Ulinzi wa data upo wapi? Hivi watu wanajua kwamba wana haki juu ya picha/taarifa zao? Hivi wenye matukio wanajua kwamba wanaweza kataa kupostiwa, wanajua ni haki yao kuruhusu au kukataa? Na hao wanaoposti wanajua ni kosa bila ridhaa ya mhusika?

Nini maoni yako?
***** video production ndio zao hizi, yaani wanachukua video za tukio zima LA shughuli then wakiingia studio kufanya editing wanachuja fresh na kukabidhi kazi then Yale makando kando (Explicit Content) yanatupiwa youtube.
Ndio michezo yao Kina

Mulastar255
 
Wakuu, Habari za muda huu?

Leo nakuja kwenu na hii mada ama sijui niite tabia ama vipi. Yaani kumekuwa ni kawaida sasa ya makundi haya: Wapiga picha, watu wa make up, ma-MC, mafundi nguo etc. Yaani wao wanakupa huduma na unalipia na bado wataku-post kwenye Mitandao ya Kijamii (Social Media) kila sehemu.

Kama alikuwa mpiga picha basi utajikuta kila mahali, au kama alikuwa MC wako basi naye atapost picha za sherehe nzima kwa jinsi alivyopiga picha yeye au kuchukua video. Inafika wageni waalikwa mnajikuta huko mitandaoni. Kama alikushonea nguo vivyo hivyo, kama alikupaka makeup naye ni yale yale.

Na kuna wale umenunua nguo, kiatu etc basi kwa kuwa anakujua, siku ukivaa tu hicho kitu labda ukapost bila hata kuwatag. Watakuja hapo “asante kwa kutuchagua” “asante kuturuhusu tukuhudumie” au watachukua picha wakapost kwao na maneno kibao. Je, kama mwenyewe nilikuwa sitaki watu wajue nimenunua kwenu?

Ni nadra kukutana na wanaokuuliza/muuliza mwenye tukio lake kabla hawajapost.

Kwa kweli hii tabia inakera sana, bora hata pangekuwa na makubalino au punguzo la bei katika huduma zao. Mkubaliane kabisa kwamba atatumia picha zako kutafutia wateja hivyo mkubaliane bei kabisa. Sio nakulipa kila kitu halafu mara paaa! picha zimejaa mtandaoni au ukiamka siku inayofuata unakuta familia nzima mpo mtandaoni.

HOJA YANGU:
Jamani hii ni sawa?

Ulinzi wa data upo wapi? Hivi watu wanajua kwamba wana haki juu ya picha/taarifa zao? Hivi wenye matukio wanajua kwamba wanaweza kataa kupostiwa, wanajua ni haki yao kuruhusu au kukataa? Na hao wanaoposti wanajua ni kosa bila ridhaa ya mhusika?

Nini maoni yako?
Mimi pia ni Mc na mada yako ina hoja nzuri sana, nakufafanulia hivi...... kinachotakiwa kufanyika ni huyo Mc, photographer au mtu wa mavazi aongee na wewe akuombe kuwa ataitumia picha yako kwenye kurasa zake za kijamii kama sehemu ya kutangaza biashara yake, na wewe utataka kuiona hiyo picha/video ili kujiridhisha kwamba haitakuwa yenye kudhalilisha utu wako.

Una haki ya kukataa asiitumie picha yako bila hata kumpa sababu, na akitumia kiburi akaamua kuitumia picha yako bila idhini yako unaweza kumshitaki.......kuna rafiki yangu mmoja Mc aliwahi kuingia kwenye matatizo kwa ajili ya suala kama hilo
 
Ni makosa kama wanafanya hivyo bila kibali cha mhusika mkuu, kwa mhusika unatakiwa kwanza kuwa na mkataba na hao wote wa yale ambayo mnakubaliana kuyafanya likiwemo la kutumia picha zako kwa shughuli ambazo ni binafsi hata kama ni harusi au hata kama ni mshona suti,suti bega lazima akuombe tena kwa maandishi,pia ndio maana haitakiwi mpiga picha wa shughuli yako aweke alama yake kwenye picha zako. Tatizo ni kuwa tunayafanya haya mambo kienyeji sana kunakuwa hakuna hati yoyote ya makubaliano au ya nini kinatakiwa kifanywe ,wewe ukishalipa pesa tu basi mambo kwisha kwa watu makini unatakiwa kuwa na mkataba wa chcohote unachofanya na mteja wako yaani mshereheshaji,mwandaaji,mpiga picha n.k kwenye mktaba mnakubaliana yapi yafanywe na yapi hayatakiwa kufanywa bila idhini yako au idhini yake.
Mamaeee video production wa kibongo ndio zao hizi, yaani wanachukua video za tukio zima LA shughuli then wakiingia studio kufanya editing wanachuja fresh na kukabidhi kazi then Yale makando kando (Explicit Content) yanatupiwa youtube.
Ndio michezo yao Kina Mig 24 Tv

Mulastar255
 
Mimi ni mtoa huduma wa Picha na video, mteja ambae hataki atokee mtandaoni wanasema kabisa na Mimi nakuwa Sina tatizo kabisa Wala sitapost picha zao. Kuna kundi la pili wao watakupiga mkwara kabisa kwamba usipowapost "utakoma", hao ndo nawapost kwelikweli!! Na kuna kundi kubwa hawataongelea kabisa lakini wasipojiona wanahisi hawakupendeza. All in all huwa najitahidi kutumia picha chache sana na pia kutowahusisha wazazi Wala waalikwa.

Ni muhimu kuwa na form ya agreement ambayo moja ya vitu wanatakiwa wajibu ni Kama watapenda/hawatapenda picha zitumike.
 
Back
Top Bottom