Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Baada ya mahubiri marefu,mchungaji aliwaambia waumini wafunge macho ili waombe.Wakiwa wamefumba macho,alizama kwa kapu la sadaka na kuibua pesa kibao,akazitia kwenye mfuko wa koti la suti yake.Alipoinua uso wake,alikutana macho kwa macho na mzee mmoja mchelewevu ambaye ndo kwanza alikuwa ameingia kanisani anatafuta kiti cha kukaa.Mchungaji akasema;HERI YAKE YULE ASIYESEMA KUHUSU YALE ALIYO SHUHUDIA KWA MACHO YAKE.Mzee naye akajibu;MAANA ATAPATA MGAO WAKE BAADA YA MISA KUISHA!