Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mchungaji Peter Msigwa, amesema kuwa thamani yake kama binadamu haijawahi na haitawahi kutegemea vyeo vya kuteuliwa au kuchaguliwa.
Akizungumza katika mahojiano na mtangazaji Neema Msafiri wa Msafiri Online, Msigwa amejibu mapigo kwa wale wanaodai kuwa alihamia CCM ili "akumbukwe" na Rais Samia Suluhu Hassan katika teuzi zinazoendelea. Msigwa ameweka wazi kuwa utambulisho wake uko imara na hautikiswi na ukosefu wa nafasi serikalini.
"Kwa hiyo kukaa hapa kusubiri uteuzi sijui hujateuliwa, hiyo siyo kazi yangu hiyo mimi. Mimi thamani yangu haitegemeani na cheo, cheo hakiongezi thamani yangu wala kutokuwa na cheo thamani yangu haipungui...cheo hakiongezi thamani yangu wala kutokuwa na cheo hakupunguzi identity yangu, identity yangu inabaki pale pale. Kwahiyo maisha yangu hayategemei niwe na cheo au sina cheo", ameeleza.
Mchungaji Msigwa amebainisha kuwa yeye si mwanasiasa wa "kuchukua chochote" kinachowekwa mezani, na kwamba ana uwezo wa kukataa uteuzi ikiwa haendani na utaalamu wake au taaluma yake.
Kwa mujibu wa Msigwa, "cheo kikubwa" anachokifurahia kwa sasa ni kuwa mwanachama wa CCM mwenye kadi, na amewataka Watanzania kumtazama kama mwanasiasa anayesimamia misingi na hoja badala ya kusaka maslahi binafsi kupitia vyeo.
Akizungumza katika mahojiano na mtangazaji Neema Msafiri wa Msafiri Online, Msigwa amejibu mapigo kwa wale wanaodai kuwa alihamia CCM ili "akumbukwe" na Rais Samia Suluhu Hassan katika teuzi zinazoendelea. Msigwa ameweka wazi kuwa utambulisho wake uko imara na hautikiswi na ukosefu wa nafasi serikalini.
"Kwa hiyo kukaa hapa kusubiri uteuzi sijui hujateuliwa, hiyo siyo kazi yangu hiyo mimi. Mimi thamani yangu haitegemeani na cheo, cheo hakiongezi thamani yangu wala kutokuwa na cheo thamani yangu haipungui...cheo hakiongezi thamani yangu wala kutokuwa na cheo hakupunguzi identity yangu, identity yangu inabaki pale pale. Kwahiyo maisha yangu hayategemei niwe na cheo au sina cheo", ameeleza.
Mchungaji Msigwa amebainisha kuwa yeye si mwanasiasa wa "kuchukua chochote" kinachowekwa mezani, na kwamba ana uwezo wa kukataa uteuzi ikiwa haendani na utaalamu wake au taaluma yake.
Kwa mujibu wa Msigwa, "cheo kikubwa" anachokifurahia kwa sasa ni kuwa mwanachama wa CCM mwenye kadi, na amewataka Watanzania kumtazama kama mwanasiasa anayesimamia misingi na hoja badala ya kusaka maslahi binafsi kupitia vyeo.
