Huyu binti amepoteaSalaam,Shalom!!
Akizungumza Leo ibadani, Mchungaji Mbarikiwa amepigia mstari kuwa, kilichomsukuma Christina Shusho kumwacha mumewe Kwa kisingizio Cha huduma, ni umalaya tu na hakuna kingine.
Itakumbukwa, Msanii huyo, hivi karibuni ameendelea kutetea uamuzi wake huo Kwa kuhusishwa kifo Cha mwimbaji WA INJILI aliyeimba wimbo wa Equemme aitwaye Osinach kuwa kifo chake kilitokana na manyanyaso ya NDOA na alitaka kuvunja NDOA ila akazuiwa na viongozi wa Dini yake, ametumia sababu hiyo kutaka kuhalalisha uamuzi wake wa kutengana na mumewe Kwa kigezo Cha huduma.
Mchungaji Mbarikiwa amesisitiza kuwa, hakuna wito wa pekee kama anavyodai Christina Shusho wa kumwacha mume Ili kufuata huduma Bali amesukumwa na Roho ya ukahaba.
Mchungaji Mbarikiwa amedai kuwa huko mbeleni, siku Si nyingi, Msanii huyo ataonyesha wazi anachokificha sasa.
Ninakubaliana na Mchungaji Mbarikiwa kuwa Christina Shusho hayuko sahihi Kwa kauli na vitendo vyake sababu anaingiza Roho ya kuvunja NDOA Kwa wanawake wakristo Walio ndani ya NDOA sababu ni Yeye ni public figure.
Tuendelee kumkemea mtu huyu Ili asilivuruge Kanisa na kuvunja moyo mabinti ambao hawajaolewa kupata HOFU ya changamoto za ndani ya NDOA.
NB: NDOA na iheshimiwe na watu wote, na kifo pekee ndio kitatamatisha mkataba wa NDOA.
Source: Shuhuda za kikosikazi Cha INJILI Tv.
Karibuni🙏
Pia soma
Christina Shusho: Nilimuacha mume nitimize ndoto zangu