Mchumba wangu ana madeni balaa

Mchumba wangu ana madeni balaa

hana madeni...stuka dogooo...huyo ana mabwana kila sehemu ndio maana hataki kuonekana na wewe anasingizia madeni. mwambie unataka mushuke kila sehemu anayodaiwa ukalipe hayo madeni ili kesho mupite kwa raha mustarehe.

stuka dogo....panya road huyooo.
 
mmmmh inawezekana ulipokuwa arusha alikuwa na michepuko mingi so anakuzuga kuwa anadaiwa kumbe anaogopa kugonganisha

umeliona kwa jicho la tatu kama mie nilivyoona....jamaa anaibiwa kimtindo na demu anamdanganya madeni...unajuwa inakuwaje vibwana vyake vikimpigia simu akiwa na mshkaji...demu anakuwa hapokei ukimuuliza vepee anakuambia huyu namjua ananidai ngoja nimchunie.

ahahahaha ... kweli kuishi kwingi kuona mengi na kujifunza vingi pia.
 
Huyo hakufai, ana maisha ya kuiga na hataki apitwe na kitu. Mwanamke mwenye kuendekeza tamaa na kushindwa kujizuia kwa mambo asiyoweza kuyamudu huwa ana sifa ya kukosa uvumilivu na huo ni udhaifu mbovu sana. Hebu Jaribu kumtenga kwa muda, maana pia inawezekana anahangaika kujiweka fresh kwa ajili ya mtu mwingine ambae ni mpya maana kama umekaa nae miaka 9 kwa mwanamke wa kawaida huwa na confidence kuwa unampenda kama alivyo na hawezi kujisumbua kwa ajili ya mwonekano wa nje kiasi cha kukosa amani kama huyo.
 
Nina girlfriend nipo naye kwa miaka Tisa sasa. Nimeanza naye mahusiano akiwa na miaka 19. Nampenda na ananipenda. Namuhudumia vzuri tu. Na tayari nimemchumbia. Zamani hakuwa na tabia za kukopa vitu na kubaki na madeni. Ila sasa imekuwa balaa.

Nilipoingia kwenya ajira nilianzia kazi ofisi zetu za Arusha yeye akabaki Dar na hapo ndipo alipobadili tabia ambayo hakuwa nayo mwanzo. Japo nilikiwa mbali hakuna kilichobadilika kwa kumjali kwa matumizi yake. Ila sijui tabia ya kukopa kaitoa wapi Na nilishamkataza na nikamuambia akiwa na shida ruksa kuniambia na analijua hilo. Ila anapenda tu kukopa.

Baadae nikahamia kikazi kurudi mjini DSM. Yaani kila njia tukipita japo ni ndani ya gari ataniambia hapa tusipite na tukipita usishushe kioo flani ataniaona. Nikimtaiti anasema ananidai nilikopa wigi.

Hii tabia inanishinda sasa. Anadaiwa hadi kwenye vibanda vya baga. Saluni nyingi haendi ameacha madeni. Maduka zaidi ya sita maeneo ya kwao mikocheni anadaiwa. Wanafunzi aliomaliza nao udsm mwaka huu karibia mashosti wake wote wanamdai. Nishafanya juhudi zote kumkataza na kuyalipia madeni yake ila anarudia na anakopa tena.

NIFANYEJE?
DMkuu huyo bibie ana tatizo la kisaikolojia na pengine linatokana na tamaa.
Anahitaji couselling ya uhakika na aelezwe madhara yake kinaga ubaga, na hata ikibidi umtishie kumwacha.
Tabia hii wanayo wanawake wengi tu.
 
inawezekana hayo maeneo hadaiwi ila ana minjemba yake haiwezekani ukae na mtoto wa watu miaka tisa hujamuoa we jamaa kiboko bado siku chache tu iwe miaka kumi uchumba gani huo nyie ndo mnaotafuta kurogwa ebu oa mkuu
 
Hahaha ujinga haunaga mwisho. Hata sie waswahili si tulikuwa tunasubiria amina chifupa afufuliwe na gwajima? sijui hadithi ikaishia wapi hii. Huwa nauliza hawa wachawi waangusha ndege wako bongo tu? Air Malaysia hawazifikii wala BA?

Bora wanawake sasa, ukikutana na mwanaume mjinga hutaamini macho yako. :A S 12:

Hii ni kweli kabisa.

Kuna mama mmoja namjua alifiwa na mdogo wake wa kike zamani kidogo.

Basi akawaongoza ndugu zake [siblings] katika juhudi za kwenda kwa waganga ili waweze kumrudisha [waliambiwa na mganga eti hakufa bali alichukuliwa ng'witunga, ni kama msukule flani hivi] huyo marehemu ndugu yao.

Mwisho wa siku wakaishia tu kuliwa hela zao na huyo ndugu yao wala hakurudi.

Pia, ninadhani hata huu utitiri wa akina ustaadhi wanaobandika matangazo yao kwenye mistimu na miti huwa wanawalenga zaidi akina na mama na akina mama/ wadada ndo wateja wao wakubwa.
 
Duuh mkuu huwa inaanza ugirlfriend na boyfriend, then nadhan baada ya muda automatically mnaenda uchumba...

Ila miaka tisa ya ugirlfriend?
Uchumba hauji automatically bana, kuna taratibu za kufuata. Au mi ndio sielewi haya mambo?

Halafu mnaweza kuwa kwenye mahusiano tangu wadogo. Wengine walianzia primary school kabisa huko. Hiyo miaka isikuogopeshe.
 
Uchumba hauji automatically bana, kuna taratibu za kufuata. Au mi ndio sielewi haya mambo?

Halafu mnaweza kuwa kwenye mahusiano tangu wadogo. Wengine walianzia primary school kabisa huko. Hiyo miaka isikuogopeshe.

Kweli ni lazima kuna vitu vifanyike ili kubadil status au kuiupgrade from uboyfriend tu uchumba.
 
mlete kwangu, sikopeshi wanawake, nawapa pesa bure..
 
Miaka 9? Kuna wanawake wavumilivu sana aise....kupunguza stress mwache akope tu
 
Mkuu mito, hivi mtu anakuwaje na mchumba kwa miaka tisa? Yani mfano walikutana wakiwa
25 kwa 23, hadi sasa wana 34 kwa 32. Tuwahurumie hawa wanawake bwana.

Yaani acha kabisa mkuu, mi mwenyewe hata sielewi vijana wanaogopa nini kuoa!!!!
 
Ngoja tupime uchumba wake na safari za vasco da gama kukaaa angani nafikiri vinashabihiana aiseeee

Point of correction. Vasco Da Gama hakuwahi kutumia usafiri wa anga.
 
Ha haa vasco da gama nadhana yeye ana 10+1 maana juz juz tu alikuwa southafrica

waambie madada wa jf walionifollow kule Instagram wapunguze kasi Zao hasa Yule Nuru Juma, Teacher flani na nanihii nimewaelewa sana.. Lakini kuna mmoja nadhani yule ni dada wa Mjini mjini lakini jina sikutajii
 
😂😂😂😂😂😂uchumba ni zaidi ya kugraduate udaktari,jamaniii hebu muoe ndio dawa ya kupunguza ukopaji
 
Yapo mapepo ya wizi.udokozi.kukopa.uzinzi.ushoga nk. Kama hii tabia hakuwa nayo na ukiongea nae huoni kama anajali au anasikitika ila hawezi kuacha ujue hayo inaerzekana kabisa yakawa mapepo.
Maombi ya nguvu ndio suluhisho.
Ila huo mlango wa uzinzi bila ndoa kwa kisingizio za urafiki ndio unaokaribisha hali hiyo.
Fanya maamuzi sahihi.
 
Ha ha ha...kuna jamaa mmoja mdau wa Bagamoyo aliniambia kuna waganga wawili Bagamoyo wateja wao zaidi ya 90% ni wanawake. Na matatizo yao ni ishu za mahusiano!!!


Yaani tusipokuwa makini tutalishwa mpaka kinyesi

Sio tu msipokuwa makini,bali ni mnalishwa mambo mengi,nyumba ndogo kwa nyumba kubwa ni mapambano tu ya kwa sangoma,mnajipatia cocktail za malimbwata....
 
Ndiyo raha yako Kuwa na mchumba mkopaji usikute hata wewe unamdai.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom