Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,072
- 136,485
Kwenye maombi na kwa waganga ndio kumejaa wanawake. Mmetufanyavso desperate, kuna wadada na elimu dunia kibao wanatapeliwa hadi unashangaa!
Hii ni kweli kabisa.
Kuna mama mmoja namjua alifiwa na mdogo wake wa kike zamani kidogo.
Basi akawaongoza ndugu zake [siblings] katika juhudi za kwenda kwa waganga ili waweze kumrudisha [waliambiwa na mganga eti hakufa bali alichukuliwa ng'witunga, ni kama msukule flani hivi] huyo marehemu ndugu yao.
Mwisho wa siku wakaishia tu kuliwa hela zao na huyo ndugu yao wala hakurudi.
Pia, ninadhani hata huu utitiri wa akina ustaadhi wanaobandika matangazo yao kwenye mistimu na miti huwa wanawalenga zaidi akina na mama na akina mama/ wadada ndo wateja wao wakubwa.