Wanajamvi ni masikitiko na majonzi kwangu na kuumia sana moyo...maana nilitokea kupendana sana na binti mmoja wa kisukuma na hata kutambulishana kwa familia zetu...mwaka jana nimebahatika kupata nafasi ya masomo nchini Afrika Kusini...na mwaka huu niliporejea nchini nimemkuta mchumba wangu tayari ni mjamzito wa miezi mitano...maana nilirudi tu bila kumpa taarifa kuwa narudi kwa likizo, na hapo alihamaki sana kuniona ghafla nyumbani kwao...tayari akiwa na tumbo kubwa.
Basi baada ya salamu na kumuomba kwa upole tutoke ndipo akanisimulia mkasa wote kuwa amepata mimba na muhusika ni mume wa mtu ambaye ni mfanyakazi mwenzake ofisi moja. Binti analia na kuniomba msamaha kwa lililotokea na anataka tuendelee na mipango yetu ya awali. Sikutaka kumwambia chochote zaidi ya kubaki na mshangao wa tukio zima na kuona kama movie ya kibongo.
Wadau kiufipi nipo katika msongo mkubwa wa mawazo na hasa aibu kwa wazazi wangu ambao walimpenda sana huyu binti na kuona ni hazina ya mke mwema katika maisha yangu.
Nawakilisha kwenu wadau kuomba mawazo na uzoefu wenu katika hali ya namna hii...ninyi mnaniambia nini. Shukrani hapa nimeweka kwa ufupi hasa mawazo makuu ya mkasa wenyewe.
Wanajamvi ni masikitiko na majonzi kwangu na kuumia sana moyo...maana nilitokea kupendana sana na binti mmoja wa kisukuma na hata kutambulishana kwa familia zetu...mwaka jana nimebahatika kupata nafasi ya masomo nchini Afrika Kusini...na mwaka huu niliporejea nchini nimemkuta mchumba wangu tayari ni mjamzito wa miezi mitano...maana nilirudi tu bila kumpa taarifa kuwa narudi kwa likizo, na hapo alihamaki sana kuniona ghafla nyumbani kwao...tayari akiwa na tumbo kubwa.
Basi baada ya salamu na kumuomba kwa upole tutoke ndipo akanisimulia mkasa wote kuwa amepata mimba na muhusika ni mume wa mtu ambaye ni mfanyakazi mwenzake ofisi moja. Binti analia na kuniomba msamaha kwa lililotokea na anataka tuendelee na mipango yetu ya awali. Sikutaka kumwambia chochote zaidi ya kubaki na mshangao wa tukio zima na kuona kama movie ya kibongo.
Wadau kiufipi nipo katika msongo mkubwa wa mawazo na hasa aibu kwa wazazi wangu ambao walimpenda sana huyu binti na kuona ni hazina ya mke mwema katika maisha yangu.
Nawakilisha kwenu wadau kuomba mawazo na uzoefu wenu katika hali ya namna hii...ninyi mnaniambia nini. Shukrani hapa nimeweka kwa ufupi hasa mawazo makuu ya mkasa wenyewe.
Sijui mahusiano yenu yalikuwaje, lakini nikiwa kama mwanamke ambaye nimeshakumbwa na dhoruba nyingi ndani ya mahusiano, ni kwamba kuna vitu huwa wanaume mnakosea. Inawezekana moyoni mwako ulikuwa na malengo mazuri kuhusu mahusiano yenu lakini hayakuwa wazi, namaanisha inawezekana haukuwa wazi nini kinafuata baada ya kuwa wazazi wenu wanafahamu mahusiano yenu, na kwa muda gani (committments). Wanawake wengi (na mimi nikiwemo) hatuwezi kuvumilia dilema kwenye mahusiano. Maisha ya kusadikika, hatima yangu kwako iko kinadhalia zaidi kuliko kivitendo. Hali kama hii ikiwepo ni rahisi sana kwa mwanamke kujikuta anatoka nje ya mstari, akiamini huko atapata kile anachokiitaji.
Wakati uko south Africa, mawasiliano yenu yalikuwaje? bado ulikuwa unamuonesha kuwa nafasi yake iko palepale. Siku hizi mawasiliano yamerahisishwa sana, sitegemei ukae SA miezi bila hata kuwasiliana na mwenzio. MAWASILIANO MAWASILIANO MAWASILIANO, ukikaa kimya siwezi kujua unawaza nini, inawezekana umeshaanza maisha mengine huko uliko.
Sio kwamba najaribu kumtetea mchumba wako, la hasha nilichokuwa najaribu kuonyesha ni loop hole gani amabazo usipozizingatia, zinaweza zikasababisha haya yaliyokukuta especially mnapokuwa mbali (long distance relationships)
Wanajamvi ni masikitiko na majonzi kwangu na kuumia sana moyo...maana nilitokea kupendana sana na binti mmoja wa kisukuma na hata kutambulishana kwa familia zetu...mwaka jana nimebahatika kupata nafasi ya masomo nchini Afrika Kusini...na mwaka huu niliporejea nchini nimemkuta mchumba wangu tayari ni mjamzito wa miezi mitano...maana nilirudi tu bila kumpa taarifa kuwa narudi kwa likizo, na hapo alihamaki sana kuniona ghafla nyumbani kwao...tayari akiwa na tumbo kubwa.
Basi baada ya salamu na kumuomba kwa upole tutoke ndipo akanisimulia mkasa wote kuwa amepata mimba na muhusika ni mume wa mtu ambaye ni mfanyakazi mwenzake ofisi moja. Binti analia na kuniomba msamaha kwa lililotokea na anataka tuendelee na mipango yetu ya awali. Sikutaka kumwambia chochote zaidi ya kubaki na mshangao wa tukio zima na kuona kama movie ya kibongo.
Wadau kiufipi nipo katika msongo mkubwa wa mawazo na hasa aibu kwa wazazi wangu ambao walimpenda sana huyu binti na kuona ni hazina ya mke mwema katika maisha yangu.
Nawakilisha kwenu wadau kuomba mawazo na uzoefu wenu katika hali ya namna hii...ninyi mnaniambia nini. Shukrani hapa nimeweka kwa ufupi hasa mawazo makuu ya mkasa wenyewe.
Mke mwema hutoka kwa Bwana, muombe Mungu atakuonyesha njia!
Yani pamoja na story ndeeeefu naona we ndo unaleta movie ya kibongo sasa.Sikutaka kumwambia chochote zaidi ya kubaki na mshangao wa tukio zima na kuona kama movie ya kibongo.
Aha aha acha masihala!Muoe na mimba akizaa unatundika ya kwako sasa.
Bado hajajifungua anakaribia sasa panapo majaliwa!Hivi Mkuu huyu mchumba wako ni ana ujauzito wa mme wa mtu au amezaa na mume wa mtu?
Zejame...mapenzi ni zaidi ya kula na kunywa!tunaweza kukushauri kumbe huyo dada ndo anakuweka mjini.ooh majanga mbona majanga
Ila mpime kwanza afya maana inawezekana ametembea peku pia na watu wengine tofauti.