Mchumba wangu amezaa na mume wa mtu!

Mchumba wangu amezaa na mume wa mtu!

Mkuu pole sana. Usitumie hisia katika hili, tumia akili zaidi. Jaribu kufikiria mchakato mzima hadi akapata mimba,inaonekana walianza mbali, kutoka kutongozana,kukubaliana, kuwekeana miadi, kukutana,na hatimae kubadilishana hardware za maungo yao.koooooote huko alikuwa hajui kama ana mchumba?
Imani yangu ni kuwa kwa kipindi chote hicho mlikuwa mnawasiliana na alikuficha, je unadhani ni mtu wa kumuamini tena huyo?
Fahamu kwamba baba wa huyo mtoto atakuwa na haki juu ya mwanawe na pia atakuwa na jukumu la kujadili na kupanga mustakbali wa mwanawe kwa kushirikiana na mama wa mtoto ambaye ni mchumba wako. Je upo tayari kuyabeba hayo katika maisha yako yote? Upo tayari kumkaribisha mume mwenzio sebuleni kwako akija kumuangalia mwanawe?upo tyari kumuacha sebuleni mchumba wako na mume mwenza wakijadili yahusuyo mtoto wao?kaka wanawake wenye sifa za kuwa wake wapo ila inategemea tu namna unavyowatafuta, mrudie mungu akuongoze katika kutafuta mke mwenye sifa sahihi za kuwa mke bora, huyo mama kijacho msahau kabisa.
 
Hakuna muda wa kufikiria mara mbili katika hilo...

Hiyo ni ishara kuwa she wasn't yours, hivi unajua hadi mwanamke ashike mimba si kitu cha bahati mbaya atii...kama kuvua tu chupi tena kwa mpenzi huwa wanajiuliza mara mbili mbili, imagine kuvua chupi kwa mtu baki na kumruhusu aweke mimba huko...
 
tafuta mwingine uanze upya, au upo tayari kumuoa mtu ambaye ushajua sio mwaminifu,la swala la mtoto wa kidume mwenzako lazima litaleta shida uko mbele
 
Mpenzi akisafiri safari za zaid ya miez 3 mpe mimba kabisa ndio uondoke. Akigegedwa huko aagh we umeshaweka chako unakuwa na guarantee.

Sasa poti unaenda S.A afu mzigo uko
nyuma? Hahahahah lawama ni kwakowenyewe pole
 
Misongo mingine ya mawazo ya kujitakia, sasa mtu ana mimba ya mwanamme mwenzio wee unasongoka nini?

Kama una kifua beba mwanamke na mtoto wake, kama huuna kifua tafuta mwingine uanze upya.

Afu unawaonea aibu wazazi wako, umekuwa mwali au ulikuwa unawaolea wao? Grow up!

Na kuzaa hakumfanyi huyo dada moja kwa moja asiwe mke mwema, labda alizidiwa na 'ash.ki' tu.
Kongosho!
linapokuja suala hilo mimi nakuwa na bifu na ushauri wako.
Siufiki,
Ingawa unakuwa na ushuhuda wa ndani.

Bazazi!
 
Last edited by a moderator:
Misongo mingine ya mawazo ya kujitakia, sasa mtu ana mimba ya mwanamme mwenzio wee unasongoka nini?

Kama una kifua beba mwanamke na mtoto wake, kama huuna kifua tafuta mwingine uanze upya.

Afu unawaonea aibu wazazi wako, umekuwa mwali au ulikuwa unawaolea wao? Grow up!

Na kuzaa hakumfanyi huyo dada moja kwa moja asiwe mke mwema, labda alizidiwa na 'ash.ki' tu.
point ya addition...huwezi mlazimisha kunguru awe njiwa...au anataka aletewe na wa pili na wa tatu?
 
Kula kona ndugu hakufai mwaka tu tayari keshabebeshwa halafu mbebeshaji yupo ofisi moja na pengine ana mshiko unaoeleweka usisubiri maumivu yajayo haya yanatosha msahau na ng'ang'anaa na kitabu kwanza mpaka kieleweke vyenginevyo utakosa yote
 
Kuna watu wanawaza hata hili, mbona mna mioyo migumu sana? Binafsi hapo ndio ingekua mwisho wa kuonana, kuwasiliana na kila kitu. Mtu kaanza kutembea na jamaa mwingine hajakwambia, kabeba mimba hajakwambia na bado unawaza kuendelea nae. Vp usingerudi like 3yrs ingekuaje? Angekwambia ukweli kwa simu afu akuombe ukirudi umuoe? BS

kwanza hata nafasi ya kuongea nae hamna tena,,, tumbo lake ushahidi kwamba amezinika,,, eti ushauri,,, wa nini sasa...close the deal man.....refresh....kip moving....
 
Yani umemkamata mwizi/Jambazi sugu halafu unauliza watu nimfanyaje....? Watu wa ajabu kweli....
 
Achana nae, tazama mbele. Hicho ni kipimo bora kabisa kwa mustakabali mwema wa maisha yako ya baadae. Hakuna love isiyokuwa na maumivu, hivyo unapitia kipindi hicho cha maumivu, JIEPUSHE.
Nami ningempa ushauri kama wako. Kashaona kwa macho yake kwamba mwenzake sio mwaminifu, je anatarajia kwamba akiingia kwenye ndoa atabadilika? Huyu mwanaume anastahili kufungwa jiwe la kusagia nafaka na kutoswa baharini
 
rekebisha hicho kichwa cha habari, umemkuta mjamzito unasemaje amezaa....?
Wanajamvi ni masikitiko na majonzi kwangu na kuumia sana moyo...maana nilitokea kupendana sana na binti mmoja wa kisukuma na hata kutambulishana kwa familia zetu...mwaka jana nimebahatika kupata nafasi ya masomo nchini Afrika Kusini...na mwaka huu niliporejea nchini nimemkuta mchumba wangu tayari ni mjamzito wa miezi mitano...maana nilirudi tu bila kumpa taarifa kuwa narudi kwa likizo, na hapo alihamaki sana kuniona ghafla nyumbani kwao...tayari akiwa na tumbo kubwa.

Basi baada ya salamu na kumuomba kwa upole tutoke ndipo akanisimulia mkasa wote kuwa amepata mimba na muhusika ni mume wa mtu ambaye ni mfanyakazi mwenzake ofisi moja. Binti analia na kuniomba msamaha kwa lililotokea na anataka tuendelee na mipango yetu ya awali. Sikutaka kumwambia chochote zaidi ya kubaki na mshangao wa tukio zima na kuona kama movie ya kibongo.

Wadau kiufipi nipo katika msongo mkubwa wa mawazo na hasa aibu kwa wazazi wangu ambao walimpenda sana huyu binti na kuona ni hazina ya mke mwema katika maisha yangu.

Nawakilisha kwenu wadau kuomba mawazo na uzoefu wenu katika hali ya namna hii...ninyi mnaniambia nini. Shukrani hapa nimeweka kwa ufupi hasa mawazo makuu ya mkasa wenyewe.
 
pole mkuu kwa janga lililokupata
aachana nae hakutaka kuolewa nawe
waeleze ukweli wazazi wako
 
Mkuu achana nae usije mkuu kama ameweza kucheza bila helment na mume wa mtu akujua kama mchumba wake upo usije ukamlaumu mungu wakati kashakupa jibu huyo ni msaliti piga buku ukirudi wapo kila siku wanazaliwa
 
Mi naamini mungu alitaka kumuumbua ili uone maovu yake kabla hamjaoana,inavyoonekana hajatulia na atakusumbua hata mkioana,fikiria hata mkiwa hapa lakini kazi zikawaweka mikoa tofauti itakuwaje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom