Tatish01
Member
- Mar 26, 2014
- 38
- 5
Hapa ndo huwa nashindwa kuwaelewa hawa madogo wasaka kaazi wa siku hizi wasiojiamini.... Mkiishi kwa kuamini kila kitu kwamba atapata mtoto wa kigogo NI UJINGA MTUPU. Na sijui shule inawasaidia nini...
Ngoja nikuulize maswali mawili tu, halafu jijibu.
1. Naamini kwenye interview walikuwepo vijana wengi, na naamini sio wote ulisoma nao au unawajua, sasa umejuaje kwamba watoto wa vigogo waliangukia pua na nyinyi watoto wa magogo au miti kamili mlifaulu??
2. Umejuaje kwamba fulani ni mtoto wa hicho kigogo na mwingine ni mtoto wa mti?? Uliwauliza wote??
Acheni habari zenu za kulalama majukwaaani.... Jiamini katika usaili.. Hata mimi baba na mama yangu ni wafanyakazi wa kada ya mwisho serikalini hawana hela na hawamjui yeyote, lakini nimefanya interview na kufaulu zaidi ya sehemu tatu sensitive hapa nchini (makampuni yanayolipa zaidi hapa nchini) bila kuhonga hata shilingi.. Na interview moja unakuta wameomba watu hadi elfu moja.. Lakini tunafanya saili za kutosha na tunashinda..
Yaani ulichoandika hapa ni sawa na vile ulivyokimbia panya road na kujificha uvunguni mwa bajaji... Vijana wa kiume wa Dar bana..
Kweli kabisa inabid tujiamin,tuondoe haya mashaka mashaka,watu wanapga pepa wanasonga mbele,tukiwa hatujiamin hata hyo interview hatuwez fika mbali