Mchemsho wa TANESCO? Nchi nzima haina umeme

Sasa Raisi asipowajibisha mtu hapo nitaona kwa kweli yeye ndio awajibike. Huu ni upuuzi. Au ma Co-president wanafanya mambo?
 
Hatujui tuendako kwa sababu tupo gizani, tumekuwa gizani kwa miaka karibu mitatu na upo uwezekano tutaendelea kuwa gizani kwa karibu miaka mingine miwili. Katika muda huo tumeshuhudia juhudi za kila wanaojaribu kututoa gizani zikibezwa na wale ambao kubaki kwetu gizani ndio salama yao. Mabaunsa wenye sura za kutisha na wenye misuli iliyojengeka wamekaa milangoni kuhakikisha hatoki mtu. Mwanga, utakaomulika hata yale yanayowezekana tu gizani kama rushwa, hujuma, ufisadi na maovu yote yanayofanyika kwa kificho, hauna nafasi humo.

Leo tunashtuka umeme kukatika nchi nzima utafikiri sio sisi hao hao ambao kila tukipata nafasi ya kuchagua kati ya mwanga na giza, hukimbilia giza. CCM na jemadari wake ukiwawashia taa ghafla watapofuka macho kwa athari za giza zilizowaathiri mpaka watoto na wajukuu zao. Uzuri moja ni kuwa giza haliwezi kushamiri kwenye mwanga na tumaini lililobaki ni kuwa hofu ya mwanga ulioanza kutokea kwa mbali inawatia kiwewe - shuhudia walivyoanza kugongana wenyewe kwa wenyewe humo gizani na si ajabu hawautaki mwanga hata kwa miaka mia ijayo !!
 
Sasa Raisi asipowajibisha mtu hapo nitaona kwa kweli yeye ndio awajibike. Huu ni upuuzi. Au ma Co-president wanafanya mambo?

Lusajo, Rais hahusiki wala msimlaumu. Yeye ni 'Rais' tu :(
 
Kikwete jiuzulu maana tunaona nchi imekushinda na tumechoka kukaa giza...Washindwe mafisadi safari hii lazima mtang'oka tu mwakani.
 
Wakulaumiwa ni wananchi wa Tanzania.

Umeme wa Tanzania ni kwaajili ya watukufu wachache wanaostahili. Tatizo ni kwamba wananchi wa kawaida hawataki kutumia vibali au koroboi wanang'ang'ania umeme.

Umeme siyo kitu muhimu kama chakula, wananhci wanaweza kusubiri mpaka zamu yao ya kuwa na umeme itakapofika. Hili jaribio lao la kutaka kutumia umeme kama waheshimiwa ni kuipamzigo Tanesco na serikali.

Wananchi wa Tanzania ni lazima waone aibu kwa kuipa mzigo waziada Tanesco wakati ufumbuzi wanao wenyewe.

KWa nini hawashikilii msimamo wao mzuri kama ule wa kukubali kufa kwa kukosa huduma bora za afya. Hivi hawatambui kwamba ni waheshimiwa waliotukuka tu ndiyo wenye haki ya kutumia fedha ya umma kutibiwa nje ya nchi.

Hivi hawajui kwamba fedha ya kuimarisha hospitali zetu hakuna kwa sababu serikali ikifanya hivyo basi fungu la kutibiwa nje litaingia wembamba?

Umeme ni starehe ambayo wananchi mmeamua kuiingilia na kuliingizia taifa taabu ya bure.
Bila nyie Wananchi msio na shukurani kwa waheshimiwa kuongeza matumizi yenu ya anasa ya umeme kusingekuwa na Songombingo ya Richmond wala Dowans.

Rostamu Aziz asingelalamika kwamba nabaguliwa kwa sbabu yeye ni Bamasinde kutoka kule kwenye nchi ya Waklidayo au Uajemi.

Ni vile haachii kidevu kikakua, yeye na mtu fulani anayesakwa wasingetofautiana.
Ninyi wananchi msio na shukurani mnge fuata taratibu za maendeleo na kuendelea kutumia koroboi na taa za chemuli mgeisaidia sana serikali na Tanesco, hata MH Lowassa angekuwa bado waziri mkuu.

Wakulaumiwa ni Wananchi wote wa Tanzania wasio na shukurani hata chembe.

Komeni kutaka maendeleo.
 
Lazima kwa mwendo huu mitambo ya Dowans inunulike tu!

Nchi nzima haina umeme ninapoandika dakika hii...

Kaazi kwelikweli

Yaani kama waona Zitto na wenzie wanavyotafuta toothpicks kwa kebehi. Ila haina shobo tutafika tuuu. Tatizo la Dar kwa usiku sio umeme kwa sana ila joto na Mbu
 
"Watanzania watafanya maamuzi yao hapo ambapo nchi itakuwa imegubikwa giza, mahospitali hayatoi huduma, viwanda havizalishi, wanafunzi vyuoni wanashindwa kusoma kwa sababu tulishindwa kufanya maamuzi"!
 
Lusajo, Rais hahusiki wala msimlaumu. Yeye ni 'Rais' tu :(


In leadership everything is your fault.

Kama yeye anaweka mabwege na wanasababisha haya ni kosa la nani.This can not happen ..........nchi nzima inakosa umeme.

Wanataka support ya wanainch kununua magenerator au kunauzembe umetokea ? yote haya ni Rais anahusika kulaumiwa.Kupunguza lawama ni kuwajibisha watu husika
 
In leadership everything is your fault.

Kama yeye anaweka mabwege na wanasababisha haya ni kosa la nani.This can not happen ..........nchi nzima inakosa umeme.

Wanataka support ya wanainch kununua magenerator au kunauzembe umetokea ? yote haya ni Rais anahusika kulaumiwa.Kupunguza lawama ni kuwajibisha watu husika
Nchi nyingine hali kama hii inaweza pelekea cabinet/congress/UWT kuhaha kutafuta maelezo kwa wahusika iweje umeme ukatike nchi nzima. Lakini Tanzania ambayo Rais wake uonesha kutojihusisha na masuala yenye kuathiri uchumi/ustawi wa nchi litapita kimya kimya kama vile nchi haina wenyewe.

BTW, wakati nchi ikiwa kizani mkwere yuko kwenye mwanga wa jenereta ambalo hata kelele zake hazisikii, ana shida gani?
 
Hivi kweli watanzania inawezekana kweli umeme ukatike nchi nzima kwa wakati mmoja? Jana tarehe 20 March umeme ulikatika nikajua ni Dar peke yake, mara nikapigiwa simu na rafiki yangu yuko Moro kuwa umeme umekatika, sijakaa sawa kaka yangu from Tanga akanipigia kuwa umeme kwao umekatika na yy simu yake itaisha charge soon. Nilipomaliza kuongea naye nikajiuliza kuwa ndio ile khabari ya TANESCO kuwa nchi ikiingia gizani kusiwe na lawama? sasa jana ilikuwa kwa masaa 4 tu, siku zinavyozidi kwenda si ndio itakuwa jehanamu ya giza? Watanzania haya ndio maendeleo tunayoyataka?
 
Ama kweli nguvu ya pesa za kifisadi ni kubwa. Hii ni hujuma wala sio hitilafu ya mitambo. MKONO WA ROSTAM MREFU, KWELI CHI ROSTAM AMEIWEKA MFUKONI. WATANZANIA TUKIMBILIE WAPI. NA RAISI YUPO TU, KIMYAA. HUYU ROSTAM MBONA ANACHEZEA WATANZANIA KAMA KWAMBA WOTE TU MABWEGE?
 
hawa mabeberu wanatumia kila aina ya njia ili kufanikisha ununuzi wa mitambo ya dowans.....alafu sasa wananchi nao sijui hawaelewi au wamerogwa.....

......Nikiangalia hata humu JF tu wa2 wanavyotetea ununuzin wa kifisadi namna ile siamini macho yangu......naishia kusikitika tu.....

......umeme unakatika masaa 7???? bila taarifa yoyote hii kweri bongo
 
Kama ulikatika nchi nzima, yawezekana ni hujuma.

Vifaa vya ndani vinapoharibika kutokana na tatizo hilo, tumwendee nani? Au ndiyo imetoka hiyo.

Kwa kweli ni usumbufu wa hali ya juu. Hivi mtu(organization) unaweza kupanga mambo ya maendeleo katika hali hii? Unreliable power supply is our culture. The culture which fosters underdevelopment and poverty.

Bado watawala wetu wanatufunga kamba za mipango ya maendeleo katika nchi hii. Tu majuha kiasi hicho?
 
Sasa kama Mtu aliyetishia kuwepo giza nchi nzima(Dr.Rashid)bado yuko TANESCO unatarajia nini.Mtu ambaye hajui njia nyingine ya kutatulia tatizo la Umeme zaidi kununua mitambo mitumba ya Dowans anafanya nini pale kama siyo kulindwa tu.aondoke awekwe mtu mwe vision pale kama tatizo la umeme halijaisha.
 
Ni kweli taarifa zinaoyesha ulikatika mikoa mingi zaidi ya uliyotaja hapo.

Tanazia tunakwenda wapi?

Kweli huko inakokwenda kwa Pez de ....ambaye Is very Neutral, amefungwa mdomo na RA/EL_EPA ... Hakemei? Anafanya timing ya kupendwa cheeply na kushinda kwa kishindo ....huko tunakwenda ni kwnye Kiza kizito ...kama cha last night.

Very sad
 
Nadhani kuna haja ya mtu kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye maana inaonesha hata kama tukinyamaza na mawe yakapiga kelele itakuwa sawa na kelele za mlango...
Wadau tuadvocacy kura za kutokuwa na imani na kabinet nzima na ikishindikana basi hata bunge nalo tulipigie kura.... (kasheshe, nani atamfunga paka kengele)

Not only sad but is real shame
 
Duh!... ndugu zangu Bongo poleni sana hii sikuipata...
Kama ni hujuma za Dowans na hizo 199mw mawaomba msikubali kabisa kudanganywa na hawa jamaa kwani hizo 100mw haziwezi kusababisha nchi nzima ikose umeme..
Hizi ni Hujuma wakifikiria kwamba Wadanganyika hawataelewa tofauti..
Na kama tatizo lipo ktk grid ya Taifa, tutahitaji maelezo ya kina toka kwa Ngereja..

NB:- Wakuu hili jina Ngereja mbona limekaa kama mtu wa kwetu?...
 
Leo ni ya pili mgao wa umeme umelikumba jiji La Daresalam na Zenji ni ya tano hakuna umeme , maji yamekatika jeneretor zinanguruma ,mifuko ya plastiki mali kwa wanaokaa magolofani hutumia kujazia haja kubwa ,na kuirusha madilishani kwa hasira.
Je huku si ndio kushindwa kwa serikali au watasingizia mtikisiko wa uchumi huko ulimwengu wa kwanza ? Maana ikiwa mtikisiko ni hivi je ukianguka ?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom