Mchawi aliyebobea anatakiwa!

Mchawi aliyebobea anatakiwa!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,860
Reaction score
50,644
Anatakiwa mchawi aliyebobea ama awe wa makafara au mchawi wa matunguli ambaye atakuwa na uwezo wa kubadili hali ya mambo kwa muda mfupi sana. Mchawi huyo awe na nguvu ya kupindua mazindiko ya mizimu ama ya "Kisomo" yaliyowekwa kwenye eneo lolote lile hata kama eneo hilo linalindwa kwa hali ya juu kiasi gani.

Malipo yake yatategemea kumaliza kazi yake kwa wakati na kwa lengo lilokusudiwa. Nafasi hii ipo wazi hata kwa wale wenye uwezo wa kuvuta majini bahari yafanye "Shughuli" na kama wewe una mizukule ama vibwengo na vinyamkela pia unakaribishwa.

Mtu anayetakiwa kulogwa anatakiwa arudi kwenye utimamu wa akili yake kwani hali aliyo nayo sasa inamfanya apende sifa hadi jina lake mwenyewe amelisahau badala yake anajitambulisha kwa jina la marehemu babu yake!! Anayelogwa anaonekana kama vile amekuwa kichaa na mlogaji anatakiwa amloge ili arudi kwenye utimamu wake!!
 
Doh, acha niwahi siti ya mbele kabisa nikingojea ujio wa huyo mchawi
 
Dogo acha dhihaka kwa watawala.
Kumbuka Mungu ameweka mamlaka za kidunia ili zitawale mienendo yetu na kustawisha ustaarabu katika jamii.
Tutafute namna nzuri ya kukosoa sio kihivi.
 
Dogo acha dhihaka kwa watawala.
Kumbuka Mungu ameweka mamlaka za kidunia ili zitawale mienendo yetu na kustawisha ustaarabu katika jamii.
Tutafute namna nzuri ya kukosoa sio kihivi.
Kama hili jambo lingekuwa ni la siasa ningeliweka kwenye Jukwaa la siasa. wewe kakwambia nani nazungumzia watawala?
 
Dogo acha dhihaka kwa watawala.
Kumbuka Mungu ameweka mamlaka za kidunia ili zitawale mienendo yetu na kustawisha ustaarabu katika jamii.
Tutafute namna nzuri ya kukosoa sio kihivi.
Silipendi hilo neno.
 
Dogo acha dhihaka kwa watawala.
Kumbuka Mungu ameweka mamlaka za kidunia ili zitawale mienendo yetu na kustawisha ustaarabu katika jamii.
Tutafute namna nzuri ya kukosoa sio kihivi.
Ametajwa mtawala gani hapo? Mbona mnajishtukia hivi kinomanoma!!!
 
Kama hili jambo lingekuwa ni la siasa ningeliweka kwenye Jukwaa la siasa. wewe kakwambia nani nazungumzia watawala?

Kuna mahali nilitakiwa kuweka tangazo langu hili ambapo nitapata wachawi kirahisi?
Sijawahi kukuona kwenye hizi maneno za kina Mshana, Mzizi mkavu na Jichawi lkn baada ya kutafakari naona mmmmh hujakosea njia iko maneno hapo ngoja nisome tena.
 
*Mwenye group la wachawi aniunganishe na mimi kuna mtu ananifuatilia maisha yangu nimfundishe adabu.
 
kuna ile kamati ya ufundi ya wazee wa ludewa inafaa sana
 
mbishi.d asante sana hao jamaa wa Ludewa kweli watafaa. Hivi Lizaboni na Wakudadavuwa hakuna mahali mnajua kuna watu wanaoweza kunisaidia. Nicholas huko Arusha hakuna mtu anayeiweza hii shughuli? Ningependa FaizaFoxy kama kuna watu wale wataalum wa kufuga majini uniunganishe nao ama kama unawafahamu wa mlingotini au kaole kule Bagamoyo utanielekeza.
 
Baba iyo Kazi mi naiweza ninauwezo wa kujigeuza inzi,upepo,panya,nk kulingana na sehemu niendayo kufanya Kazi nipedili uyo chizi atakuwa mzima tu usihofu
 
Ametajwa mtawala gani hapo? Mbona mnajishtukia hivi kinomanoma!!!
We mbulumundu sitaki lwenya. Tangu lini id yangu ikashabihiana na lumumba?!
The inner context of this thread is to provoke ongoing leadership of our beloved country.
Najua Nchi yetu na Wananchi wake bado tupo nyuma kwenye nyanja nyingi. Na ni kweli utawala uliopo una madhaifu mengi.
Tukosoe kistaarabu. Kumbukeni Nchi yetu imezungukwa na majirani ambao kila kukicha wanafuatilia feedback za utawala wetu na impact zake kwa wananchi. Sasa ni ujinga kuendekeza mada zisizo na mashiko(kama hizi). Tukosoe kwa mada zenye mlengo wa kuboresha. Tuyataje mapungufu yaliyopo na njia mbadala wa kipi kilipaswa kufanyika. Kejeli za kishenzi hazijengi, ukiongea upupu hata kama ndani yake kuna hoja ya msingi welevu wataipuuza.
Huyu dogo(mleta mada) kajifanya janja janja kutaja ujinga ujinga wake kwenye jukwaa la habari na hoja mchanganyiko ili iwe defence kwake!! Kumbe ujinga mtupu.
 
Kisima usilete mambo yako ya siasa kwenye mada yangu. Liko jukwaa la siasa nenda huko!!
 
Back
Top Bottom