Leslie Mbena
JF-Expert Member
- Nov 24, 2019
- 207
- 677
MCHANGO WA DR. JOHN POMBE MAGUFULI NCHINI TANZANIA NA BARA LA AFRIKA KWA UJUMLA.
Dr. John Pombe Magufuli aliyehudumu kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya Tano aliheshimika nchini Tanzania, Barani Afrika na Duniani kwa Ujumla kutokana na namna alivyosimama kidete kuhakikisha maslahi ya Wananchi wa Tanzania na Nchi za Kiafrika kwa ujumla yanapewa kipaumbele cha kwanza.
Dr. Magufuli ametoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Bara la Afrika kwa namna tofauti tofauti katika kipindi chake cha Uongozi.
MCHANGO WA DR. MAGUFULI KATIKA UKUAJI WA KISWAHILI BARANI AFRIKA.
Dr. John Pombe Magufuli alihamasisha matumizi ya Kiswahili kama lugha kuu ya mawasiliano katika Nchi za Bara la Afrika. Nchi nyingi za Bara la Afrika zilihamasika kuanza kutumia kiswahili katika shughuri zake za kila siku na pia kuanza kufundishwa kwa lugha ya kiswahili katika mataifa malimbali Barani Afrika. Wakati fulani Dr. Magufuli alisafiri katika nchi mbalimbali za Bara la Afrika ikiwa ni pamoja Afrika Kusini ambako aliwapelekea zawadi ya Vitabu vya Kiswahili wananchi wa Nchi hizo ikiwa ni kuonyesha namna alivyosimamia kampeni yake kuhusu maendeleo ya lugha ya Kiswahili. Baada ya jitihada hizo Nchi mbalimbali ikiwemo Afrika Kusini zilianza kufundisha Kiswahili na pia Kiswahili kilitambulishwa kama Lugha Rasmi katika mikutano yote ya Jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) pamoja na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Pia Dr. Magufuli alihamasisha kutafsiriwa kwa sheria zote za Tanzania pamoja na mikataba mbalimbali kama sehemu ya kukifanya kiswahili kuwa lugha rasmi katika Shughuri zote za kiserikali nchini Tanzania. Dr. John Pombe Magufuli alitumia lugha ya Kiswahili katika mikutano yake takkribani yote hali iliyopelekea wakosoaji wake kusema kuwa hajui kuongea lugha ya Kiingeleza. Muda wote Dr Magufuli alijivunia kuongea Kiswahili kwa vile aliamini matumizi ya lugha ya Kigeni ni sehemu ya Ukoloni wa Kifikra.
MCHANGO WA DR MAGUFULI KATIKA UKOMBOZI WA KIFIKRA.
Muda mwingi Dr. Magufuli alisisitiza kuwa Afrika ni tajiri sana. Dr Magufuli aliwahamasisha wa Afrika na Watanzania kutembea Kifua mbele kwa kujivunia uafrika wao. Dr. Magufuli hakuwahi kuamini kuwa suluhisho la matatizo ya Afrika litapatikana kutoka Nje ya Bara la Afrika. Hivyo alisisitiza Nchi za Afrika kutumia raslimali walizo nazo kwa manufaa ya Wananchi wao na kutokujihisi wanyonge mbele ya wawekezaji wa kigeni ama mataifa ya Kigeni. Dr. Magufuli alikuwa tayari kuhatarisha uhusiano na muwekezaji yoyote yule ama Taifa lolote lile ambalo lingetaka kuonyesha kutaka kufanya maamuzi yenye kunyonya ama kudharau Watanzania na wa Afrika kwa ujumla. Lakini pia Dr Magufuli alipandikiza fikra ya kufanya kazi kwa bidii kupitia kauli mbiu yake "HAPA KAZI TU, "ASIYEFANYA KAZI ASILE" na nyinginezo kama hizo. Kauli mbiu hizi ziliwachochea wananchi hususani Vijana kufanya kazi kwa bidii.
MCHANGO WA DR MAGUFULI KATIKA SAYANSI NA UTAFITI.
Dr. John Pombe Magufuli ambaye kitaaluma ni Mwanasayansi alitoa changamoto kubwa kwa wataalamu wa Bara la Afrika kufanya tafiti badala ya kusubiri kuletewa madawa kutoka katika mataifa ya Kigeni. Wakati wa Janga la CORONA Dr. John Pombe Magufuli aliamua kutofautiana na madakati wengi wa Bara la Afrika pamoja na wale wa Shirika la Afya Duniani kwani aliamua kupima Ubora wa Vifaa vya kupima ugonjwa wa CORONA ambapo alibaini kuwa Vifaa vile havikuwa madhubuti hata kidogo kwani vilionyesha kuwa mbuzi, papai, na sampuli iliyochukuliwa kwenye ndege aina Kanga vina maambukizi ya Ugonjwa wa CORONA. Ugunduzi huu uliwaamsha usingizini wanasayansi kutoka mataifa mbalimbali ambao waliamua kuzuia kwa muda matumizi ya Vifaa hivyo. Lakini pia Dr. Magufuli alikataa matumizi ya Barakoa zilizozalishwa kutoka katika mataifa ya Kigeni kwani zinaweza kutumika kueneza maambukizi kwa kiasi kikubwa. Lakini pia Dr. Magufuli alihamasisha matumizi ya Tiba mbadala badala ya kutumia Chanjo ambayo ilikuwa bado kwenye majaribia na iliyokuwa ikionyesha madhara kwa kiasi kikubwa kwa watumiaji.
MCHANGO WA DR. MAGUFULI KATIKA KUPIGANIA UHURU WA KIUCHUMI.
Dr. John Pombe Magufuli aliamini katika ushirikiano na uwekezaji usio na Chembe ya Uonyonyaji. Muda wote alikuwa mkali kwa makampuni ya uwekezaji yaliyokuwa yakikwepa Kodi na kufanya Shughuri za uhujumu uchumi. Kutokana na msimamo wake huu Viongozi wengi wa Bara la Afrika walianza kuiga nyendo zake na hapa ndipo msamiati "MAGUFULIFICATION OF AFRICA" ulipotengenezwa ukimaanisha Kuchukua maamuzi ama kutenda mambo kama Magufuli kwa manufaa ya Bara la Afrika. Itakumbukwa vema namna msimamo wa Dr. Magufuli kuhusu kampuni ya BARRICK ulivyosaidia kuanzisha mfumo mpya wa uwekezaji ambao ulilenga kuwanufaisha Watanzania. Mfumo huu ndio ambao sasa unatumiwa na Kampuni ya Barrick kote barani Afrika katika kutekeleza shughuri za Uchumbaji wa madini.
MCHANGO WA DR. JOHN POMBE MAGUFULI KISIASA NA KIJAMII.
Dr John Pombe Magufuli aliamini katika ushirikiano na mataifa ya Afrika kuwa ndiyo njia pekee ya kuleta maendeleo barani Afrika. Hivyo Dr. Magufuli alihubiri katika siasa zenye Kuchochea maendeleo kwa wananchi. Dr. Magufuli aliguswa na matatizo ya Wananchi wa Bara la Afrika kwa kiasi kikubwa sana. Muda wote yalipotokea majanga katika Nchi za Afrika alikuwa msatari wa mbele kutoa msaada katika Nchi hizo. Mfano Dr. Magufuli alitoa msaada wa madawa, Blanketi na wataalamu pale Nchi ya Msumbuji ilipopigwa na Kimbunga. Lakini pia Dr. Magufuli ameshiriki kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kuwa usalama , amani na mshikamano miongoni mwa Nchi za Afrika unakuwa mkubwa.
Kwa kuhitimisha, Dr. Magufuli alikuwa mwana wa Afrika, Kiongozi aliyeielewa vema na Kuiishi Falsafa ya Umajumui wa Afrika. Kiongozi huyu aliamini katika kuliunganisha Bara la Afrika na miundombinu bora ingekuwa Suluhisho la matatizo mbalimbali ndani ya Bara la Afrika. Katika kufanya hivyo alijenga miradi ya Kimkakati iliyolenga kunufaisha Bara zima la Afrika kama Bomba la Mafuta kutoka Tanzania mpaka Hoima Uganda, Ujenzi wa Reli ya Umeme ambao ungeunganisha Nchi za Congo, Burundi, Rwanda nk, lakini pia Ujenzi wa Bwawa la Umeme ambalo lingezalisha umeme ambao ungetosheleza kuuzwa katika Nchi Jirani pia.
Josias Charles
MAGUFULIST
Dr. John Pombe Magufuli aliyehudumu kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya Tano aliheshimika nchini Tanzania, Barani Afrika na Duniani kwa Ujumla kutokana na namna alivyosimama kidete kuhakikisha maslahi ya Wananchi wa Tanzania na Nchi za Kiafrika kwa ujumla yanapewa kipaumbele cha kwanza.
Dr. Magufuli ametoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Bara la Afrika kwa namna tofauti tofauti katika kipindi chake cha Uongozi.
MCHANGO WA DR. MAGUFULI KATIKA UKUAJI WA KISWAHILI BARANI AFRIKA.
Dr. John Pombe Magufuli alihamasisha matumizi ya Kiswahili kama lugha kuu ya mawasiliano katika Nchi za Bara la Afrika. Nchi nyingi za Bara la Afrika zilihamasika kuanza kutumia kiswahili katika shughuri zake za kila siku na pia kuanza kufundishwa kwa lugha ya kiswahili katika mataifa malimbali Barani Afrika. Wakati fulani Dr. Magufuli alisafiri katika nchi mbalimbali za Bara la Afrika ikiwa ni pamoja Afrika Kusini ambako aliwapelekea zawadi ya Vitabu vya Kiswahili wananchi wa Nchi hizo ikiwa ni kuonyesha namna alivyosimamia kampeni yake kuhusu maendeleo ya lugha ya Kiswahili. Baada ya jitihada hizo Nchi mbalimbali ikiwemo Afrika Kusini zilianza kufundisha Kiswahili na pia Kiswahili kilitambulishwa kama Lugha Rasmi katika mikutano yote ya Jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) pamoja na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Pia Dr. Magufuli alihamasisha kutafsiriwa kwa sheria zote za Tanzania pamoja na mikataba mbalimbali kama sehemu ya kukifanya kiswahili kuwa lugha rasmi katika Shughuri zote za kiserikali nchini Tanzania. Dr. John Pombe Magufuli alitumia lugha ya Kiswahili katika mikutano yake takkribani yote hali iliyopelekea wakosoaji wake kusema kuwa hajui kuongea lugha ya Kiingeleza. Muda wote Dr Magufuli alijivunia kuongea Kiswahili kwa vile aliamini matumizi ya lugha ya Kigeni ni sehemu ya Ukoloni wa Kifikra.
MCHANGO WA DR MAGUFULI KATIKA UKOMBOZI WA KIFIKRA.
Muda mwingi Dr. Magufuli alisisitiza kuwa Afrika ni tajiri sana. Dr Magufuli aliwahamasisha wa Afrika na Watanzania kutembea Kifua mbele kwa kujivunia uafrika wao. Dr. Magufuli hakuwahi kuamini kuwa suluhisho la matatizo ya Afrika litapatikana kutoka Nje ya Bara la Afrika. Hivyo alisisitiza Nchi za Afrika kutumia raslimali walizo nazo kwa manufaa ya Wananchi wao na kutokujihisi wanyonge mbele ya wawekezaji wa kigeni ama mataifa ya Kigeni. Dr. Magufuli alikuwa tayari kuhatarisha uhusiano na muwekezaji yoyote yule ama Taifa lolote lile ambalo lingetaka kuonyesha kutaka kufanya maamuzi yenye kunyonya ama kudharau Watanzania na wa Afrika kwa ujumla. Lakini pia Dr Magufuli alipandikiza fikra ya kufanya kazi kwa bidii kupitia kauli mbiu yake "HAPA KAZI TU, "ASIYEFANYA KAZI ASILE" na nyinginezo kama hizo. Kauli mbiu hizi ziliwachochea wananchi hususani Vijana kufanya kazi kwa bidii.
MCHANGO WA DR MAGUFULI KATIKA SAYANSI NA UTAFITI.
Dr. John Pombe Magufuli ambaye kitaaluma ni Mwanasayansi alitoa changamoto kubwa kwa wataalamu wa Bara la Afrika kufanya tafiti badala ya kusubiri kuletewa madawa kutoka katika mataifa ya Kigeni. Wakati wa Janga la CORONA Dr. John Pombe Magufuli aliamua kutofautiana na madakati wengi wa Bara la Afrika pamoja na wale wa Shirika la Afya Duniani kwani aliamua kupima Ubora wa Vifaa vya kupima ugonjwa wa CORONA ambapo alibaini kuwa Vifaa vile havikuwa madhubuti hata kidogo kwani vilionyesha kuwa mbuzi, papai, na sampuli iliyochukuliwa kwenye ndege aina Kanga vina maambukizi ya Ugonjwa wa CORONA. Ugunduzi huu uliwaamsha usingizini wanasayansi kutoka mataifa mbalimbali ambao waliamua kuzuia kwa muda matumizi ya Vifaa hivyo. Lakini pia Dr. Magufuli alikataa matumizi ya Barakoa zilizozalishwa kutoka katika mataifa ya Kigeni kwani zinaweza kutumika kueneza maambukizi kwa kiasi kikubwa. Lakini pia Dr. Magufuli alihamasisha matumizi ya Tiba mbadala badala ya kutumia Chanjo ambayo ilikuwa bado kwenye majaribia na iliyokuwa ikionyesha madhara kwa kiasi kikubwa kwa watumiaji.
MCHANGO WA DR. MAGUFULI KATIKA KUPIGANIA UHURU WA KIUCHUMI.
Dr. John Pombe Magufuli aliamini katika ushirikiano na uwekezaji usio na Chembe ya Uonyonyaji. Muda wote alikuwa mkali kwa makampuni ya uwekezaji yaliyokuwa yakikwepa Kodi na kufanya Shughuri za uhujumu uchumi. Kutokana na msimamo wake huu Viongozi wengi wa Bara la Afrika walianza kuiga nyendo zake na hapa ndipo msamiati "MAGUFULIFICATION OF AFRICA" ulipotengenezwa ukimaanisha Kuchukua maamuzi ama kutenda mambo kama Magufuli kwa manufaa ya Bara la Afrika. Itakumbukwa vema namna msimamo wa Dr. Magufuli kuhusu kampuni ya BARRICK ulivyosaidia kuanzisha mfumo mpya wa uwekezaji ambao ulilenga kuwanufaisha Watanzania. Mfumo huu ndio ambao sasa unatumiwa na Kampuni ya Barrick kote barani Afrika katika kutekeleza shughuri za Uchumbaji wa madini.
MCHANGO WA DR. JOHN POMBE MAGUFULI KISIASA NA KIJAMII.
Dr John Pombe Magufuli aliamini katika ushirikiano na mataifa ya Afrika kuwa ndiyo njia pekee ya kuleta maendeleo barani Afrika. Hivyo Dr. Magufuli alihubiri katika siasa zenye Kuchochea maendeleo kwa wananchi. Dr. Magufuli aliguswa na matatizo ya Wananchi wa Bara la Afrika kwa kiasi kikubwa sana. Muda wote yalipotokea majanga katika Nchi za Afrika alikuwa msatari wa mbele kutoa msaada katika Nchi hizo. Mfano Dr. Magufuli alitoa msaada wa madawa, Blanketi na wataalamu pale Nchi ya Msumbuji ilipopigwa na Kimbunga. Lakini pia Dr. Magufuli ameshiriki kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kuwa usalama , amani na mshikamano miongoni mwa Nchi za Afrika unakuwa mkubwa.
Kwa kuhitimisha, Dr. Magufuli alikuwa mwana wa Afrika, Kiongozi aliyeielewa vema na Kuiishi Falsafa ya Umajumui wa Afrika. Kiongozi huyu aliamini katika kuliunganisha Bara la Afrika na miundombinu bora ingekuwa Suluhisho la matatizo mbalimbali ndani ya Bara la Afrika. Katika kufanya hivyo alijenga miradi ya Kimkakati iliyolenga kunufaisha Bara zima la Afrika kama Bomba la Mafuta kutoka Tanzania mpaka Hoima Uganda, Ujenzi wa Reli ya Umeme ambao ungeunganisha Nchi za Congo, Burundi, Rwanda nk, lakini pia Ujenzi wa Bwawa la Umeme ambalo lingezalisha umeme ambao ungetosheleza kuuzwa katika Nchi Jirani pia.
Josias Charles
MAGUFULIST