Mch. Mwasapile vs. Mch. Rwakatale

Nina maswali mengi sana yananiumiza kichwa na majibu yako ya jumla yanazidi kunichanganya, hivi huyu "babu" aliongea na Mungu kama alivyoongea na Musa wakati anampa amri kumi?

Hapana, kwa maelezo yake (Babu) ni wazi hakuwa anaongea na Mungu kama ilivyokuwa kwa Moses. Yeye amekuwa akipewa maelekezo na Mungu ndotoni. Mimi ninachokataa ni hoja ya kukataa 'unabii' huo kwa kigezo cha hiyo pesa inayotozwa.

Nadhani pengine kinachotupa shida watu wengi ni kutofahamu uwezo wa Mungu na namna anavyofanya kazi. Mungu amekuwa akitenda kazi na kufanya miujiza mara nyingi ila kwa sababu we take most of things for granted, tunashindwa kuyaona au kuyashuhudia kama alivyofanya Babu na tunaishia kufikiri pengine mambo yanatokea kwa uwezo wetu tu.

Babu angeweza kusema amefanya 'utafiti' wake na amegundua dawa/tiba ya hayo magojwa anayodai kuyatibu (hata kama kiukweli hakufanya utafiti huo, bali 'ameoteshwa tu' dawa hiyo!). Kama kweli inatibu (say HIV), angeweza kucharge mamilioni na kwa tabu ya gonjwa hili, tungezitoa tu bila maswali - maana zinatibu.

Shida imekuja kwa yeye kukiri hadharani kuwa dawa hiyo haitokani na uwezo wake bali ameoteshwa tu (ametoa ushuhuda!) - ni kama amekataa ku-claim credits kwa jambo ambalo halifanyi kwa uwezo wake.

Kumbuka pia Mungu amekuwa akiwatumia wataalamu na wanasayansi mbalimbali kutatua matatizo ya kitabibu na mengineyo yaliyowakabli binaadamu - ndui, polio etc lakini katika yote haya (hata kama kwa hakika Mungu aliwaonesha dawa hizo/aliwapa solution wataalamu hao ndotoni) hakuna aliyeweza kumshuhudia Mungu (si wanadhani yamefanyika kwa uwezo wao!).
 
Me nafikiri mch.mwasapile ametumwa na mungu kuja kuonyesha maajabu ya mungu hivyo mwacheni atibu watu na serikari itambue ya kwamba kuna maswala ya kisayansi; mitishamba na kiimani pia. Hivyo kuna haja ya ya kutunga sheria ndogondogo za kuwalinda badala ya kupinga tu.
 
Mimi sina shida na ndoto yake ila wasiwasi wangu mie upo kwenye "mia tano" huyo aliemuotesha ndoto ni huyu huyu Mungu wa Isaya na Yakobo? aliemfanya Yesu akawaponya watu bila malipo? au kuna Mungu mwingine aliemuotesha? je hizi mia tano (sio nyingi kwa mtu kushindwa kuimudu) lakini je zinaenda wapi? Mungu alimpa maelezo ya hizo "mia tano"? je Mungu huyu tumjuae sie wa Isaya na Yakobo anahitaji mia tano zetu??????????
hivi yule dogo shehe sharif alikuwa anafanya tiba bure?
 
hivi yule dogo shehe sharif alikuwa anafanya tiba bure?

Sheikh Shariff Who? acha kutoka nje ya mada hapa tunazungumzia

. Homework tuliyonayo ni:
1. je, hii ni imani ya aina gani?
2. imani hii inamuelekea mungu gani?
3. hii ni imani ya dini gani?
4. mungu mwenye utaratibu huo alioutoa ni yupi?, yuleyule aliyemtuma Yesu duniani kuokoa wanadamu, au mwingine?

Toka mwanzo nimesema waziwazi kuwa kutokana na utaratibu mzima wa ndoto hii na ufunuo huu na jinsi unavyotekelezwa likiwemo:
· hilo la kutoza sh. 500/- kwa kila kichwa,
· tiba kwa kikombe kimoja cha dawa bila kumhudumia mgonjwa kiroho,
· tiba kufanyikia loliondo peke yake,
· wengine wanapewa kikombe wakiwa ndani ya magari na wakishakunywa wanageuza na kuondoka bila hata neno moja la Mungu
· nk.
 
Mi naona tatizo watu wanataka muujiza kama huu utokee kwa viongozi wakubwa wa dini ndo labda wata amini! Wanawaona kama watu wengine hawako sawa kiimani kiasi kwamba Mungu anaweza kuwatumia.

Mungu anaweza kumtumia mtu yeyoye kukamilisha mission yake, siyo lazima awe mtu anaye heshimika sana kwenye Jamii. Uzuri wa Babu hawaulizi majina wateja wake, wala haulizi imani zao, wala wanakotoka, wala vyama vyao na wala haulizi unaumwa nini.

Yeye anakupa KIKOMBE UNA KUNYWA unatembea, wewe shauri yako na maswali maswali yako utajiju, lakini yeye katimiza alichotumwa kamaliza. Muacheni Babu atoe dozi kwa anayetaka, halazimishi wala hapigi kampeni kama za kutokomeza malaria na chanjo ya mabusha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom