Mbwa kala Mbwa (kituko)

Memtata

JF-Expert Member
Jul 27, 2013
552
1,800
Hiki kituko kilinitokea miaka kadhaa iliyopita, nilikuwa dingi tayari sema ujana ulikuwa mwingi sana hadi kujisahau🤣 lakini kwa sasa mimi ni ustaadh hizi zimebaki hadithi tu.

Kuna sehemu nilikuwa na project kwenye kampuni moja hivi. Kila siku kabla ya kuingia lango kuu nilikuwa na utaratibu wa kupitia vitafunwa kwa kina mama ambao walikuwa wamejipanga hapo nje kwenye container maalum waliloandaliwa na kampuni.

Siku hiyo nikashuka kwenye gari nikiwa na haraka ili nisimcheleweshe dereva, moja kwa moja kwa dada mmoja aliyejaaliwa sehemu za kukalia 🤣 japokuwa wanawake vibonge siyo hobby yangu lakini hawa viumbe wakiwa wameubana huwa wanatamanisha sana 😍

Nikatoa noti na kuomba chapati mbili na sambusa wakati huo kuna jamaa waliokuwa wakihudumiwa pia, ilipofika zamu yangu dada akanipa bahasha ya vitafunwa na akanirudishia change yangu, bila hata kuhesabu nikakunja na kuweka mfukoni.

Jioni wakati nimetoka job nikiwa home nilipocheki zile hela katikati kulikuwa na kikaratasi kimeandikwa 'nitafute kwa namba hii nna ujumbe wako' chini yake kukiwa na namba ya simu 🤣🤣🤣

Moyo ukapiga paah! 😍😍😍 Akili ikavurugika kidogo kisha nikaanza kuwaza 🤣

"Kwamba yule binti kanielewa! Kwahiyo anataka kunitunuku lile shepu lake?"

Aiseee.... Niliwaza mengi kwakweli, yani muda huo nilishamvua nguo mtoto wa watu nikimuangalia kwa makini akiwa amejilaza kifudifudi kitandani huku akificha uso wake kwa aibu 🤣

Ukweli yule dada hakuwa mzuri sana ila alikuwa na lishepu la kinyankole kiuno kidogo, hips umbo la 🖤 na kalio ndo usiseme yani akiachia ushuzi leo harufu unaanza kuisikia kesho yake maana safari ni ndefu 🤣.

Anyway tuachane na shape turudi kwenye story. Basi nikakaa nikitafakari ile namba, nikawaza nipige nisipige? Kauoga fulani kakaniingia nikaona nitume text kwanza 😁

Huku nikiwa nimejilaza kitandani mkono mmoja ukiwa juu ya boxer nikaanza........

"Mambo!”
sikujibiwa muda huo lakini baada ya dakika kadhaa nikajibiwa.
"Pouwa"
"Za wapi?"
"Nyumbani, nani mwenzangu?"
"Aah! Hujanifaham tu?"
"Hapana, nikumbushe"

Kimya kwa muda mchache nikawaza nijitambulishe vipi, kisha nikamjibu.
"Leo asubuhi kwenye vitafunwa ulinipa namba yako nikutafute"

Fasta nikajibiwa....
"Ahaa!.... Nimekumbuka, umefanya vizuri kunitafuta.

Moyo wangu ukatulia nikajifariji "kumbe kweli! Nimependwa" wee..! 🤣🤣🤣

Kabla sijajibu ikaingia sms nyingine.
"Kwahiyo ndio hivyo mi nimekuelewa sana naomba tu unikubalie"

Hapa nilishtuka kidogo nikaona aah wapi! Mbona kama muandiko haueleweki huu alafu kama ni kweli mbona kirahisi hivi.

Nikamuuliza "Kwahiyo unasemaje?" Akajibu "mi nakusikiliza wewe mi nimeshafikisha ujumbe wangu kama vipi hata leo tuonane, ukweli kila siku nikipita pale huwa nakuangalia sana sababu ya uzuri wako"

"Oyaa kwani we nani?" Nilijikuta naulizia kwa hasira maana kila wakati muandiko sikuuelewa kabisa.

"Mi si ndio nimekupa namba asubuhi pale lango kuu wakati nanunua vitafunwa kwako, we ukiniona utanikumbuka tu" akajibu 🤣🤣🤣

"Dadeki! Kwahiyo wewe ni mwanaume?" Nikauliza nikiwa na hasira zaidi, bahati mbaya sms haionyeshi muonekano 🤣🤣 akajibu fasta...
"Swali gani hilo? Ndio!"
"Oya umechemka mi mwenyewe kidume inaonekana wakati unampa hizo namba uliweka kwenye hela ambazo alinirudushia chenji mimi, mi mwenyewe nilijua nachat na yule dada!" 🤣🤣🤣🤣

Jamaa hakunijibu tena na mimi nikafuta namba hadi leo sijawahi kumjua huyu baharia ila tu nilisikitika uzembe wake wa kuogopa kumface yule dada ndio umesababisha yote haya🤣
 
Hiki kituko kilinitokea miaka kadhaa iliyopita, nilikuwa dingi tayari sema ujana ulikuwa mwingi sana hadi kujisahau🤣 lakini kwa sasa mimi ni ustaadh hizi zimebaki hadithi tu.

Kuna sehemu nilikuwa na project kwenye kampuni moja hivi. Kila siku kabla ya kuingia lango kuu nilikuwa na utaratibu wa kupitia vitafunwa kwa kina mama ambao walikuwa wamejipanga hapo nje kwenye container maalum waliloandaliwa na kampuni.

Siku hiyo nikashuka kwenye gari nikiwa na haraka ili nisimcheleweshe dereva, moja kwa moja kwa dada mmoja aliyejaaliwa sehemu za kukalia 🤣 japokuwa wanawake vibonge siyo hobby yangu lakini hawa viumbe wakiwa wameubana huwa wanatamanisha sana 😍

Nikatoa noti na kuomba chapati mbili na sambusa wakati huo kuna jamaa waliokuwa wakihudumiwa pia, ilipofika zamu yangu dada akanipa bahasha ya vitafunwa na akanirudishia change yangu, bila hata kuhesabu nikakunja na kuweka mfukoni.

Jioni wakati nimetoka job nikiwa home nilipocheki zile hela katikati kulikuwa na kikaratasi kimeandikwa 'nitafute kwa namba hii nna ujumbe wako' chini yake kukiwa na namba ya simu 🤣🤣🤣

Moyo ukapiga paah! 😍😍😍 Akili ikavurugika kidogo kisha nikaanza kuwaza 🤣

"Kwamba yule binti kanielewa! Kwahiyo anataka kunitunuku lile shepu lake?"

Aiseee.... Niliwaza mengi kwakweli, yani muda huo nilishamvua nguo mtoto wa watu nikimuangalia kwa makini akiwa amejilaza kifudifudi kitandani huku akificha uso wake kwa aibu 🤣

Ukweli yule dada hakuwa mzuri sana ila alikuwa na lishepu la kinyankole kiuno kidogo, hips umbo la 🖤 na kalio ndo usiseme yani akiachia ushuzi leo harufu unaanza kuisikia kesho yake maana safari ni ndefu 🤣.

Anyway tuachane na shape turudi kwenye story. Basi nikakaa nikitafakari ile namba, nikawaza nipige nisipige? Kauoga fulani kakaniingia nikaona nitume text kwanza 😁

Huku nikiwa nimejilaza kitandani mkono mmoja ukiwa juu ya boxer nikaanza........

"Mambo!”
sikujibiwa muda huo lakini baada ya dakika kadhaa nikajibiwa.
"Pouwa"
"Za wapi?"
"Nyumbani, nani mwenzangu?"
"Aah! Hujanifaham tu?"
"Hapana, nikumbushe"

Kimya kwa muda mchache nikawaza nijitambulishe vipi, kisha nikamjibu.
"Leo asubuhi kwenye vitafunwa ulinipa namba yako nikutafute"

Fasta nikajibiwa....
"Ahaa!.... Nimekumbuka, umefanya vizuri kunitafuta.

Moyo wangu ukatulia nikajifariji "kumbe kweli! Nimependwa" wee..! 🤣🤣🤣

Kabla sijajibu ikaingia sms nyingine.
"Kwahiyo ndio hivyo mi nimekuelewa sana naomba tu unikubalie"

Hapa nilishtuka kidogo nikaona aah wapi! Mbona kama muandiko haueleweki huu alafu kama ni kweli mbona kirahisi hivi.

Nikamuuliza "Kwahiyo unasemaje?" Akajibu "mi nakusikiliza wewe mi nimeshafikisha ujumbe wangu kama vipi hata leo tuonane, ukweli kila siku nikipita pale huwa nakuangalia sana sababu ya uzuri wako"

"Oyaa kwani we nani?" Nilijikuta naulizia kwa hasira maana kila wakati muandiko sikuuelewa kabisa.

"Mi si ndio nimekupa namba asubuhi pale lango kuu wakati nanunua vitafunwa kwako, we ukiniona utanikumbuka tu" akajibu 🤣🤣🤣

"Dadeki! Kwahiyo wewe ni mwanaume?" Nikauliza nikiwa na hasira zaidi, bahati mbaya sms haionyeshi muonekano 🤣🤣 akajibu fasta...
"Swali gani hilo? Ndio!"
"Oya umechemka mi mwenyewe kidume inaonekana wakati unampa hizo namba uliweka kwenye hela ambazo alinirudushia chenji mimi, mi mwenyewe nilijua nachat na yule dada!" 🤣🤣🤣🤣

Jamaa hakunijibu tena na mimi nikafuta namba hadi leo sijawahi kumjua huyu baharia ila tu nilisikitika uzembe wake wa kuogopa kumface yule dada ndio umesababisha yote haya🤣
😅😅😅😅
 
Daaah hatari sana haya mambo.. ila bora ulijiongeza mapema kugundua kwamba mbona muandikiko wa kiume huo kwa maana mngeweza kupanga mpk location ya kukutana ikawa kituko huko.
Unafika location unauliza umekaa wapi? Alaf unam-beep kuhakikisha... kuona hivi mwanaume mwenzako!!😃 mimi ningejua labda dem kampa simu mume wake anikamatae alafu na jamaa nae angewaza yake 😂😂😂
 
Hahahahaha😂😂😂😂😂😂 noma sana haiyo kweli mbwa kala mbwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom