Mbwa aliyemuuma kingunge

Mbwa aliyemuuma kingunge

Watoto wake walishasema kuwa, wakati wa kulala wakishafunga milango, mlinzi huwafungulia. Alfajiri sana, huwafungia bandani. Hao mbwa walikuwa hawamfahamu!
Yote kwa yote, kwa mchango wake kwa Nchi hii, si yeye, wala mke wake tiba zao zingeishia Muhimbili tu! Serikali ingepaswa kuwatafutia tiba hata nje ya Nchi! Na si hivyo tu, hata bendera ya taifa, ilipaswa imlilie kwa nusu mlingoti, hata kwa siku moja, kama si tatu!
Tusilione hili ghorofa ( Tanzania) limesimama hivi, wapo waliojitolea kulijenga!
Kuwa nje ya KIJANI, si sababu ya kunyimwa haki yake!
Siku ikifika hata matibabu yatolewe ujerumani unakwenda tu.. Kikubwa ni kuwa kwa wakati wake mzee kigunge alitimiza yale aliyoona ni sahihi kwake.
 
hahaa mzee Kingu alikuwa hatambui uwepo wa dini, hata mpwa wake nao hawatambui uwepo wake km owner wakaona wamng'ate tu@What goes around comes around
Kwa hiyo wote wanaoumwa na mbwa wao hawatambui uwepo wa dini?

Halafu nani kakwambia Kingunge alikuwa hatambui uwepo wa dini?
 
Tokea tulipopata taarifa kuwa mzee kingunge ngombale mwilu amelazwa Hospitali ya Taifa muhumbili baada ya kuumwa na mbwa wake akiwa nyumbani kwake, hadi leo tumepata taarifa kuwa mzee kingunge ameaga Dunia hatujapewa taarifa kuwa yule mbwa amechukuliwa hatua gani, nakama bado yupo palepale sehemu ya tukio yaani nyumbani kwa marehemu hataweza kufanya tukio kamahilo kwa mwanafamilia mwingine?
Toroka kwenu af uugue uone.
 
isije ikawa huyu mbwa alitumwa na watu wasiojulikana baada ya mzee kung'angania msimamo wa kutorejea kundini na kuunga mkono juhudi!
 
Dunia ya leo bado tunafuga mbwa? zipo spy camera za kila aina. huyo mbwa akibweka anayoka na panga?
Hata Donald Trump na Vladmir Putin wanalindwa na mbwa.
Vikosi vingi maalum vya polisi au askari jeshi vina mbwa wanaotekeleza majukumu yao kijeshi. Na wana vyeo.
Usilete mzaha na vitu usivyovijua.
 
Mnataka kumwangushia jumba bovu kijana wa watu.

Mbwa anamjua kijana wa kazi kuliko mwenye nyumba wakati kijana wa kazi ni wa kupita, ilitakiwa Mzee mwenye nyumba awe ni mmoja wa aliyezoewa na mbwa.

nimekuelewa mkuu nahisi niliteleza hapo kwenye kuandika mwenye kosa ni... sikumaanisha kisheria kisheria hapo kijana hana kosa nilichokuwa namaanisha ni vile alivyoenda nje ya utaratibu waliojiwekea (muda wa kuwafungia mbwa) ni binadamu alipitiwa tu kama mimi nilivyopitiwa katika uandishi hapo juu mpaka ukanielewa vibaya
 
Huyo mbwa amekosa ubinadamu. Hilo tendo alilolifanya sio la kiutu.
 
Hii habari ya mbwa kwangu bado najiuliza tu kwa kweli
 
Ndo maana napenda mbwakoko kanabweka ni balaa, hata kakiona mende katabweka hadi asubuhi, kosa akatize mjusi mbio utakakuta chumbani kwako kameshajikojolea tayari
 
Mbwa huyo atakuwa alipandwa na hasira kutokana na msongo wa mawazo, Si unajua Wanyama nao huwa wanawaza.Sasa labda aliona amalizie hasira zake kwa Bosi wake.
 
kwa wafugaji wa mbwa (haswa wa ulinzi sio wa show off) mtakuwa mmelielewa hili suala...

kwa kawaida na mara nyingi sisi tunaofuga haya majibwa (sio mbwa) maana yameshiba kweli kweli huwa tuna kasumba moja ya kumzoesha mbwa watu wasiozidi watatu ndan ya nyumba ili tuuu kuongeza ufanisi wake yani kuna kawaida kuwa mbwa akizoea watu wengi ufanisi (ukali) wake hupungua..

mara nyingi mbwa huzoeshwa watu watatu tuuu watakaokuwa wanampa huduma na kumfungia na kumfungua

ikifika saa nne usiku wote ambao mbwa hajawazoea inabidi msitoke nje sababu ndio mda wa kufunguliwa mbwa.. na kwa waliomzoea wanaamka asubuhi sa kumi na moja kuwafungia mbwa ili watu wengine waendelee na shughuli zao


kilichotokea kwa marehemu mzee kingunge... hao mbwa hawakuwahi hata kumuona kwan wamemzoea kijana wa kazi anayewashughulikia huwa wanafunguliwa saa 4 usiku na kufungiwa saa kumi na moja alfajiri kabla ya wanafamilia kuamka

siku ya tukio kijana anayewapa huduma wale mbwa alipitiwa na usingizi akachelewa kuwafungia huku mzee kingunge akijua kwa muda ule tayar watakuwa wamefungiwa akatoka ili aelekee mazoezin ile tu alipotoka akiwa anakaribia geti hamaadii mbwa wakamuona wakamvamia wakijua ni mwizi sababu hawajawahi kumuona hata siku moja licha ya kuwa yy ndio mwenye nyumba.... kosa sio la mbwa kwan walikuwa wanatimiza jukumu lao la ulinzi
Kwahyo kilicho muondoa mzee wetu ni nn?
Kichaa cha mbwa ama!!
 
Akili za mbwa ni kama za yule KING wa VIBAMIA Tanzania
 
Mzee alikua kashajichokea mbwa sababu tu. Na ndo maana akamtanguliza wife,
Kumbuka kinjekitile ngombare mwiru alikua kiongozi wa kamati ya utaalam juju kukiwezesha TANU kupata uhuru .
Hahaa mzee wa kupanga misafara?
Mola amuhifadhi
 
Huyo mbwa ni wazi hakuwa na mafunzo kama bado yupo anaweza kushambulia tena mbwa aliyefundishwa hufahamu harufu ya kila aliyetambulishwa kwake Huyo ni mbwa koko tu
 
Huyo mumbwa atakuwa alikuwa mgeni aise, mana hii sio tabia ya mbwa wa kibantu, au mzee alikuwa hajawahi kutana na huyo mumbwa
Inasemekana alikuwa anafunguliwa usiku na kuingizwa bandani alfajiri sana kwa maana hiyo mbwa alikuwa anamjua mlinzi tu mweehh!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom