BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,377
- 8,121
Mbunge wa Viti Maalum Jaquelin Msongozi (CCM) amependekeza sheria ya Tanzania kuhalalisha bangi itumike kama Tumbaku.
Msongozi ametoa kauli hiyo leo Septemba 14, 2022 bungeni wakati akichangia muswada wa sheria ya Mabadiliko ya sheria mbalimbali namba 2 wa mwaka 2022.
Hata hivyo si mara ya kwanza hoja hiyo kutolewa bungeni kwani ilishawahi kutolewa na wabunge Jumanne Kishimba (Kahama), Joseph Msukuma (Geita Vijijini) na mbunge wa zamani wa Nkasi Kaskazini Ali Keisy.
Akichangia leo kwenye marekebisho ya sheria ya dawa za kulevya, mbunge huyo amesema Kuna Mataifa ambayo yaliruhusu bangi kwa faida yao na sasa wanaingiza Kodi.
"Tuige mfano wa Nchi kama Jamaica na Malawi, wenyewe wameruhusu bangi na sasa hakuna shida kwao, tuifanye ikubarike na kama Kuna shida tuandike tahadhari kama ilivyo kwa sigara,” amesema.
Mbunge huyo ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria amesema ikifanyika hivyo hata nchi inaweza kupata mapato.
Akijibu hoja hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk Eliezer Feleshi amesema bado hakuna sheria ya kuruhusu bangi hasa kwenye biashara isipokuwa kuna sheria inaruhusu kama bangi inahitajika kwa kazi maalumu.
Msongozi ametoa kauli hiyo leo Septemba 14, 2022 bungeni wakati akichangia muswada wa sheria ya Mabadiliko ya sheria mbalimbali namba 2 wa mwaka 2022.
Hata hivyo si mara ya kwanza hoja hiyo kutolewa bungeni kwani ilishawahi kutolewa na wabunge Jumanne Kishimba (Kahama), Joseph Msukuma (Geita Vijijini) na mbunge wa zamani wa Nkasi Kaskazini Ali Keisy.
Akichangia leo kwenye marekebisho ya sheria ya dawa za kulevya, mbunge huyo amesema Kuna Mataifa ambayo yaliruhusu bangi kwa faida yao na sasa wanaingiza Kodi.
"Tuige mfano wa Nchi kama Jamaica na Malawi, wenyewe wameruhusu bangi na sasa hakuna shida kwao, tuifanye ikubarike na kama Kuna shida tuandike tahadhari kama ilivyo kwa sigara,” amesema.
Mbunge huyo ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria amesema ikifanyika hivyo hata nchi inaweza kupata mapato.
Akijibu hoja hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk Eliezer Feleshi amesema bado hakuna sheria ya kuruhusu bangi hasa kwenye biashara isipokuwa kuna sheria inaruhusu kama bangi inahitajika kwa kazi maalumu.