Mbunge wa Momba, David Silinde rasmi ahamia CCM

Mbunge wa Momba, David Silinde rasmi ahamia CCM

Mm chama tawala na wapinzani kwangu wote ni umbwa tu...

Maana juzi kama sio jana imeletwa nyuzi umu ya kushambuliwa na fisi wamama waliokua wanaenda kuteka maji nyakati za usiku maana maji ni tabu wakati huo huo hii mijamaa inayohama hama ina mishahara minene na posho za ajabu ajabu na huduma kama zote alaf wanapigapiga mayowe tu umo bungeni
 
Hana jipya.nchi hii wapo wengi wanaoweza kulinda utu na haki ya mtanzania.aende zake.
 
Yaani kahamishwa kiti hapo hapo, hakuna kufuata taratibu za kisheria tena, Ndugai ndie Spika wa ajabu kuwahi kutokea kwenye bunge la JMT.
Ni wa hovyo Sana yule jamaa.
Mimi nilivyoona anaongea pumba muda wote niliacha kuangalia bunge.
 
Ls
Mh.Silinde leo ameomba rasmi kujiunga na Chama Mapinduzi, na amesema yupo tayari kukitumikia Chama Cha Mapinduzi kwa nguvu zote.

Spika Ndugai amemkaribisha na kumhamisha kwenye viti vya Upinzani kumpeleka kwenye viti vinavyokaliwa na wabunge wa CCM.

Hivyo kuanzia leo rasmi Silinde ni mbunge wa CCM na atakaa upande wa wabunge wa CCM.

Live kutoka bungeni.

====
Mbunge wa Jimbo la Momba, Mkoani Songwe David Ernest Silinde kwa tiketi ya CHADEMA ametangaza kujiunga CCM. Davidi amekuwa mbunge kwa tiketi ya CHADEMA tangu mwaka 2010

Mbunge huyo alijiuzulu nafasi zote za uongozi ndani ya CHADEMA mwezi Mei, baada ya wabunge wenzake kumtaka kufanya hivyo kwa kutotii agizo la kutokwenda bungeni

Wakati anajiuzulu alisema wananchi ndio walimtuma bungeni, hivyo hata akikosa udhamini wa CHADEMA, atatumia chama kingine
Lakini hivi sasa hana haki ya kuwa mbunge.....

Kwa mujibu wa Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano, 1977

Ila Spika Ndugai kwa kuendelea kumbakisha Bungeni, ameamua kuisigina Katiba ya Jamhuri ambayo aliapa kuitii.

Ndiyo sababu wameamua kupeleka Muswada Bungeni, wa kutaka na yeye Spika, asishtakiwe na mahakama yoyote hapa nchini, kwa kuvunja Katiba ya nchi!
 
Ila hili bunge la ajabu kweli yaani,wanasema wanampongeza rais lkn kila anayesimama anapambana na mboweanasahau kama ni kipindi cha kumpongeza rais
 
Anatafuta huruma ya ccm arudi mjengoni
Umetoka chuo ajira yko ya kwanza ubunge
Akiukosa Sasa ataishiji

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Uteuzi wa mgombea uraisi ndani ya chadema Mchungaji Msigwa kapigwa pini hata vikiletwa vitu vyake jamii forums vinakuwa deleted na moderators

Inaelekea wanataka zisikike taarifa za mgombea Tundu Lisu tu hawataki za Msigwa lakini hawamtendei haki kwa chama kinachojiita Cha kidemokrasia inaelekea jamii forums Kuna moderators team Lisu wanamdhibiti Msigwa asiwe hewani na jinsi uthibiti kwake ulivyo mkubwa sidhani Kama hata ubunge Iringa mjini Kama atapitishwa inaonekana Kuna agenda dhidi ya Msigwa kutangaza kugombea uraisi imekuwa nongwa Wanatangaza watu wagombee wakitaka visasi na vinyongo vinaanza

Hili zoezi la ugombea uraisi halitaiacha chadema salama litakikata chama vipande

Sababu Msigwa kanda ya nyanda za juu ana nguvu Sana Tena mno Team Lisu wasidhani watapata kura kirahisi nyanda za juu kusini kwa kumchezea rafu Msigwa watakiona Cha mtema kuni

Chadema wanachezea wababe wa kanda .Kanda ya ziwa wamecheza na Rwakatare na profesa Baregu na wahanga wa MV butiama hawakwenda hata msibani Hadi mbunge akatimuka kuhamia CCM inakula Kwao.Kanda ya kaskazini wamecheza na Dr Slaa,Lowasa,selasini na Komu na Mbatia ya Pwani wamecheza na profesa Safari na Sumaye , Zanzibar na Pemba wamecheza na Duni Haji na watakiona Cha mtema kuni Sasa wanahamia nyanda za juu kusini kwa Msigwa navSilinde wasubiri majibu uchaguzi mkuu kila sehemu wamevuruga na kote Kuna Giants

Safari hii chadema itapata kura chache Sana masna wafuasi wa hao Giants wataipabwakati mgumu chadema kwenye maeneo Yao

Silinde kuhama kaondoka na team
Kusini wakacheza na Cecil Mwambe na Makamu Mwenyekiti wa CUF



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mh.Silinde leo ameomba rasmi kujiunga na Chama Mapinduzi, na amesema yupo tayari kukitumikia Chama Cha Mapinduzi kwa nguvu zote.

Spika Ndugai amemkaribisha na kumhamisha kwenye viti vya Upinzani kumpeleka kwenye viti vinavyokaliwa na wabunge wa CCM.

Hivyo kuanzia leo rasmi Silinde ni mbunge wa CCM na atakaa upande wa wabunge wa CCM.

Live kutoka bungeni.

====
Mbunge wa Jimbo la Momba, Mkoani Songwe David Ernest Silinde kwa tiketi ya CHADEMA ametangaza kujiunga CCM. Davidi amekuwa mbunge kwa tiketi ya CHADEMA tangu mwaka 2010

Mbunge huyo alijiuzulu nafasi zote za uongozi ndani ya CHADEMA mwezi Mei, baada ya wabunge wenzake kumtaka kufanya hivyo kwa kutotii agizo la kutokwenda bungeni

Wakati anajiuzulu alisema wananchi ndio walimtuma bungeni, hivyo hata akikosa udhamini wa CHADEMA, atatumia chama kingine

Galasa lingine hilo.
 
Back
Top Bottom