Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,897
- 941
Mbunge wa Jimbo la Momba, Mhe. Condester Michael Sichalwe mara baada ya kumalizika kwa Bunge Novemba 2023 alipokea gari la kubeba wagonjwa la Halmashauri ya Momba.
Gari hilo la kubeba wagonjwa la Halmashauri ya Momba, Condester Sichalwe alilipokea kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson na Waziri wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa.
"Watu wa Halmashauri ya Momba hawatachangishwa tena kuhusiana na gharama ya Mafuta ya Ambulance kupeleka watu Hospitali. Gari hili nimelipokelea Bungeni mahali ninapoombea hoja nikiwa na dereva wa Momba, DMO" - Mhe. Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Jimbo la Momba Mkoa wa Songwe.