Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ataka matokeo ya Urais yahojiwe Mahakamani

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,692
218,210
Kauli hiyo ya kishujaa ameitoa ndani ya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akichangia kwenye bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu

Pamoja na hilo pia amependekeza umuhimu wa kuwa na Tume huru ya uchaguzi , ambapo amedai kwamba pamoja na yeye kushinda kwa kishindo kwenye nafasi ya ubunge kwa uchaguzi wa 2010 na 2015 lakini kabla ya matokeo kutangazwa kwa mbinde kulitokea mauaji ya mtu mmoja na ulemavu kwa watu watatu ambao anawahudumia hadi leo

Note : Tunashindwa kuweka video hapa kwa vile bunge la Tanzania limedhibitiwa na linaendeshwa kama vikao vya siri

----
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu ‘Sugu’ ametaka sheria za uchaguzi zibadilishwe ili matokeo ya urais kupingwa mahakamani kama ilivyo kwa ubunge.

Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Aprili 2, 2020 katika mjadala wa bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu mwaka 2020/21.

Sugu ambaye pia ni mwanamuziki amesema mbali na matokeo kupingwa, uwepo wa tume huru ya uchaguzi utafanya uchaguzi uwe huru na haki.

“Mbeya hamjawahi kunipa ushindi kwenye silver plate, mwaka 2010 alikufa mtu mmoja kwa ajili ya kulinda kura, uchaguzi wa mwaka 2015 walemavu watatu hadi leo bado nawahudumia.”

“Kwa hiyo tunataka tume huru yenye uwezo wa kuchagua wasimamizi wake na watumishi wake yenyewe ila isiteuliwe,” amesema Sugu.

Mwananchi
 
Hongera Sugu. Wote tudani na kudai na kudai bila kuchoka:. Katiba Mpya, Tume huru ya uchaguzi na kuhoji matokeo ya Uraisi mahakamani.....
Wakati wa uchaguzi kura zote zikiwemo za raisi zihesabiwe na kubandikwa vituoni
 
Naomba wanasheria mnisaidie hivi walio andika katiba yetu walitoa sababu zipi za matokeo ya urais kutopingwa mahakamani?

Hili swali linaniumiza kichwa maana naona wazi kipengele hiki kinaenda kuiletea nchi matatizo hapo baadae.
 
Naomba wanasheria mnisaidie hivi walio andika katiba yetu walitoa sababu zipi za matokeo ya urais kutopingwa mahakamani?

Hili swali linaniumiza kichwa maana naona wazi kipengele hiki kinaenda kuiletea nchi matatizo hapo baadae.
Umeona wapi mwizi anataka kuhojiwa? Hiyo ndiyo njia yao ya kujikinga kwa wizi wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba wanasheria mnisaidie hivi walio andika katiba yetu walitoa sababu zipi za matokeo ya urais kutopingwa mahakamani?

Hili swali linaniumiza kichwa maana naona wazi kipengele hiki kinaenda kuiletea nchi matatizo hapo baadae.
Kwa sababu wanakua wameiba kura hadi kupitiliza, rejea incidences za 2015. Anayebisha aje hapa
 
Kauli hiyo ya kishujaa ameitoa ndani ya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akichangia kwenye bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu

Pamoja na hilo pia amependekeza umuhimu wa kuwa na Tume huru ya uchaguzi , ambapo amedai kwamba pamoja na yeye kushinda kwa kishindo kwenye nafasi ya ubunge kwa uchaguzi wa 2010 na 2015 lakini kabla ya matokeo kutangazwa kwa mbinde kulitokea mauaji ya mtu mmoja na ulemavu kwa watu watatu ambao anawahudumia hadi leo

Note : Tunashindwa kuweka video hapa kwa vile bunge la Tanzania limedhibitiwa na linaendeshwa kama vikao vya siri

----
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu ‘Sugu’ ametaka sheria za uchaguzi zibadilishwe ili matokeo ya urais kupingwa mahakamani kama ilivyo kwa ubunge.

Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Aprili 2, 2020 katika mjadala wa bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu mwaka 2020/21.

Sugu ambaye pia ni mwanamuziki amesema mbali na matokeo kupingwa, uwepo wa tume huru ya uchaguzi utafanya uchaguzi uwe huru na haki.

“Mbeya hamjawahi kunipa ushindi kwenye silver plate, mwaka 2010 alikufa mtu mmoja kwa ajili ya kulinda kura, uchaguzi wa mwaka 2015 walemavu watatu hadi leo bado nawahudumia.”

“Kwa hiyo tunataka tume huru yenye uwezo wa kuchagua wasimamizi wake na watumishi wake yenyewe ila isiteuliwe,” amesema Sugu.

Mwananchi
Tena ikithibitika kwamba hizo kura ziliibwa hayo matokeo yafutiliwe mbaliiiiiiiiiiiii

Ccm najua walivyozoea wizi hawatakubali hilo jambo
 
Kama ni kikao cha siri we hii habari uliipataje? Mbona unapenda kupotosha potosha! Mmekosa sehemu ya kupapasa kabisa?
Isingekuwa uzembe na udhaifu wa Jakaya Kikwete mwaka 2015 wakati wa mchakato wa Rasimu ya Katiba Mpya, haya maswali ya akina Sugu yasingekuwapo.

Ni nini kilimpata JK mpaka akashindwa kumalizia Katiba ya Wananchi?
 
Back
Top Bottom