Jimbo la Igunga Sasa Kujenga Ofisi za CCM

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944
IGUNGA: "TUMEAMUA KUACHANA NA VIKAO VYA CHINI YA MITI NA KWENYE STOO ZA PAMBA".

Mbunge wa Jimbo la Igunga Mhe Nicholaus George Ngassa ameendelea na Ziara ya Kikazi Jimboni, Ziara inayoambatana na zoezi la ujenzi wa Ofisi za Kata za Chama cha Mapinduzi (CCM). Akiongea na Wanachama wa CCM Kata ya Nguvumoja Leo tarehe 21 Mei, 2023 Mheshimiwa Ngassa (MB) amesema;

"... Ndugu zangu, tuendelee kushirikiana katika ujenzi wa Ofisi zetu za Kata... Igunga tuwe mfano kwenye kufanikisha jambo kubwa kama hili Nchini ambapo Kila Kata itakuwa na Ofisi ya Chama ya kisasa yenye ukumbi wa mikutano, Ofisi za Chama na Jumuiya zake na vibanda vya biashara (flames). Tufikirie kuachana na utamaduni uliozoeleka wakufanya vikao chini ya miti au kwenye stoo za pamba..."

Mheshimiwa Ngassa (MB) amehitimisha Ziara ya Kikazi ya Siku Tatu kwenye Kata Nne Jimboni na kurejea Dodoma kuendelea na Vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"KAZI NA MAENDELEO"

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Igunga

WhatsApp Image 2023-05-21 at 18.00.49.jpeg
WhatsApp Image 2023-05-21 at 18.00.50.jpeg

WhatsApp Image 2023-05-21 at 18.00.54.jpeg

WhatsApp Image 2023-05-21 at 18.00.59.jpeg

WhatsApp Image 2023-05-21 at 18.00.59.jpeg
WhatsApp Image 2023-05-21 at 18.01.06.jpeg
WhatsApp Image 2023-05-21 at 18.01.08.jpeg
 
Hata afanye nn Mbunge Ngasa hawezi shinda Igunga 2025. He is very unpopular

Mbunge Ngasa ALISHINDWA vibaya kura za maoni na Henry Kobeho na Dalali Kafumu lkn yy akateuliwa.Hawezi mshinda Kabeho wala Kafumu 2025.

Dr Kafumu alikosana na Rais Magufuli pale alipo mtembelea mbunge Lema gerezani Kisongo ktk kesi ya Lema ya ‘kuoteshwa kama Rais Magufuli asipo jirekebisha kwneye ukatili wake atakufa’

Lema alikua kwenye kamati ya Wizara ya Nishati iliyokuwa chini ya Dr Kafumu na Vick Kamata Likwelile kwa hiyo walimtembelea gerezani mwana kamati mwenzao.

Kwa kumtembelea Lema hawa viongozi wa kamati ya Nishati walitoswa na Magufuli kwa ukatili kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom