Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,786
- 1,710
Mambo si shwari ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) jimbo la Mbarali mkoani Mbeya baada ya mbunge wa jimbo hilo Mheshimiwa Dickson Kilufi kukamatwa na jeshi la polisi na kusindikizwa mjini Mbeya kwa ulinzi mkali jioni ya tarehe 7-10-2011 na kufikishwa Mahakamani leo hii.
Mbunge huyo amekamatwa na jeshi la polisi mkoa wa Mbeya kwa tuhuma za kutishia kumuua kwa bastola Afisa Mtendaji wa Kata ya Ruiwa Wilaya ya Mbarali Bwana Jordan Matweve .
Imedaiwa kuwa mtego wa kumnasa mbunge huyo uliwekwa na jeshi la polisi mapema leo na kufanikiwa kumnasa mbunge huyo na kumpeleka polisi kwa ulinzi mkali na leo amefikishwa mahakamani na hadi sasa yupo rumande baada ya ombi la dhamana kukataliwa
Mbunge huyo amekamatwa na jeshi la polisi mkoa wa Mbeya kwa tuhuma za kutishia kumuua kwa bastola Afisa Mtendaji wa Kata ya Ruiwa Wilaya ya Mbarali Bwana Jordan Matweve .
Imedaiwa kuwa mtego wa kumnasa mbunge huyo uliwekwa na jeshi la polisi mapema leo na kufanikiwa kumnasa mbunge huyo na kumpeleka polisi kwa ulinzi mkali na leo amefikishwa mahakamani na hadi sasa yupo rumande baada ya ombi la dhamana kukataliwa