WAKAZI wa Kata ya Kivule, jijini Dar es Salaam, wamelalamikia kitendo cha madereva wa daladala kuwatoza wanafunzi sh. 300 kwa kisingizio cha ubovu wa barabara.
Wakizungumza katika kikao cha kuchangia ununuzi wa Kivuko cha Kipunguni Mtaa wa Mara Picknic kilichoitishwa na Diwani wa Kivule, Nyansika Gaitama, wakazi hao walisema hali hiyo kwa kiasi kikubwa inaweza kusababisha wazazi kushidwa kupeleka watoto wao shule.
Kutokana na hali hiyo, mmoja wa wakazi hao Mwalimu Mulokozi aliitaka Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), kupeleka watendaji wake huko ili kujionea hali halisi badala ya kubaki maofisini.
Katika uchangishaji wa kivuko, jumla ya sh milioni 3.6 zilipatikana ambapo kati ya hizo Diwani alichangia sh.100,000.
Diwani Gaitama alisema kukamilika kwa kivuko hicho kutawezesha barabara hiyo kupitika hadi kipidi cha mvua.
Hata hivyo, alisema zinahitajika sh milioni 11.6 ili kukamilika kwa ujenzi wa kivuko hicho ambapo alitoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kuchangia.
Wananchi wa Ukonga wamekuwa kwa muda mrefu wakipata matatizo makubwa kutokana na miundombinu mibovu ya barabara kiasi kwamba katika nyakati za mvua hususan masika nauli ya daladala imekuwa ikifika hadi shilingi 1000 kwa safari moja.Mbali ya kivule maeneo mengine yanayoathirika na hali hii kwa ubovu wa barabara ni Mombasa kwenda Moshi bar hadi kwa Mkolemba, Mombasa hadi kwa diwani banana kwenda Machimbo na banana hadi kitunda.
Pamoja na malalamiko ya muda mrefu lakini mbunge wa jimbo hilo mwanamama Eugene Mwaiposa amekuwa hachukui hatua yoyote hata ya kuzungumza na wananchi wake kiasi cha kulifanya jimbo hilo kuwa hatarini kupokonywa mikononi mwa CCM
Source:Tanzania Daima.
Wakizungumza katika kikao cha kuchangia ununuzi wa Kivuko cha Kipunguni Mtaa wa Mara Picknic kilichoitishwa na Diwani wa Kivule, Nyansika Gaitama, wakazi hao walisema hali hiyo kwa kiasi kikubwa inaweza kusababisha wazazi kushidwa kupeleka watoto wao shule.
Kutokana na hali hiyo, mmoja wa wakazi hao Mwalimu Mulokozi aliitaka Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), kupeleka watendaji wake huko ili kujionea hali halisi badala ya kubaki maofisini.
Katika uchangishaji wa kivuko, jumla ya sh milioni 3.6 zilipatikana ambapo kati ya hizo Diwani alichangia sh.100,000.
Diwani Gaitama alisema kukamilika kwa kivuko hicho kutawezesha barabara hiyo kupitika hadi kipidi cha mvua.
Hata hivyo, alisema zinahitajika sh milioni 11.6 ili kukamilika kwa ujenzi wa kivuko hicho ambapo alitoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kuchangia.
Wananchi wa Ukonga wamekuwa kwa muda mrefu wakipata matatizo makubwa kutokana na miundombinu mibovu ya barabara kiasi kwamba katika nyakati za mvua hususan masika nauli ya daladala imekuwa ikifika hadi shilingi 1000 kwa safari moja.Mbali ya kivule maeneo mengine yanayoathirika na hali hii kwa ubovu wa barabara ni Mombasa kwenda Moshi bar hadi kwa Mkolemba, Mombasa hadi kwa diwani banana kwenda Machimbo na banana hadi kitunda.
Pamoja na malalamiko ya muda mrefu lakini mbunge wa jimbo hilo mwanamama Eugene Mwaiposa amekuwa hachukui hatua yoyote hata ya kuzungumza na wananchi wake kiasi cha kulifanya jimbo hilo kuwa hatarini kupokonywa mikononi mwa CCM
Source:Tanzania Daima.