Hadha ya ubovu wa barabara kivule

isky

JF-Expert Member
Mar 31, 2014
884
737
Ndugu wana jamvi nikiwa kama mmoja wa wakazi wa kivule naomba mawazo yenu pengine ninyi mliwahi fanikiwa mlipokuwa na shida kama ya kwetu.

Ili kufika kivule njia kuu ni moja kupitia banana - kitunda - kivule, ni barabara yenye urefu wa takribani km 12hv

Kero kubwa tunayokabiliana sisi wakazi wa maeneo haya ni ubovu wa barabara ambao umepitiliza na hakuna kiongozi yoyote anayeonekana kujali licha ya kuwepo kwa hospitali kubwa iliyojengwa enzi za mwendazake na kupewa hadhi ya hospitali ya wilaya ila kwa hali ya barabara iliyopo kama mgonjwa akipakiwa kwenye ambulance kutokea kivule hadi amana ama muhimbili ni dhahiri hali yake itakuwa mbaya zaidi kwani kutokana na kuchekewa njiani na kurushwarushwa awapo ndani ya ambulance.

Barabara hii ipo katika ilani ya chama kuwekwa lami kwa ukamilifu ila hakuna dalili, hapo Kati alimfanya ziara mkuu wa mkoa Chalamila wakati akizungumzia ubovu wa barabara akasema wananchi tutulie tungetaka barabara safi tungejenga magomeni. Mbunge wetu haoneshi ushirikiano kwa wanakivule, diwani haonekani, mkurugenzi inawezekana anaungana na mkuu wa mkoa ki mtazamo.

Nina Imani ya kuwa humu kuna wabobezi wa mambo na kupitia jukwaa hili sauti hufika mbali.

Tunaomba ushauri nini tufanye kuilazimisha serekali yetu sikivu itukumbuke wakazi wa kivule?

Nawasiliaha.
 
Kuna hii barabara kutoka Mombasa mpaka bombambili hadi mbondole ni balaaa, yaani ukipita hiyo barabara ukiwa kwenye pikipiki mwili wote lazima uume kama mtu aliyefanya kazi ngumu.
 
Cha muhimu hii serikali ya ccm inatudharau sana na ni kuipiga chini kwa ustawi wa siku zijazo bila hivyo tutapata tabu sana

Viongozi wote wa serikali na WA chama wanafika kila siku kukagua miradi ya maendeleo hususani hii hospital ila hakuna jipya wanalotatua wanapongezana tuu

Hospitali yenyewe baada ya Yale majengo ya awali kuwa na usimamizi mzuri, mengine yote yanayojengwa sasa yapo chini ya kiwango kwa macho tuu unaona

Barabara inatesa sana huwezi amini kama upo ndani ya Jiji

Rai yangu,hiki kikombe tutakiepuka endapo tutawapuuza Hawa ccm maana kila siku huku kivule wao wanafanya kampeni sijui zinasaidia nn

WanaKivule poleni kwa mateso mnayofanyiwa na serikali yenu
 
Ndugu wana jamvi nikiwa kama mmoja wa wakazi wa kivule naomba mawazo yenu pengine ninyi mliwahi fanikiwa mlipokuwa na shida kama ya kwetu.

Ili kufika kivule njia kuu ni moja kupitia banana - kitunda - kivule, ni barabara yenye urefu wa takribani km 12hv

Kero kubwa tunayokabiliana sisi wakazi wa maeneo haya ni ubovu wa barabara ambao umepitiliza na hakuna kiongozi yoyote anayeonekana kujali licha ya kuwepo kwa hospitali kubwa iliyojengwa enzi za mwendazake na kupewa hadhi ya hospitali ya wilaya ila kwa hali ya barabara iliyopo kama mgonjwa akipakiwa kwenye ambulance kutokea kivule hadi amana ama muhimbili ni dhahiri hali yake itakuwa mbaya zaidi kwani kutokana na kuchekewa njiani na kurushwarushwa awapo ndani ya ambulance.

Barabara hii ipo katika ilani ya chama kuwekwa lami kwa ukamilifu ila hakuna dalili, hapo Kati alimfanya ziara mkuu wa mkoa Chalamila wakati akizungumzia ubovu wa barabara akasema wananchi tutulie tungetaka barabara safi tungejenga magomeni. Mbunge wetu haoneshi ushirikiano kwa wanakivule, diwani haonekani, mkurugenzi inawezekana anaungana na mkuu wa mkoa ki mtazamo.

Nina Imani ya kuwa humu kuna wabobezi wa mambo na kupitia jukwaa hili sauti hufika mbali.

Tunaomba ushauri nini tufanye kuilazimisha serekali yetu sikivu itukumbuke wakazi wa kivule?

Nawasiliaha.
 
Ndugu wana jamvi nikiwa kama mmoja wa wakazi wa kivule naomba mawazo yenu pengine ninyi mliwahi fanikiwa mlipokuwa na shida kama ya kwetu.

Ili kufika kivule njia kuu ni moja kupitia banana - kitunda - kivule, ni barabara yenye urefu wa takribani km 12hv

Kero kubwa tunayokabiliana sisi wakazi wa maeneo haya ni ubovu wa barabara ambao umepitiliza na hakuna kiongozi yoyote anayeonekana kujali licha ya kuwepo kwa hospitali kubwa iliyojengwa enzi za mwendazake na kupewa hadhi ya hospitali ya wilaya ila kwa hali ya barabara iliyopo kama mgonjwa akipakiwa kwenye ambulance kutokea kivule hadi amana ama muhimbili ni dhahiri hali yake itakuwa mbaya zaidi kwani kutokana na kuchekewa njiani na kurushwarushwa awapo ndani ya ambulance.

Barabara hii ipo katika ilani ya chama kuwekwa lami kwa ukamilifu ila hakuna dalili, hapo Kati alimfanya ziara mkuu wa mkoa Chalamila wakati akizungumzia ubovu wa barabara akasema wananchi tutulie tungetaka barabara safi tungejenga magomeni. Mbunge wetu haoneshi ushirikiano kwa wanakivule, diwani haonekani, mkurugenzi inawezekana anaungana na mkuu wa mkoa ki mtazamo.

Nina Imani ya kuwa humu kuna wabobezi wa mambo na kupitia jukwaa hili sauti hufika mbali.

Tunaomba ushauri nini tufanye kuilazimisha serekali yetu sikivu itukumbuke wakazi wa kivule?

Nawasiliaha.

Ambatanisha na picha au Video za hiyo Barabara Mkuu
 
Back
Top Bottom