Mbunge wa Bunda ameidhalilisha CCM na anapaswa kukatwa jina lake uchaguzi ujao

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,301
9,727
Ndugu Zangu Watanzania: Umuhimu wa Uongozi Mzuri na Viongozi wa Kuaminika

Katika kipindi hiki cha mjadala wa kisiasa na kuleta maendeleo nchini Tanzania, ni muhimu sana kwa viongozi wetu, hasa wabunge, kuelewa jukumu kubwa wanalolobeba katika jamii. Wabunge ni wawakilishi wa wananchi, sauti ya watu, na wana jukumu la kuwawakilisha ipasavyo kwa masuala muhimu ya kitaifa.

Sauti ya mbunge ni kubwa, na wana uwezo wa kuhamasisha na kufikisha ujumbe kwa serikali na jamii kwa ujumla. Wanawakilisha wananchi wote, waliowapigia kura na hata wale ambao hawakupiga kura. Hivyo, wanapaswa kuwa makini na maneno yao na vitendo vyao, kwani yanaweza kuwa na athari kubwa kwa jamii.

Wakati wa kutoa matamshi au kauli hadharani, ni muhimu kwa wabunge kuzingatia uhalisia wa mambo wanayoyazungumza. Wanapaswa kufikiri kwa kina kabla ya kutoa kauli, kwa kuwa maneno yao yanaweza kusababisha athari na hata sintofahamu katika jamii. Uongozi mzuri unahitaji hekima, busara, na uvumilivu.

Mbunge anahusika na majukumu mengi, kutoka kwenye vikao vya wazi hadi vikao vya siri. Wanapaswa kuwa na ufahamu wa mambo mazito na mepesi, na wanahitaji kuwa timamu kiakili katika majukumu yao. Hata katika hali ya furaha au hasira, wanapaswa kujizuia na kudhibiti hisia zao, ili kuepuka kuleta mtafaruku au machafuko.

Ni wazi kwamba viongozi wetu wanapaswa kuwa na kifua cha kuweza kuvumilia mawazo tofauti, kuheshimu maoni ya wengine, na kutoa kauli zinazojengwa kwa msingi wa hoja na tafakari. Wanapaswa kuwa viongozi wa mfano kwa jamii, na hivyo ni muhimu kwa wao kuwa watulivu na kufanya maamuzi sahihi.

Hata hivyo, matamshi na vitendo visivyo na uzito vinaweza kuathiri sifa za mbunge na chama chake. Hivyo, ni jukumu la chama kuhakikisha kuwa viongozi wake wanazingatia heshima, misingi ya uongozi, na wajibu wao kwa wananchi. Kujitokeza hadharani na kusema mambo ambayo si sahihi ni kujidhalilisha na kuathiri imani ya wananchi.

Tunapaswa kuhimiza viongozi wetu kuchukua jukumu lao kwa uzito na kujitahidi kuwa viongozi wa kuaminika na wa heshima. Matamshi yao yanaweza kuwa na athari kubwa katika jamii, hivyo wanapaswa kutumia nafasi yao kwa hekima na umakini. Tuna wajibu wa kuwachagua viongozi wenye kujali maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.

Tuzidi kujitahidi kuwa na viongozi waadilifu na wenye ufahamu wa majukumu yao, ili kusongesha nchi yetu mbele kwenye maendeleo na amani. Tuwe macho na kuhakikisha kuwa wawakilishi wetu wanatimiza ahadi zao na kuendeleza ustawi wa nchi yetu.

Imetolewa na Lucas Hebel Mwashambwa, Mtanzania Mzalendo.

Simu: 0742-676627.

Pia, soma: Chacha Maboto, Mbunge wa Bunda (CCM): Lugha ya kwenye Mkataba wa DP World sikuielewa, mnisamehe
 
Kasema ukweli kabisa. Wabunge wengi huwa wanaburuzwa ili kuendana na matakwa ya rais hata kwenye upuuzi kama huu wa bandari. Ukiwahoji wabunge mmojammoja utagundua kuwa huu mkataba waliupitisha kwa kuburuzwa na spika ili kutimiza matakwa ya rais ya kuuza bandar.
 
Watu wote tunajua kuwa wabunge walipitisha ule mkataba bila kujua kulichomo Huyu ameamua tu kuwa mkweli.

Ule Mkataba hata leo ukimpa mbunge mmoja mmoja akufafanulie kipengele kwa kipengele, nakuhakikishia 90% ya wabunge hawajui chochote.

Ukweli ni kwamba hii Nchi Kuna ujinga mwingi sana
 
Kasema ukweli kabisa.wabunge wengi huwa wanaburuzwa ili kuendana na matakwa ya rais hata kwenye upuuzi kama huu wa bandari.Ukiwahoji wabunge mmojammoja utagundua kuwa huu mkataba waliupitisha kwa kuburuzwa na spika ili kutimiza matakwa ya rais ya kuuza bandar
Kama aliburuzwa alikuwa na sababu gani ya kwenda kuongea aliyo yaongea? Kwa faida ya nani? Kama hakuridhishwa na mswaada kwanini alipigia kura ? Kwanini siku ya kura asinge kaa kwenye makazi yake tu bila kuingia bungeni? Sasa kama hajuwi alichopigia kura ni vipi atapata ujasiri wa kwenda kuomba nafasi nyingine ya kuwa mbunge uchaguzi ujao ? Ni vipi aaminiwe kuwa mbunge kwa awamu nyingine wakati hawezi kutimiza majukumu yake ya kibunge?
 
Nikupongeze kwa kukumbuka kuweka namba ya simu. Naona vijana wa hovyo mnaendekeza uchawa mkiamini kuwa ndiyo njia ya kutoka kimaisha badala ya kufanya kazi kwa bidii.

Ni kawaida kwa muungwana kukiri alipokosea na kuomba radhi kuliko kushupaza shingo kupigania jambo usilolielewa.
 
Ajihudhulu ubunge ili upewe wewe?.
Hapana siyo nipewe mimi bali apewe mwingine mwenye uwezo na anayekidhi vigezo vya ubunge anayejuwa kero, changamoto na matatizo ya wana Bunda,anayejuwa nini atawafanyia wanaunda katika yale yote yaliyochangamoto kwao. Aliye mkazi na mwenyeji wa Bunda na ambaye analifahamu kwa undani jimbo lake.
 
Ndugu zangu watanzania,

Ukiwa mbunge wa jimbo lazima ufahamu na kutambua kuwa wewe ni kiongozi mkubwa sana ndani ya jamii,sauti yako ni kubwa ,una uwezo wa kufikisha chochote na kikasikilizwa na kupokelewa na Serikali,wewe ni sauti ya wananchi na mwakilishi wa watu waliokupigia kura na ambao hawajakupigia kura. Hivyo usimamapo popote pale bila kujali umejaa furaha kiasi gani au hasira kiasi gani ndani ya kifua chako ,wakati wote na muda wote unapaswa kuuchunga sana ulimi na mdomo wako.

Unapaswa kuwa mwenye kifua ,mwenye kupima kauli kabla ya kutamka hadharani,mwenye kudhibiti furaha,jaziba ,mihemuko,sifa na hata kujiepusha kutoa neno au maneno ambayo yataleta athari na sintofahamu katika jamii. Mbunge ni mtu anayeshiriki vikao vingi vya wazi na siri,mwenye kujuwa mambo mengi mazito na mepesi,machungu na matamu,ya viapo na miiko,ya siri na nyeti. Hivyo mbunge ni mtu anayepaswa kuwa timamu kiakili hata akiwa amelewa hapaswi kuendeshwa na pombe kichwani pasipo tafakari au kujielewa nini anatamka na anakusudia kutamka.

Kitendo cha mbunge kusimama Hadharani na kusema kuwa Alipitisha na kupigia kura kitu ambacho alikuwa Hakijuwi ni fedheha na aibu kwa mbunge mwenyewe ,ni kujidhalilisha na kukidhalilisha chama na wanachama waliomuamini na kumpitisha katika kura za maoni,ni kuwavunja moyo waliompigia kura kuwa mwakilishi wao Bungeni na kuwakatisha Tamaa viongozi wetu wa chama wanaokipigania chama usiku na mchana ,kwa jasho na machozi katika kuhakikisha kuwa chama kinapata ushindi katika kila uchaguzi wa ngazi zote na kuwatumikia wananchi kwa bidii na maarifa katika kuhakikisha kuwa wanapata huduma iliyo bora kutoka kwa serikali yao.

Amenifedhehesha na kunikwaza sana kama mwana CCM kindaki ndaki,Amenishangaza na kunisononesha Sana .Hapaswi kupewa nafasi ya kugombea tena uchaguzi ujao ,anapaswa kukatwa jina lake mapema sana .Hata kama pia anajuwa hatagombea uchaguzi ujao hakupaswa kuzungumza aliyoyazungumza kwa kuwa amekichafua chama na kuleta Taswira mbaya kwa chama. Ameonyesha kuwa hapaswi kuendelea kuaminiwa na chama ,hapaswi kushirikishwa mipango na mikakati mikubwa kwa kuwa ameonyesha kuwa na kifua kidogo na kukosa utulivu ,hekima na busara za kiuongozi,Ameonyesha kuwa chama kilikosea kumuamini na kumpa nafasi ya kupeperusha bendera ya chama ,anaonyesha kuwa chama kinapaswa kuwaomba msamaha wananchi wake kwa kuwapa mtu ambaye kumbe hana uelewa wa kufanya uchambuzi wa miswaada ilihali alikuwa anajuwa kuwa kazi ya Bunge na mbunge ni kutunga sheria,kuisimamia serikali n.k na wala hatoshi kuwa mbunge na kuwa Bungeni.

Anapaswa kukatwa jina lake kwa kuwa amejikata mwenyewe kabla ya kukatwa kwa kuwa ameonyesha hatoshi kuwa mbunge, hatoshi kuwa mwakilishi wa wananchi,hapaswi kushiriki wala kushirikishwa kwenye mipango na mikakati mikubwa ya aina yoyote ile , chama kina paswa kuwa naye chonjo sana ili asiendelee kukichafua chama na kuharibu Taswira njema ya chama chetu cha CCM. Kulikuwa na sababu gani ya kuongea aliyo yaongea hadharani? Alikuwa anamfaidisha nani? Alikuwa anatuma ujumbe gani kwa chama? Alikuwa anataka kuwaambia nini wapiga kura wake? Alikuwa anataka kupeleka ujumbe gani kwa jamii? Msimamo wake ni upi kwa sasa?

Kama mtu huna cha kuongea ni bora ukae kimya tu, hata kama umepewa nafasi ya kuongea ni bora uishie kusalimia tu na kukabidhi maiki.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa,kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Mtaanza kurukana wenyewe kwa wenyewe hadi pale unaa na ukweli utakapo jitenga dhahiri na kwa uwazi mkubwa🚶
 
Back
Top Bottom