Mbunge: Matamko ya Kisiasa yanaharibu Elimu. Mtu mwenye Madaraka anaamka tu na kutoa tamko bila kusikiliza Wataalam

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,279
Mbunge wa Viti Maalum, Tunza Malapo amesema elimu ya Tanzania inaathiriwa na matamko ya kisiasa.

Tunza ameyasema hayo jana Jumatano Mei 5, 2021 wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Amesema kubadilisha mtaala kufanyike kwa utulivu kwa kusikiliza wadau wa elimu wakiwemo wataalam wa elimu.

“Mara nyingi elimu yetu inaathiriwa na matamko ya kisiasa. Wakati mwingine mwenye madaraka akiamka asubuhi anatamka bila kufuata ushauri wa wataalam,” amesema.

Amesema kubadili mtaala sio suala la siku moja na kwamba wanatakiwa kufanya utafiti mfumo uliopo kama haufai na kama haufai kiongezwe nini katika mitaala hiyo. Tunza amesema pia maandalizi ya walimu yanatakiwa ili waweze kufundisha.

“Kinachofanyika sasa walimu wa ngazi ya cheti wanachofundishwa sio tunachotaka wanafunzi wafundishwe. Tuangalie tumetoka wapi tunaenda wapi? Tuache mihemko, tuwatumie wataalam tuepuke siasa,” amesema.

Chanzo: Mwananchi
 
Mara Kiswahili iwe lugha ya kufundishia. Na hakuna anayezungumzia vitabu tunavyotumia sasa vya Kiingereza ni nani atavibadilia (vina patent rights). Na wanaosema hivo hawana hata watoto wanaosoma shule za serikali!

Tunapewa mfano eti nchi nyingine zimeanzisha kiswahili kama somo kwa hiyo tukikuze. Kumbe hawajua maamuzi yetu ya kukiacha Kiingereza yanaleta pengo wanalotaka wachukulie advantage. Tunasahau kuwa nchi hizo hizo hazijafuta Kiingereza na lugha zao kama technical languages.

Ninatamani Kusini tungejifunza kwa kiingereza na kireno. Magharibi kiingereza na kifaransa! Tungekuwa na nafasi nyingi zaidi kwa nchi jirani!! Sasa tunawakaribisha wao kuvamia soko letu ambalo litatawaliwa na wawekezaji wa kigeni waliokuja na lugha zao za kitaalamu!! Bado kiswahili ni lugha muhimu SANA. Lakini haiifungui dunia kwa Watanzania!!

Na kuongea lugha ya mtu mwingine si utumwa! Tuache kuchezea elimu. Ni huko taifa la kesho litakuwa na upungufu wa taaluma/maarifa!
 
Hahaaaa! Naona jiwe amelengwa kimtindo. Eti tuanzishe somo la Historia kwa Kiswahili kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha sita.

Upunguani mkubwa huu.
Lifundishe historia ya jinsi mabeberu yamekuwa yakitulaghai na kutuibia mali zetu, somo hilo liambatane na nyimbo za kizalendo🤣
 
Kabla ya kusoma nilikubaliana nae lakini kwa angle tofauti kidogo,Kuhusu kusikiliza wataalamu ni muhimu lakini kuna uhitaji wa 'KIONGOZI' ,Kiongozi ataelekeza nini cha kufanya kisha 'Wataalamu' Watashauri Jinsi ya Kutekeleza.

Kuhusu Kiswahili,tunalia na ukosefu wa ajira Tukikitangaza vya kutosha Kiswahili tutafungua Milango mingi ya ajira,Lugha sio Utaalamu angalia Mainjinia wa kichina wanavyochapa Kazi
 
Kwenye uo utafiti naomba mnipendekeze nami niwepo kuangalia mapungufu ya elimu yetu na wapi tuboreshe , mda mwingine Kuna kupandikizana ujinga sana katika elimu yetu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unawezaje kushauri juu ya kauli ya rais? Mtu anasema nataka mkabidhi jengo hili kabla ya mwisho wa mwezi huu, mtu huyo huyo hajui cement au zege inatakiwa iachiwe kwa siku ngapi ikauke, yeye anachojua ni siku ya kukabidhiwa jengo!
Mkuu kazi ya wataalamu ni kutoa ushauri,ili anayefanya maamuzi (Kiongozi) afanye maamuzi sahihi.Na kuhusu kushauri ndiyo maana kuna washauri wake.
 
Lakini kwa nini kiinhereza kinafumdishwa toka primary mpaka advance lakini kinawasumbua mpaka PhD holders case study ni mwendazake JIWEPM
 
Unawezaje kushauri juu ya kauli ya rais? Mtu anasema nataka mkabidhi jengo hili kabla ya mwisho wa mwezi huu, mtu huyo huyo hajui cement au zege inatakiwa iachiwe kwa siku ngapi ikauke, yeye anachojua ni siku ya kukabidhiwa jengo!
Sahihi kwa bongo ni ngumu
 
Hahaaaa! Naona jiwe amelengwa kimtindo. Eti tuanzishe somo la Historia kwa Kiswahili kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha sita.

Upunguani mkubwa huu.
Watoto wa shule za msingi wanasoma Civic and Moral/Uraia, secondary wanasoma Civics, A level wanasoma GS, sijui hilo somo la historia linaloanzishwa watafundishwa nini

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu kazi ya wataalamu ni kutoa ushauri,ili anayefanya maamuzi (Kiongozi) afanye maamuzi sahihi.Na kuhusu kushauri ndiyo maana kuna washauri wake.
Sawa, mtaalamu anashauri muda gani, kabla au baada ya kauli ya mtawala?
 
Kabla ya kusoma nilikubaliana nae lakini kwa angle tofauti kidogo,Kuhusu kusikiliza wataalamu ni muhimu lakini kuna uhitaji wa 'KIONGOZI' ,Kiongozi ataelekeza nini cha kufanya kisha 'Wataalamu' Watashauri Jinsi ya Kutekeleza.

Kuhusu Kiswahili,tunalia na ukosefu wa ajira Tukikitangaza vya kutosha Kiswahili tutafungua Milango mingi ya ajira,Lugha sio Utaalamu angalia Mainjinia wa kichina wanavyochapa Kazi

Mkuu. Umetaja mchina na anavochapa kazi. Alifundishwa kazi hiyo kiswahili?? Unachothibitisha hapa ni kuwa alifundishwa kwa kichina lakini kwa sababu anajua kiswahili basi anaweza kufanya kazi hata hapa Tz. Je elimu yetu inatolewa kwa lugha gani? Kiingereza!!

Endelea kumwelewa kama mwanzo kwa sababu angle yako haina maana. Kwa hiyo unadhani ukipanua Kiswahili chako itakuja siku utakwenda Singapore kufanya kazi kama engineer?? Kwanini tunapaswa kukazia Kiingereza ni kwa sababu lugha ya Kiswahili haijafanikiwa kuwa lugha ya taaluma za sayansi. Imewahiwa na lugha nyingi. Oxford ilikuwa university mwaka 1167 - mwaka huo taifa letu hata halijawa na historia!! Waliotangulia walifanya ambayo hatuwezi kuyafanya tena kwa sababu yameshakuwa sehemu ya maisha yetu!! Kufahamu kiingereza kwa ufasaha kunafungua mianya mingi kuliko itakayofunguliwa kwa Kiswahili. Kiingereza ndio lugha inayoongewa na watu wengi kuliko yoyote! Na idadi inakua kila siku! Tujifunze lugha hii.
 
Mkuu. Umetaja mchina na anavochapa kazi. Alifundishwa kazi hiyo kiswahili?? Unachothibitisha hapa ni kuwa alifundishwa kwa kichina lakini kwa sababu anajua kiswahili basi anaweza kufanya kazi hata hapa Tz. Je elimu yetu inatolewa kwa lugha gani? Kiingereza!!

Endelea kumwelewa kama mwanzo kwa sababu angle yako haina maana. Kwa hiyo unadhani ukipanua Kiswahili chako itakuja siku utakwenda Singapore kufanya kazi kama engineer?? Kwanini tunapaswa kukazia Kiingereza ni kwa sababu lugha ya Kiswahili haijafanikiwa kuwa lugha ya taaluma za sayansi. Imewahiwa na lugha nyingi. Oxford ilikuwa university mwaka 1167 - mwaka huo taifa letu hata halijawa na historia!! Waliotangulia walifanya ambayo hatuwezi kuyafanya tena kwa sababu yameshakuwa sehemu ya maisha yetu!! Kufahamu kiingereza kwa ufasaha kunafungua mianya mingi kuliko itakayofunguliwa kwa Kiswahili. Kiingereza ndio lugha inayoongewa na watu wengi kuliko yoyote! Na idadi inakua kila siku! Tujifunze lugha hii.
Ninatumia nguvu kubwa lakini huonekani kuelewa,Kuna uhusiano gani wa lugha na maendeleo?

Kuhusu oxford,leo hii waingereza wamepitwa mbali sana na China kwenye uchumi,Ukitizama kwa undani utagundua kuwa sio suala la kuanza zamani ni Suala la kuboresha teknolojia na utafanikiwa zaidi ukitumia lugha unayoielewa kwa ufasaha.

Labda nikuulize unafikiri ni suala dogo kwa BBC,VOA,DW ,Na wengineo kuanzisha matangazo kwa lugha ya kiswahili? Jibu ni moja kuna jamii kubwa ya mataifa yanayozungumza kiswahili katika ukanda huu na 'kuwafikia' lazima utumie lugha wanayoielewa hivyo tunapaswa kuiona hii kama fursa.
 
Ninatumia nguvu kubwa lakini huonekani kuelewa,Kuna uhusiano gani wa lugha na maendeleo?

Kuhusu oxford,leo hii waingereza wamepitwa mbali sana na China kwenye uchumi,Ukitizama kwa undani utagundua kuwa sio suala la kuanza zamani ni Suala la kuboresha teknolojia na utafanikiwa zaidi ukitumia lugha unayoielewa kwa ufasaha.

Labda nikuulize unafikiri ni suala dogo kwa BBC,VOA,DW ,Na wengineo kuanzisha matangazo kwa lugha ya kiswahili? Jibu ni moja kuna jamii kubwa ya mataifa yanayozungumza kiswahili katika ukanda huu na 'kuwafikia' lazima utumie lugha wanayoielewa hivyo tunapaswa kuiona hii kama fursa.
Mmmh! Sizani Kama umeshafanya kazi na watu waliotoka nje ya nchi au umetoka hata nchi jirani zetu, mawasiliano ya kiingereza ni muhimu sana ndugu yangu, hicho kiswahili tutumie tu kama lugha ya kuwasiliana hapa ndani kwa waswahili wenzetu ila ikija kwenye kufanikiwa na kushirikiana na dunia Kama hujui lugha ya kiingereza utashindwa kwenye ushindani mwingi, huwezi kuomba kazi UN hata ya udereva hujui kiingereza, nenda wageni wanaokuja Kama mabalozi hata house keeping anajua kiingereza sasa unataka tuwe duni kuchangamana na dunia nikimaanisha kwenye fursa.
 
Alafu cha ajabu hizo nchi zinazosema tutumie lugha ya kiswahili wao wanawahamashisha watoto wao kutumia kiingereza na kiswahili inakuwa kwa wanasiasa wachache ambao wanatumia kubebea sifa na kupumbaza Tanzania watoto wao wasipate maarifa ya lugha ya kiingereza Ili nchi zao ziwe juu ziteke fursa zote, imagine tunataka kuuza bidhaa nje na hatuna jina kubwa Kama nchi zingine uandike kiswahili chako Nani atanunua?
 
Watanzania wanaidharau Sana somo la Historia!!
Mimi binafsi naliheshimu Sana na Kama ningepewa nafasi ya kufanya maamuzi katika sekta ya Elimu basi KISWAHILI kingekuwa lugha ya kufundishia kuanzia awali mpaka vyuo,kingereza kingekuwa somo tu!pia somo la HISTORIA kingekuwa la lazima kwa kila ngazi ya Elimu!!
Utajuaje ulipo na unakoenda Kama hujui ulikotoka??!!!!
How would you know what is if you don't know what was???!!!!
Kwenye hili MWENDAZAKE NAMUUNGA MKONO BILA HAYA🙄🙄
 
Back
Top Bottom