Mbunge Joseph Haule 'Prof. Jay' msemaji rasmi wa Kilosa

Mbunge Joseph Haule 'Prof. Jay' msemaji rasmi wa Kilosa

Bagamoyo

Platinum Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
31,927
Reaction score
36,721
29 Juni 2020,

Mbunge wa CHADEMA mkoani Morogoro leo ameonesha sababu ya wananchi wa Morogoro siyo tu jimboni kwake Mikumi kumkubali kwa kusema wazi bila woga changamoto zinazoikabili mkoa wa Morogoro.

Pia wananchi wameonesha kumkubali bila kujali vyama ikiwa mbunge anatetea maslahi ya ustawi wa wananchi kijamii, kiuchumi, kiafya na kielimu.

 
Maelezo yake yanaakisi kapevuka,tofauti na wakora wengine wa chadomo
 
Kilosa ilipoa sana, Wananchi walikaa kimya kusikiliza hotuba za tambo na sifa toka CCM kuwa watatatua migogoro ya ardhi na kujengewa barabara za lami

Cha kushangaza na kusikitisha baada ya kukamilika tambo na sifa akakaribishwa mbunge wa Mikumi wa chadema Prof J atoe salamu

Prof J aliongea point bila kusifu na kuanisha matatizo ya jimbo la kilosa,Wananchi wakaanza kushangilia na kuamua kusimama kupiga makofi

Hili jambo linaumiza sana wana ccm, kwanini wananchi walishangilia sana hotuba ya Prof J kilosa na jimbo sio lake

Hii ni picha mbaya sana, Wananchi hamuoni maendeleo yaliofanywa na CCM au ni kiburi tu

Hao chadema wanewapa kitu gani ?Hawajafanya siasa miaka mitano bado mnawashangilia kuliko CCM

Kilosa nani amewaroga?

Kwa style hii nashauri vyama vya upinzani vifutwe tuwe na chama kimoja,Kilosa mmetuabisha ccm,Kilosa mmejenga picha mbaya kwenye ule mkutano

Prof J sio mbunge wa kilosa na ni mtu ambae hajui matatizo ya kilosa,Kwanini mnapiga makofi na kusimama kushangilia

Kilosa hamuoni Mahandaki ya reli ya kisasa SGR

Kilosa mmetuabisha kwa hali kama hii uchaguzi mwaka huu upigwe marufuku

Kilosa ni kijijini na porini kumejaa wajinga lakini bado mnashangilia watu waliofichwa miaka mitano wasiongee na wananchi,Imetuumiza sana hatujalala tunawaza kilichotokea kilosa
 
We piga makofi,bungeni anaenda wa ccm
Ccm oyeee oyeee zaidi

Tutashinda kwa mbinu majimbo ya upinzani

Mwaka huu tutatumia kitu kinaitwa"SHIKWAMBI" maana yake shinda kwa mbinu iwe jua au mvua


Sisi ni wazee wa shikwambi tutashinda tu


Tuna mbinu nyingi mwaka huu tunawapiga Shikwambi habaki mtu bungeni labda Zito na Mbatia
 
Ccm oyeee oyeee zaidi

Tutashinda kwa mbinu majimbo ya upinzani

Mwaka huu tutatumia kitu kinaitwa"SHIKWAMBI" maana yake shinda kwa mbinu iwe jua au mvua


Sisi ni wazee wa shikwambi tutashinda tu


Tuna mbinu nyingi mwaka huu tunawapiga Shikwambi habaki mtu bungeni labda Zito na Mbatia
Zitto akauze mawese, ubunge atausikia kwenye bomba
 
Maendeleo Hayana Chama
Kushangiliwa Ndiyo Nini, Ccm Ina Fitna Sana 🙄😏😏
 
Kwanini aliitwa Prof J na sio mbunge wa Kilosa?
 
Wakibaki fisiemu peke yao bungeni sitoona ajabu wale wanaosifiwa "UPUMBAF..." wakiongezeka na ndipo anguko kuu litakapofuatia na hakuna atakayesalia bali ndipo hapo utawala ule utakuwa umekoma na majigambo ya "kudumu" yatakuwa yamefika tamati.
 
Maendeleo Hayana Chama
Kushangiliwa Ndiyo Nini, Ccm Ina Fitna Sana [emoji849][emoji57][emoji57]
Serikali za mitaa tuliwapiga kitu inaitwa "KATA" Kwa ufupi ni katisha tamaa upinzani na wananchi na ilifanya kazi vizuri maeneo mengi walisusa tukashinda

Uchaguzi huu tunatumia"SHIKWAMBI"maana yake shinda kwa mbinu iwe safi au chafu

Shikwambi ndio inaenda kuwamaliza upinzani

Tutashinda kwa mbinu

Mwaka huu ni raha tupu ccm

SHIKWAMBI inawamaliza iwe jua au mvua
 
Prof Jay ni mwanahiphop halisi, watu wa aina yake kuzuga hawawezi.
Wao ni black and white.

Magufuli anapiga kazi haswaaa, sema kuna baadhi ya maeneo watendaji wa serikali ndio wanazingua, uzuri akiwabaini harembi anawafumua tu.

Hii nchi tukipata kiongozi mwingine akaja na pozi za kuchekacheka, tutarudi miaka 60 nyuma. Kila kiongozi ajae, mwendo ni huu huu.
 
Prof Jay ni mwanahiphop halisi, watu wa aina yake kuzuga hawawezi.
Wao ni black and white.

Magufuli anapiga kazi haswaaa, sema kuna baadhi ya maeneo watendaji wa serikali ndio wanazingua, uzuri akiwabaini harembi anawafumua tu.

Hii nchi tukipata kiongozi mwingine akaja na pozi za kuchekacheka, tutarudi miaka 60 nyuma. Kila kiongozi ajae, mwendo ni huu huu.
Safi sana wewe ni Mzalendo

Sasa mnatambua kazi ya awamu ya tano .

Tumejenga Flyover
.Tumeongeza ajira za madaktari na sekta nyingi
Watanzania mna maisha mazuri sasa
 
Back
Top Bottom