Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
Mbunge Cherehani: Tusiache Kumuombea Rais Samia
Mbunge wa jimbo la Ushetu Mhe. Emmanuel Cherehani amewahimiza waumini wa dini zote kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt .Samia Suluhu Hassa ili kumpa nguvu zaidi katika kuwatumikia watanzania
Wito huo umetolewa katika misa takatifu ya mkesha wa sikukuu ya Krismas iliyofanyika katika kanisa la mtakatifu Yohane Parokia ya Mpunze ambapo amesema ,Rais anafanya kazi kubwa kwa wananchi hivyo ni vyema kumuombea
“Ndugu zangu nawaomba tuendelee kumuombea Rais wetu anafanya kazi kubwa ya kuijenha nchi yeti,tazamq fedha nyingi anazotoa kwenye Afya,Maji,Elimu na Barabara na Fedha nyingi kwaajili ya kukamilisha miradi ya maendeleo.” - Mhe Cherehani