kisugujira
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 774
- 200
Kutokuwa na busara na hekima kwa viongozi wetu kutaendelea kuleta matatizo na kutoelewana miongoni mwetu katika nchi yetu iliyokuwa na amani Tanzania.
Leo hii katika mjadala wa bajeti ya wizara ya uchukuzi 2013-2014, mbunge wa Ilala Azan Zungu, amesababisha kutokea kwa kelele bungeni zilizotokana na minong'ono toka kwa baadhi ya waheshimiwa wabunge hasa toka vyama vya upinzani, baada ya kutangaza na kuwatambulisha vijana wawili, Mwampamba na Juliana Shoza waliohama toka CHADEMA na kujiunga na CCM!
Bila ya kutokuwa na haya, mbunge huyo amediriki pia kuwataka wanafunzi wa shule ya msingi Ilala wakue haraka ili waje kumpigia kura siku zijazo! Ameshindwa kuwaasa wanafunzi hao waliokwenda bungeni kujifunza, kuwa wasome sana ili kesho waje kuwa viongozi bora na waadilifu katika nchi! Badala yake anawafundisha kuwa na tamaa ya kukaa madarakani kwa muda mrefu!
"Leave your mark where others can only dream on going."
Leo hii katika mjadala wa bajeti ya wizara ya uchukuzi 2013-2014, mbunge wa Ilala Azan Zungu, amesababisha kutokea kwa kelele bungeni zilizotokana na minong'ono toka kwa baadhi ya waheshimiwa wabunge hasa toka vyama vya upinzani, baada ya kutangaza na kuwatambulisha vijana wawili, Mwampamba na Juliana Shoza waliohama toka CHADEMA na kujiunga na CCM!
Bila ya kutokuwa na haya, mbunge huyo amediriki pia kuwataka wanafunzi wa shule ya msingi Ilala wakue haraka ili waje kumpigia kura siku zijazo! Ameshindwa kuwaasa wanafunzi hao waliokwenda bungeni kujifunza, kuwa wasome sana ili kesho waje kuwa viongozi bora na waadilifu katika nchi! Badala yake anawafundisha kuwa na tamaa ya kukaa madarakani kwa muda mrefu!
"Leave your mark where others can only dream on going."