MBUNGE wa Jimbo la Buchosa, Samwel Chitalilo ameingia katika mkasa mpya baada ya kudaiwa kumshambulia Mabula Matulanya, ambaye ni mlinzi wa ghati la ofisi ya kivuko cha Nyakaliro Kome, linalomilikiwa na serikali.
Mlinzi huyo anadai alishushiwa kipigo hicho na mbunge huyo kwa kushirikiana na washirika wake wawili mara baada ya kummulika tochi Chitalilo wakati akiwa kwenye haja ndogo karibu na mlango wa ofisi ya kivuko hicho, ambalo ni eneo la lindo lake.
"Nilimulika nikidhani pengine anaweza kuwa mwizi katika lindo lango... sikujua kama ni mbunge na wala sikuwa natambua kama alikuwa katika baa ya jirani akinywa pombe.
Naye Mbunge Chitalilo, alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu mkasa huo, alikiri kuwepo kwa shambulio hilo na kusema kuwa mlinzi huyo alishambuliwa na wananchi waliokuwa jirani kutokana na yeye kulalamika kudhalilishwa kwa kumulikwa wakati akiwa anakojoa.
"Sikiliza suala hili, mimi nilishalisamehe, polisi kwa kuwaomba wamfutie mashtaka mlinzi huyo kwa vile watu wengi waliniomba samahani... alinidhalilisha kwa kunimulika makusudi licha ya kujua nilikuwa mimi... alishambuliwa na watu ambao nilifanya kazi ya kuwatuliza, sasa mimi kosa langu ni kumsamehe?" alihoji.
source; http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=8433
Du mbunge anakojoa chocho!!!!!!!!!!!!!!!!
Mbunge ashtakiwe kosa kujisaidia hovyo porini- ni kinyume cha sheria!
Mzalendo vipi kama hapo zamani za kale kuna ka grocery ambako hakana choo lakini kalipewa leseni ya kuendesha shughuli zake hapo kwenye eneo la tukio? na hapo jirani hakuna choo hata cha serekali? Mheshimiwa akajisaidie wapi? angekuwa si mbunge watu wangetaka ashtakiwe? Kama kujisaidia porini ni uvunjaji wa sheria na tunataka suala hili lichukuliwe seriously basi tutaomba nafasi kwenye magereza ya nchi jirani! Think about idadi ya mabasi yanayosimama njiani 'kuchimba dawa' utajua naongea nini........Tumvalie njuga kwa issue ya kumpiga mlinzi lakini sio hili la kukojoa, tena alikuwa keshakula bia!
Acha hizo ndugu yangu, yaani wewe unaona ni jambo la kawaida kwa Mbunge kukojoa njiani? Yaani yeye kama Mbunge kama alijua kwamba hiyo sehemu haina choo kwa nini isifungwe? unajua watu tunapenda kutoa sababu hata kama ni za kipumbavu ili kuhalalisha upumbavu wetu. Huyo Mbunge ambaye inabidi awe mfano kwa wananchi yaani ndio hayo anayofanyaa? maana hata watoto wadogo wanaweza wakaanza kukojoa njiani kwa sababu wanaona ni kitu cha kawaida kwa sababu hata Mbunge anakojoa tuu popote. Bongo inabidi kuwe na elimu ya usafi sasa, hii ni kitu ambacho watu wanaweza wakashiriki.Mzalendo vipi kama hapo zamani za kale kuna ka grocery ambako hakana choo lakini kalipewa leseni ya kuendesha shughuli zake hapo kwenye eneo la tukio? na hapo jirani hakuna choo hata cha serekali? Mheshimiwa akajisaidie wapi? angekuwa si mbunge watu wangetaka ashtakiwe? Kama kujisaidia porini ni uvunjaji wa sheria na tunataka suala hili lichukuliwe seriously basi tutaomba nafasi kwenye magereza ya nchi jirani! Think about idadi ya mabasi yanayosimama njiani 'kuchimba dawa' utajua naongea nini........Tumvalie njuga kwa issue ya kumpiga mlinzi lakini sio hili la kukojoa, tena alikuwa keshakula bia!
....Tumvalie njuga kwa issue ya kumpiga mlinzi lakini sio hili la kukojoa, tena alikuwa keshakula bia!
"Sikiliza suala hili, mimi nilishalisamehe, polisi kwa kuwaomba wamfutie mashtaka mlinzi huyo kwa vile watu wengi waliniomba samahani... alinidhalilisha kwa kunimulika makusudi licha ya kujua nilikuwa mimi... alishambuliwa na watu ambao nilifanya kazi ya kuwatuliza, sasa mimi kosa langu ni kumsamehe?" alihoji.
"hapana Mheshimiwa Mbunge,
Kosa lako ni kukojoa hadharani, ofisini kwa watu, na GBH kwa huyo mlinzi aliyekuwa lindoni. Ungetwangwa risasi, au kuambiwa unawanga?"
Tena eti Mheshimiwa....Ndio tatizo watu wengine walishajizoelea maisha ya kihuni basi hata wakiwa na nyadhifa wanajisahau...Huyo mlinzi angemtandika hata rungu sawa tu...Mbunge unaharibu mazingira kwa kukojoa hadharani???Wabunge wengine bwana!!! Naye huyu anastahili kweli kuitwa mbunge wetu?
...; SASA INABIDI YEYE AADABISHWE KWA MUJIBU WA SHERIA ILI AWE FUNDISHO KWA WENGINE WENYE TABIA KAMA YAKE.