Mbunge amdunda mlinzi

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,839
MBUNGE wa Jimbo la Buchosa, Samwel Chitalilo ameingia katika mkasa mpya baada ya kudaiwa kumshambulia Mabula Matulanya, ambaye ni mlinzi wa ghati la ofisi ya kivuko cha Nyakaliro Kome, linalomilikiwa na serikali.

Mlinzi huyo anadai alishushiwa kipigo hicho na mbunge huyo kwa kushirikiana na washirika wake wawili mara baada ya kummulika tochi Chitalilo wakati akiwa kwenye haja ndogo karibu na mlango wa ofisi ya kivuko hicho, ambalo ni eneo la lindo lake.

"Nilimulika nikidhani pengine anaweza kuwa mwizi katika lindo lango... sikujua kama ni mbunge na wala sikuwa natambua kama alikuwa katika baa ya jirani akinywa pombe.

Naye Mbunge Chitalilo, alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu mkasa huo, alikiri kuwepo kwa shambulio hilo na kusema kuwa mlinzi huyo alishambuliwa na wananchi waliokuwa jirani kutokana na yeye kulalamika kudhalilishwa kwa kumulikwa wakati akiwa anakojoa.

"Sikiliza suala hili, mimi nilishalisamehe, polisi kwa kuwaomba wamfutie mashtaka mlinzi huyo kwa vile watu wengi waliniomba samahani... alinidhalilisha kwa kunimulika makusudi licha ya kujua nilikuwa mimi... alishambuliwa na watu ambao nilifanya kazi ya kuwatuliza, sasa mimi kosa langu ni kumsamehe?" alihoji.

source; http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=8433



"hapana Mheshimiwa Mbunge,

Kosa lako ni kukojoa hadharani, ofisini kwa watu, na GBH kwa huyo mlinzi aliyekuwa lindoni. Ungetwangwa risasi, au kuambiwa unakwanga?"

 
Du mbunge anakojoa chocho!!!!!!!!!!!!!!!!

...huyu mheshimiwa sana ndiye yule polisi waliothibitisha kawalaghai wapiga kura wake kiwango chake cha Elimu.

...na ndiye huyu huyu aliyemtetea mheshimiwa sana, Andrew Chenge na sakata lake la 'vijisenti' kuwa hajamuibia mtu!

Taswira jamani, taswira...
 
Wabunge wengine bwana!!! Naye huyu anastahili kweli kuitwa mbunge wetu?
 
Mbunge ashtakiwe kosa kujisaidia hovyo porini- ni kinyume cha sheria!

Mzalendo vipi kama hapo zamani za kale kuna ka grocery ambako hakana choo lakini kalipewa leseni ya kuendesha shughuli zake hapo kwenye eneo la tukio? na hapo jirani hakuna choo hata cha serekali? Mheshimiwa akajisaidie wapi? angekuwa si mbunge watu wangetaka ashtakiwe? Kama kujisaidia porini ni uvunjaji wa sheria na tunataka suala hili lichukuliwe seriously basi tutaomba nafasi kwenye magereza ya nchi jirani! Think about idadi ya mabasi yanayosimama njiani 'kuchimba dawa' utajua naongea nini........Tumvalie njuga kwa issue ya kumpiga mlinzi lakini sio hili la kukojoa, tena alikuwa keshakula bia!
 
Mzalendo vipi kama hapo zamani za kale kuna ka grocery ambako hakana choo lakini kalipewa leseni ya kuendesha shughuli zake hapo kwenye eneo la tukio? na hapo jirani hakuna choo hata cha serekali? Mheshimiwa akajisaidie wapi? angekuwa si mbunge watu wangetaka ashtakiwe? Kama kujisaidia porini ni uvunjaji wa sheria na tunataka suala hili lichukuliwe seriously basi tutaomba nafasi kwenye magereza ya nchi jirani! Think about idadi ya mabasi yanayosimama njiani 'kuchimba dawa' utajua naongea nini........Tumvalie njuga kwa issue ya kumpiga mlinzi lakini sio hili la kukojoa, tena alikuwa keshakula bia!

Kana-Ka-Nsungu,
Kwani sheria ni wapi inasema kama jirani hakuna choo basi ndugu yangu tujisaidie tu popote?
Huyu jamaa alikuwepo Mwanza mjini.. sheria ndogo2 za miji ndo zitumike kumshtaki!
 
Mzalendo vipi kama hapo zamani za kale kuna ka grocery ambako hakana choo lakini kalipewa leseni ya kuendesha shughuli zake hapo kwenye eneo la tukio? na hapo jirani hakuna choo hata cha serekali? Mheshimiwa akajisaidie wapi? angekuwa si mbunge watu wangetaka ashtakiwe? Kama kujisaidia porini ni uvunjaji wa sheria na tunataka suala hili lichukuliwe seriously basi tutaomba nafasi kwenye magereza ya nchi jirani! Think about idadi ya mabasi yanayosimama njiani 'kuchimba dawa' utajua naongea nini........Tumvalie njuga kwa issue ya kumpiga mlinzi lakini sio hili la kukojoa, tena alikuwa keshakula bia!
Acha hizo ndugu yangu, yaani wewe unaona ni jambo la kawaida kwa Mbunge kukojoa njiani? Yaani yeye kama Mbunge kama alijua kwamba hiyo sehemu haina choo kwa nini isifungwe? unajua watu tunapenda kutoa sababu hata kama ni za kipumbavu ili kuhalalisha upumbavu wetu. Huyo Mbunge ambaye inabidi awe mfano kwa wananchi yaani ndio hayo anayofanyaa? maana hata watoto wadogo wanaweza wakaanza kukojoa njiani kwa sababu wanaona ni kitu cha kawaida kwa sababu hata Mbunge anakojoa tuu popote. Bongo inabidi kuwe na elimu ya usafi sasa, hii ni kitu ambacho watu wanaweza wakashiriki.
 
....Tumvalie njuga kwa issue ya kumpiga mlinzi lakini sio hili la kukojoa, tena alikuwa keshakula bia!

...ha ha, Under Influence ya 'dawa ya shingo' sio? haya bana...

lakini mimi inanisumbua huyo mheshimiwa sana alipofanya mambo matatu;

1.kukojoa karibu na mlango wa ofisi,
2.hata baada ya kupigwa tochi, hakuomba msamaha,
3.yeye alitoa kibano na kuamuru mlinzi awekwe ndani.

huyu na vibweka vyake anaingia kundi la VIP, Very Ignorant Person, without morals.
 
Mbunge ashtakiwe kwa kuchafua mazingira. Hakuna sheria yeyote inayomlinda. Kama hiyo sehemu aliyokuwa anakunywa bia haina choo itajulikana mbele ya sheria. Mmiliki wa hiyo grocery ikibainika anauza vinywaji bila kuwa na choo naye asweke ndani. Lakini huwezi kuhalalisha kosa la mbunge kwa kosa la mwenye grocery. Hayo no makosa 2 tofauti. Watz umefika wakati tubadilike, dunia inaenda mbele. Mbunge alipaswa kutoa mfano mwema.
 
"Sikiliza suala hili, mimi nilishalisamehe, polisi kwa kuwaomba wamfutie mashtaka mlinzi huyo kwa vile watu wengi waliniomba samahani... alinidhalilisha kwa kunimulika makusudi licha ya kujua nilikuwa mimi... alishambuliwa na watu ambao nilifanya kazi ya kuwatuliza, sasa mimi kosa langu ni kumsamehe?" alihoji.

This guy is hilarious, he is so ignorant he actually seem to believe he was wronged and is now issuing a pardon.
 
Beer za chocho bwana..ana makosa mbunge..kabisa angenda mbali kidogo..sio kwenye lindo la mtu.
 
Kosa la kwanza la Mbunge ni kukojoa ofisini kwa mtu( eneo la lindo)

Kosa la pili la mbunge ni kujisaidia hadharani.


Kosa la tatu la mbunge ni kuchimba mzizi mahali pasipo stahili, mahali panapo stahili ni chooni.

Kosa la nne la mbunge ni kumgeuzia kibao mlinzi na kumbambika kesi kwa kutumia cheo, umaarufu na mazoea mabaya ya kujisahau kwamba kukojoa ovyo ni haki yake kama mbunge(hasa akipata kinywaji).

Kosa la tano ni kuwadharirisha wabunge wenzie na watu waliomchagua, kwa kudhani kwamba ujinga wake ni ujiko na ni jambo lenye staha mbele ya wabunge wenzie na taifa kwa ujumla.

Kosa la sita ni kuvunja sheria na taratibu za usafi wa mazingira, afya na tabia njema huku akiwa na fahamu zake zote hasa ukizingatia kwamba mbunge ni mtunga sheria kwa niaba ya wananchi waliomchagua na taifa kwa ujumla.

Kosa la saba ni dharau majivuno ubabe na kukosa adabu,litokanalo na kula ovyo kunywa ovyo na kujisaidia ovyo.

Kama katika karne hii ya 21 Mbunge bado anakojoa ovyo ovyo na kuanzisha songombingo pale adhanipo kuna mtu alimdharirisha akiwa katikati ya tendo lake chafu la kukojoa mahali pasipo na choo. Je itatuchukua karne ngapi kujenga jamii inayo jali usafi wa mazingira na umuhimu wa kutumia choo hata ikibidi ubane mkojo wako kwa saa nzima??

Ovyooo!!

Mbunge anatakiwa kumwomba radhi mlinzi.
Polisi wanatakiwa kumchukulia hatua mbunge kwa kutenda kosa la jinai la kuchafua mazingira kwa makusudi.
 
Wabunge wengine bwana!!! Naye huyu anastahili kweli kuitwa mbunge wetu?
Tena eti Mheshimiwa....Ndio tatizo watu wengine walishajizoelea maisha ya kihuni basi hata wakiwa na nyadhifa wanajisahau...Huyo mlinzi angemtandika hata rungu sawa tu...Mbunge unaharibu mazingira kwa kukojoa hadharani???

Hivi ile habari ya kufoji vyeti iliishia wapi???
 
Jamani wabunge kwani si ni wao wantakiwa wawe mfano kwa jamii. Fikiria anapita mtoto anyemfahamu mheshimiwa huyu, anakuta jongoo lake linatema maji kama bomba atacopy nini huyu? Hata nyumbani kwake basi utakuta mikojo kila mahali. Ashtakiwe kwa makosa ya kukojoa hadharani na kuchafua mazingira.
 
Sio sababu kuwa hakuna choo ndio achafue mazingira. Je angekuwa amebanwa na haja kubwa angejisaidia hapo ofisini kwa watu kwavile hakuna choo cha serikali? Huyu ni kiongozi ANAYETAKIWA KUWA MFANO KWA WATU ANAOWAONGOZA; SASA INABIDI YEYE AADABISHWE KWA MUJIBU WA SHERIA ILI AWE FUNDISHO KWA WENGINE WENYE TABIA KAMA YAKE.
 
...; SASA INABIDI YEYE AADABISHWE KWA MUJIBU WA SHERIA ILI AWE FUNDISHO KWA WENGINE WENYE TABIA KAMA YAKE.

...safi sana, kwa kuanzia angestahili kupiga deki eneo hilo, kisha apande maua, na ahakikishe yanamwagiliwa kila siku kwa muda wa siku thelathini, hata watoto wakipita hapo liwe fundisho, "HAPA NDIPO ALIPOKOJOA/JISAIDIA MH MBUNGE."

community service hiyo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom