Mbowe: Yanayotokea ni hofu ya watawala kushindwa kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe amesema kibano wanachokipata wapinzani kutoka Serikalini kinatokana na hofu waliyonayo viongozi wa chama tawala cha CCM.

Amesema hofu hiyo inatokana na CCM kuhofia kushindwa kwenye uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020 kwa Chadema kuibuka mshindi na kuongoza dola.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alitoa kauli hiyo Jumamosi Mei 4 wakati anazindua tawi maarufu la Chadema la Urusi lililopo Mwanga mjini Kigoma.

Alisema viongozi na wanachama wa CCM wana hofu ya kushindwa katika uchaguzi mkuu ujao, hivyo kuamua kuzuia mikutano ya hadhara na kuhakikisha viongozi wa vyama vya upinzani wanafunguliwa kesi mahakamani kila uchao.

"CCM wapo hoi, wamelegea wameishiwa mbinu za kisiasa ndio maana vyama vya upinzani vinapata kibano kwa viongozi wake kukamatwa, kupigwa na hata kuumizwa," alisema Mbowe.
 
Vita ya uwenyekiti Chadema huja na visa vingi..kama vile kulishana sumu na kutekana
 
Mbowe bana msaidizi wake wa ofisini Ben Saanane amepotea yuko kimya hana habari huyo Mdude ndio ahangaike nae? Mbowe ni mtumishi mtiifu wa TISS
 
Mbowe bana msaidizi wake wa ofisini Ben Saanane amepotea yuko kimya hana habari huyo Mdude ndio ahangaike nae? Mbowe ni mtumishi mtiifu wa TISS
Mbowe anatia huruma sana, yaani bado anaota Chadema kushika dola ! Lisu alisema "tukishindwa kushika dola 2015 hatuji kushinda kamwe" naona mbowe hakumwelewa
 
haijawahi kutokea ccm ikawa na hofu ya kushinda uchaguzi hizo ndi ndoto za mbowe na genge lake la kihuni
 
Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe amesema kibano wanachokipata wapinzani kutoka Serikalini kinatokana na hofu waliyonayo viongozi wa chama tawala cha CCM.

Amesema hofu hiyo inatokana na CCM kuhofia kushindwa kwenye uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020 kwa Chadema kuibuka mshindi na kuongoza dola.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alitoa kauli hiyo Jumamosi Mei 4 wakati anazindua tawi maarufu la Chadema la Urusi lililopo Mwanga mjini Kigoma.

Alisema viongozi na wanachama wa CCM wana hofu ya kushindwa katika uchaguzi mkuu ujao, hivyo kuamua kuzuia mikutano ya hadhara na kuhakikisha viongozi wa vyama vya upinzani wanafunguliwa kesi mahakamani kila uchao.

"CCM wapo hoi, wamelegea wameishiwa mbinu za kisiasa ndio maana vyama vya upinzani vinapata kibano kwa viongozi wake kukamatwa, kupigwa na hata kuumizwa," alisema Mbowe.

Kama Mheshimiwa Mbowe ana Hoja zingine alizoziacha nitamuelewa ila kwa hii / hizi nitakuwa wa mwisho Kumuelewa na bado hazijanishawishi.
 
Kama Mheshimiwa Mbowe ana Hoja zingine alizoziacha nitamuelewa ila kwa hii / hizi nitakuwa wa mwisho Kumuelewa na bado hazijanishawishi.
Kama TISS, NEC, returing officers, RCs, DCs, Jeshi la polisi, wote ni wako kinachokufanya uzuie mikutano na uwafunge wapinzani ni kitu gani kama siyo hofu.
 
Kama TISS, NEC, returing officers, RCs, DCs, Jeshi la polisi, wote ni wako kinachokufanya uzuie mikutano na uwafunge wapinzani ni kitu gani kama siyo hofu.

Mimi siyo Msemaji wa Jeshi la Polisi, TISS, NEC, RC's na DC's tafadhali na badala yake nenda ukawaulize hao Wahusika watakujibu ila hapa Mimi nachangia kama tu Mchangiaji Huru wa huu Mtandao wa JamiiForums sawa?
 
Back
Top Bottom