Mbowe: Tutashika dola kirahisi 2015

Mbowe: Tutashika dola kirahisi 2015

Na George Ramadhan|21st February 2013


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema sera mpya ya majimbo itakiwezesha chama hicho kushika dola na kuongoza nchi kwa urahisi zaidi.

Akifungua kikao cha kazi za Chadema kilichofanyika jijini hapa jana, Mbowe alisema sera ya majimbo ni mkakati uliobuniwa na chama hicho kwa lengo la kusogeza madaraka kwa wananchi ili kushiriki kufanya maamuzi ya jinsi ya kuongoza nchi.

Alisema utamaduni, ambao umezoeleka hapa nchini na ambao unatumiwa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni kuongoza nchi kutokea Dar es Salaam. Mbowe alisema hatua hiyo imeonyesha kushindwa kuboresha hali ya maisha ya Watanzania wengi.
“Kwa zaidi ya miaka 20 sasa Tanzania tumekuwa na utamaduni wa kutawala nchi kutokea Dar es Salaam. Chadema tumeliona hili na tumegundua kasoro zake. Ndiyo maana tumeamua kuja na sera ya majimbo ili kusogeza madaraka kwa wananchi,” alisema.

Alisema kwa kutumia mfumo huo, CCM imeonyesha kushindwa kushughulikia matatizo ya msingi ya wananchi, ikiwamo mgawanyo sahihi wa rasilimali za taifa. “Pamoja na kusogeza madaraka kwa wananchi, sera ya majimbo inalenga kutaka kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali zao tofauti na sasa. Maeneo yenye raslimali nyingi kama madini, ndiyo yenye kiwango kikubwa cha umaskini,” alisema.

Alisema pia kwa kufuata mfumo huo, ndiyo sababu serikali ya CCM imekuwa ikijipanga kuwadhibiti viongozi wa Chadema kila wanapojipanga kwenda kufanya shughuli za kisiasa maeneo mbalimbali nchini.

Alisema kwa kufuata sera ya majimbo, serikali ya CCM haiwezi tena kuwadhibiti viongozi wa Chadema isipokuwa watashtukia chama hicho kimeshika dola na kuongoza nchi.



CHANZO: NIPASHE





Tafadhali Mbowe na wenzako. Ninawaomba mkishika hii nchi kunako 2015, chonde anzisheni tume ya kuchunguza viongozi wote wa CCM waliokuwa madarakani katika utawala wa Mkapa na Kikwete. Wakibainika kumiliki pesa za umma/serikali wataifishwe na kunyongwa mara moja. Ua inzi.
 
Kwanini watu ambao tayari wana nyadhifa ndani ya chama wanapewa nafasi nyingine za kuongoza kwenye kanda?

Mie nadhani umejibiwa vizuri CDM cant be any more careful than it is, coz fitina za ccm sio siri - hawana nia ya dhati ya kudumisha demokrasia ni presha za magharibi tu zinatukeep afloat. kuna watu ktk ccm vingunge, hawaamini ccm will ever lose power wako tayari kufanya lolote liwezekanalo kifupi hawaamini demokrasia ipo. sasa hapo tunapoona yaliyotokea kwa kina shonza na wengine kama kuna ukurupukaji ktk kuentrust watu (na hapa mie nasema hata shibuda viongozi walikurupuka wasinge mwamini sio kikanda wala na jimbo). Kama kuna jambo linaloweza angusha chadema kwa wepesi kama nyumba ya karata - ni fitina. About the party, it is doing fine for now whatever it is they do its redefining tz forever tuangalie na hilo. Whats got into us watanzania? We are all in the blame game! it is refreshing kuona vijana coming from nothing are trained up and given the platform like nowhere else, like never before. Malalamiko mengi ni kwamba kila mtu alidhani atakuwa fulani chadema haiko hivyo hata marekani we have to learn to be supporters and let party business be party business, watanzania wengi tuna shida hiyo on the other hand of the coin tunapenda usultani, sijui kwasababu mwarabu aliwahi huku. Nakumbuka kafulila alikimbilia nccr only to suffer the same fate, he was just too ambitious-and thats our problem mnataka kushindana na ccm ambao tayari wamestaarabika enough to call authority what it is, alafu nyie wenyewe mpo devided. Like bob marley used to sing in Zimbabwe <i> 'africa, lets unite and fight this little struggle first'.</i> fuatilia midahalo kila mtu anadhani anakijua cdm kuliko Slaa mwenyewe. Mie huwa najiuliza hivi dr akiangalia si huwa anacheka sana.
 
Wewe unachofanya humu mtandaoni ni kitu gani tofauti na hao unaowasema wanalalamika na kupiga majungu?Practice what you preach.
Mimi sijalilia madaraka huko chadema. Wewe unayedai vyeo wamepewe watu wengine kwa kujuana badala ya kukupa wewe ambaye unadhani unastahili.

Sasa kipi kinachokufanya udhani unastahiki wewe badala ya hao waliopewa?
 
Mimi sijalilia madaraka huko chadema. Wewe unayedai vyeo wamepewe watu wengine kwa kujuana badala ya kukupa wewe ambaye unadhani unastahili.

Sasa kipi kinachokufanya udhani unastahiki wewe badala ya hao waliopewa?
cheo gani?
 
2015 ni CHADEMA TU KUBALI USIKUBALI HISTORIA YA UKOMBOZI WA TAIFA HILI INAENDA KUANDIKWA 2015.
Hata J.K analijua hilo itakuwa wewe hoi hai ???????????
 
cheo gani?

Daima aliye ndani ya gari kamwe hawezi kulisukuma,bali aliyeko chini. Kwa dhani hiyo basi hauwezi kusema nafaa kuwa rais kuliko yule. Ninachotaka kusema ni kwamba,wanaokutazama ndiyo wanakujua zaidi kama unafaa au la!
 
Kwa hiyo majibu ndio tatizo la Watanzania.
 
Umelalamika vyeo wanapeana kwa kujuana. Maana yake wewe unahitaji sana cheo huko chadema ila hupewi kwa sababu hujulikani. Umeongea kwa uchungu sana.
Nimemlalamikia nani?Nimelalamikia vyeo gani?Sijulikani na nani huko chadema?Mkuu una uhakika hujadandia treni kwa mbele?
Msenyele said:
Daima aliye ndani ya gari kamwe hawezi kulisukuma,bali aliyeko chini. Kwa dhani hiyo basi hauwezi kusema nafaa kuwa rais kuliko yule. Ninachotaka kusema ni kwamba,wanaokutazama ndiyo wanakujua zaidi kama unafaa au la!
Ok,ulilielewa swali langu na kwanini nilimjibu Mkeshaji nilivyomjibu?
 
Last edited by a moderator:
nyie ngojeni tu watu waje na visingizio vingine ije 2015....
Unawachokoza au unasukumwa na UZALENDO? Hawa watu kutokana na kupagawa kwao kwa "Ushindi" wa Mwaka 2015 hawasikii la muadhini wala la mchota maji!!
 
Back
Top Bottom