Mbowe: Tutashika dola kirahisi 2015

Mbowe: Tutashika dola kirahisi 2015

Kwanini watu ambao tayari wana nyadhifa ndani ya chama wanapewa nafasi nyingine za kuongoza kwenye kanda?
Kwa sababu wana uzoefu wa kutosha, hili si la kulifanyia majaribio, si ajabu hao wapya wakawa PM7 wakavuruga sera hii nzuri ya majimbo
 
Mkuu nakubaliana na wewe. Watake wasitake kama wanataka kuchukua madaraka lazima watake risks. You can not take down the system by acting like the system. Hata kwenye boxing mtu ukipambana na mtu mwenye nguvu hushindani nae kwa nguvu unatafuta njia nyingine. To win Chadema must be different na kama ulivyo sema CCM siyo wajinga kama baadhi ya watu wanavyo taka kujiaminisha au kuaminisha watu wengine.

Haya ndiyo maamuzi magumu katika chama. Hakuna kitu kigumu kama kubadilisha mtazamo na utendaji wote katika chama. Just imagine, CDM toka kianzishwe kimekuwa na utendaji uliokuwa CLOSED ( centralisation) halafu unaamuka kesho na kusema kuanzia sasa ni OPEN (decentralisation).

Ngoma iko kwa viongozi, hata hivyo inategemewa watafanikiwa kwa sababu huwezi kuwalipa viongozi zaidi ya Tsh 7 milion per month na wasiweze ku-deliver. They have to justfy...
 
Haya ndiyo maamuzi magumu katika chama. Hakuna kitu kigumu kama kubadilisha mtazamo na utendaji wote katika chama. Just imagine, CDM toka kianzishwe kimekuwa na utendaji uliokuwa CLOSED ( centralisation) halafu unaamuka kesho na kusema kuanzia sasa ni OPEN (decentralisation).

Ngoma iko kwa viongozi, hata hivyo inategemewa watafanikiwa kwa sababu huwezi kuwalipa viongozi zaidi ya Tsh 7 milion per month na wasiweze ku-deliver. They have to justfy...


Mkuu ni kweli mabadiliko ni magumu kwa binadamu ila kama kiongozi lazima uwe na vision na vision ni kuona mbele zaidi. Kitu mimi ambacho ningesuggest ni Chadema kuangalia wapi wenzao walipo teleza. Kama tunavyo jua historia ya nchi yetu vyama vya upinzani vyenye nguvu vimekuja na kuondoka, tuliona NCCR 1995, tukaona CUF 2000 na sasa Chadema 2010 mpaka sasa. Inarudi pale pale kwamba CCM siyo wajinga kama watu wanavyo dhani. Ni lazima Chadema ikae na kutafakari what went wrong na wenzio (NCCR, CUF) na wao wafanyeje kuepuka hilo. Mimi ningekua Chadema ningetumia haswa haswa CUF as a case study kwa sababu njia CCM walioitumia kuki assasin CUF ndicho wanacho tumia kwa Chadema which ni kupaint Chadema kama chama cha dini fulani na majimbo fulani. Kwa kiasi fulani CCM imefanikiwa kwa hilo kwa sababu kuna a significant namba of people wanao kiona Chadema kama chama cha Kikatoliki na Kilimanjaro. Hilo wasipuuzie hata kidogo haswa kuelekea 2015 ambapo hamna incumbent na hamjui CCM itamsimamisha nani.

Kuhusu hilo la kujustify mishahara mkuu ni a given. Halafu siasa bwana mchezo mchafu sana, ukiwa at the hight of your fame you can do no wrong (kama ilivyo kuwa kwa JK 2005) lakini watu wakisha anza kukuchoka tu (na hii humtokea kila mwanasiasa) basi hapo ndipo hata swala dogo linapo kuzwa. Sasa hivi wanaweza wakaamua kumlipa Slaa hata milioni 20 kwa mwezi na hakuna atakae hoji.
 
Mbowe mbona unataka kuwaadaa wafuasi wenu mtashika dola kirahisi saabu mmeigawa nchi kikanda. Unadhani Watanzania ni wajinga wawape nchi kanda ya kaskazini.
 
Naona kama tunatofautiana hapa.Kumbuka hii hoja imeanzia kwenye vetting.
Naomba uniweke sawa. Wapi hasa tofauti yetu inagonga kwa sababu mazingira ya kisiasa Tanzania ndiyo yanatoa mtazamo wa vigezo kwenye vetting ya viongozi wa kisiasa.
Does the person qualify for the position?
This is the fact, Kujuana is an added advantage kwenye vetting when it come to any political position in any unpredictable political field like Tanzania.
Pia kuwa mwanachama si kweli kwamba umeingia kwenye system.

Kwa mtazamo wako, kuingia kwenye system ya siasa kunaanzia wapi. Na kigezo cha chini kabisa cha kuwa viongozi kinaanzia wapi.
 
Mkuu ni kweli mabadiliko ni magumu kwa binadamu ila kama kiongozi lazima uwe na vision na vision ni kuona mbele zaidi. Kitu mimi ambacho ningesuggest ni Chadema kuangalia wapi wenzao walipo teleza. Kama tunavyo jua historia ya nchi yetu vyama vya upinzani vyenye nguvu vimekuja na kuondoka, tuliona NCCR 1995, tukaona CUF 2000 na sasa Chadema 2010 mpaka sasa. Inarudi pale pale kwamba CCM siyo wajinga kama watu wanavyo dhani. Ni lazima Chadema ikae na kutafakari what went wrong na wenzio (NCCR, CUF) na wao wafanyeje kuepuka hilo. Mimi ningekua Chadema ningetumia haswa haswa CUF as a case study kwa sababu njia CCM walioitumia kuki assasin CUF ndicho wanacho tumia kwa Chadema which ni kupaint Chadema kama chama cha dini fulani na majimbo fulani. Kwa kiasi fulani CCM imefanikiwa kwa hilo kwa sababu kuna a significant namba of people wanao kiona Chadema kama chama cha Kikatoliki na Kilimanjaro. Hilo wasipuuzie hata kidogo haswa kuelekea 2015 ambapo hamna incumbent na hamjui CCM itamsimamisha nani.
Kwa hili nakubaliana na wewe.
Kama ulivyogusia kwenye mabandiko yako hapo juu. Sidhani kama CDM walishafanya tasmini ya wapi walijigonga na kuanguka katika chaguzi zilizopita kama kauli za viongozi wa juu wa chama ndizo hizi kuwa watashika dola kirahisi 2015 na juzi juzi Mh. Zitto pale Temeke alikuwa anasema kwenye mkutano wa hadhara kuwa Dr. Slaa ni Rais wa Tanzania ambaye hakutangazwa. Kwa mwenye fikra pana, maneno kama haya kabla ya miaka miwili kuingia kwenye uchaguzi ni dalili ya viongozi kuwa arrogant or bovile or prone to gaffe. Either way, Labda na CCM wawe kama wao, lakini kama CCM watakuwa makini, kauli kama hizi lazima wazifanyie kazi kujua kilichoko nyuma ya kauli hizi za viongozi wa CDM.

Kuhusu hilo la kujustify mishahara mkuu ni a given. Halafu siasa bwana mchezo mchafu sana, ukiwa at the hight of your fame you can do no wrong (kama ilivyo kuwa kwa JK 2005) lakini watu wakisha anza kukuchoka tu (na hii humtokea kila mwanasiasa) basi hapo ndipo hata swala dogo linapo kuzwa. Sasa hivi wanaweza wakaamua kumlipa Slaa hata milioni 20 kwa mwezi na hakuna atakae hoji.
Hii ni kweli kwa siasa za Tanzania. Angalia siasa za wenzetu hasa wa West. Kila kitu kinakuwa justfied kutolewa na kupokelewa not based on emotion kama ilivyo kwa Tanzania.
 
Kwa sababu wana uzoefu wa kutosha, hili si la kulifanyia majaribio, si ajabu hao wapya wakawa PM7 wakavuruga sera hii nzuri ya majimbo

Nyongeza ni kuwa naamini hilo limetokana na maamuzi ya chama taifa kwa kuanza tunatakiwa waongoze wanaolijua inside and out ili kuondoa vacuum kati ya chama na jamii.Kimkakati limesimama sana hili na naamini litaleta results..
 
Kwanini watu ambao tayari wana nyadhifa ndani ya chama wanapewa nafasi nyingine za kuongoza kwenye kanda?

I think wanachokifanya CDM is evolutional developement of leadership rather than revolutional, which make sense. They first build leadership in the party, then wakatengeneza sera, then wakahamasisha watu, na sasa wanafanya hypothesis test kwa kudecentralize uongozi wao.

Decentralization could be one and the first step, but development of leadership hierarchy could be the second step in which case the leadership itself is expected to gradually evolved from community inayohusika na siyo CDM makao makuu! Hata hivyo contribution ya CDM makao makuu kwa sasa is very vital to allow this smooth transition.

Wakifanya revolutional change basi wajiandae for a catastrophy huko baadae!!

U know sometimes its important to know that human being behave like non living things in so many ways including psychologically, culturally and economically. We all follow a similar pattern of change with, for example, water molecules or iron atoms when heated etc.


Kwa hiyo kwa mtazamo wangu this is the best way!!
 
Kweli wanasiasa wanaongoza kuota ndoto za mchana..Tena wanasiasa wa Tz kama wamelogwa hawataki kuongea ukweli kabisa.Mmelaniwa wote mnaoota Chadema kushika nchi 2015

Umelaaniwa wewe unayedhani mpaka leo CCM ni chama cha siasa kumbe ni bendi ya taarabu na genge la wahuni fulani.
 
Mbowe mbona unataka kuwaadaa wafuasi wenu mtashika dola kirahisi saabu mmeigawa nchi kikanda. Unadhani Watanzania ni wajinga wawape nchi kanda ya kaskazini.

Naiona vita ile kwa kauli zenu CCM za ukanda,ukabila na udini
 
Siku chache zilizopita, asha dii alikuja na mjadala mzuri juu ya kwanini yeye binafsi anadhania CCM itashinda uchaguzi mkuu wa 2015; Mwendelezo wa kauli kama hizi kutoka kwa Mbowe (ukiachilia ile ya mwaka jana kwamba CCM ikishinda 2015 atajiuzulu siasa), inaonyesha kwamba aidha kwa kujua au kutojua, kuelekea 2015, kutakuwa na more rhetoric (from chadema leaders) kuaminisha wananchi kwamba CCM itaanguka, kuliko effective practice/action ya kushirikiana na wananchi mapema kufanikisha hilo, hasa kwa Chadema kuachana na strategy ya kuvua wanachama milioni tano wa CCM and recruit them kuongezea idadi yao (chadema) ya wanachama takribani milioni mbili - tatu, na badala yake kujikita na swing voters bila ya kuhangaika kuwageuza kwanza kuwa wapiga kura wenye political affilitions na chadema; Kwa mujibu wa takwimu za wapiga kura 2010 ambao ilikuwa ni watanzania millioni kumi na nane, ukitoa wanachama wa CCM milioni tano, na wa chadema na vyama vingine vya siasa ambao sidhani kama wanazidi milioni tatu in total, it means column ya swing voters ni zaidi ya idadi ya wanachama wa vyama vyote vya siasa Tanzania, na hawa ndio watakuwa key to victory ya chama chochote baina ya hivi viwili iwapo turn out itakuwa ni kubwa 2015;

Unless chadema imefanya utafiti na kubaini kwamba ili kupigiwa kura na watanzania, ni lazima kwanza watanzania hao wawe wanachama wa Chadema; vinginevyo mimi kama mwanachama wa CCM pamoja na wengine wengi, tulipigia kura mgombea wa Chadema jimbo la Kawe - Halima Mdee kwani tuliona anatosha zaidi ya wagombea wa CCM na NCCR, huku kura yetu ya urais ikienda CCM kwa Kikwete kwani tulikuwa na imani nae kwamba atatekeleza mambo mengi kwa kasi zaidi baada ya serikali kuanguka 2008; mwenendo wetu wa kupiga kura kwa chadema 2010 (ubunge) means Chadema ina kura nyingi zaidi katika column ya swing voters (let alone ccm members) hata kama hawatakuwa wanachama wa Chadema by 2015; all Chadema needs is to engage them kisaikologia na kuwahamisha wajitokeze 2015, hasa kwa kuwa na rekodi zao ili wawe in constant communication kuliko kuhangaika kukusanya kadi za CCM; isitoshe, enzi za mass - based political parties zimeshapitwa na wakati, it no longer works for CCM, so Chadema should stop copying something which is already obsolete;

Vinginevyo, kama ya 2010 yatajirudia ambapo zaidi ya nusu ya wapiga kura hawakujitokeza kupiga kura, Chadema wasisahau kwamba a low voter turn out 2015 itakuwa ni ushindi wa CCM kwenda ikulu;

Hii imetulia mkuu,nimeipenda sana,ni darasa zuri kwa cdm.
 
Kweli wanasiasa wanaongoza kuota ndoto za mchana..Tena wanasiasa wa Tz kama wamelogwa hawataki kuongea ukweli kabisa.Mmelaniwa wote mnaoota Chadema kushika nchi 2015
nani asiyejua wote wanao kishabikia magamba kwa sasa wana maslai,nani asiyejua njaa na hujuya wa kutokujua wapi mnapokwenda,kwa kupewa kofia,kanga,pilau,2000,mjinga atabaki na ujinga wake werevu watajua wapiana kwenda,ashukuriwe mungu wajinga wamebaki wachache,kuliko werevu ndiomaana leo ccm hawalali maana mtaji wao wajinga wamebaki wachache,tuliatu utapata akili 2015 rais kutoka cdm akila kiapo cha kuongoza nchi,
 
Hii nchii bado ipo gizani sana,bado watu ambao wangeweza kuwa na uwezo wa uongozi na kuleta chachu katika siasa za vyama hapa kwetu Tz hawajitokezi kwa sababu bado chama kimeshika hatamu,kwa hiyo watu wengi wanaogopa kushughulikiwa,siasa za vyama vingi hapa ni uadui wa kutoana hata roho,sembuse kukuvurugia utaratibu wa maisha kwa kukukatia kila kimrija cha maslahi yako? Kwa hiyo bado watu wengi wamekuwa waoga,mtu anapiga hesabu ya familia yake na watu ambao wataathirika ikiwa atafanya kosa la kujoin opposition openly na hiyo kupelekea yeye kushughulikiwa.Wapo watz wengi sana ambao hawakubaliani na mfumo wa utawala wa ccm ulivyo nchini,but they wont't dare say it openly or join opposition kwa mazingira ya sasa ya kisiasa nchini mwetu.Kwa hiyo wanachokifanya chadema kwangu mimi naona sawa tu hata kama watawatumia watu hao hao,lakini ni waaminifu bila kujali sana hata viwango ilhali malengo ya chama chama kuleta ukombozi yanatekelezwa na kufikiwa,na wakati huo huo unakuwa gradual growth of well groomed leaders ambao wanakuja kuongeza nguvu na hatimaye kukabidhiwa ofisi.Mazingira yetu si mazuri kwa chama kumpa mtu yeyote madaraka nyeti kwenye chama kisha baadae anawaadhiri baada ya kupokea visenti kidogo kutoka kwa wapinzani wenu ambo wana nguvu ya pesa na dola,anawasemea mbovu awezavyo na kupotosha hata wengine.Chadema wako sahihi kwa wanachofanya,sasa kama mnaona njooni bongo mpate first hand experience na siasa zetu hapa bongo.Hali ni ngumu mno.
 
inapendeza sana na watu tuliowengi hata ambao tuko serikalini tunawaunga mkono sana cha msingi mdhibit mamluki sasa hivi si kila mmoja anayetoka ccm ni mwenzenu maana mnasifika kwa sifa ya kuachia vilivyo vyenu pale mnapoona wanaccm wamehamia kwenu hili hapana ama mlifanye kwa step
 
Umelaaniwa wewe unayedhani mpaka leo CCM ni chama cha siasa kumbe ni bendi ya taarabu na genge la wahuni fulani.

ngoja najazia nyama ndg,chama cha kupiga dili.kama unadili za kimagumashi,ccm,ndiko kichaka cha kujifichia,ivi hamjui kwamba ilenembo kwenye bendera yao wamesha badilisha siku iziwame weka nembo mpya,kisu na uma,sasa kinaitwa chama cha kula mema ya nchi,
 
Mbowe mbona unataka kuwaadaa wafuasi wenu mtashika dola kirahisi saabu mmeigawa nchi kikanda. Unadhani Watanzania ni wajinga wawape nchi kanda ya kaskazini.
ile vita ya udini mliopandikiza mmefanikiwa sana ndio maana znz sasa hivi mnavuna sasa endekezeni na hii ya ukabila! si unakumbuka wakati mzee dhaifu alipoona dr slaa kampumulia kooni akaanza ooh wakristu ooh sijui ni ni na wewe anza kuachama tu
 
Sikatai wala sikubaliani na wewe.
Sio kwamba sikubali juhudi wanazofanya. La hashaaa. Ni kwa sababu ya hawa ndugu zetu wa chama tawala. Enewei, tungoje tuone.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
sijui kama mna wa fahamu wanyama flani wanapatikana kwa wingiiiiiiisana serengeti wanaitwa nyumbu,sasa basi nitazielezea tabia za nyumbu[1]hawaji wanapo kwenda,[2]mmoja akiamua kutamkia kwenye maji wote watafuata,[3]ni majinga,[4]wapo wapo tu,/kushabikia ccm leo ni mfano wa nyumbu,nyumbu hajui hata bei za mafuta ya taa,petrol,diesel,sukari,mafuta kupikia,mchele,unga,na lingine nyumbu hajui migomo ya walim,ma dr,wananchi kuporwa aridhi na kupewa muwekezaji,ufisadi,nyumbu hajui,deni la taifa limefika sh,trilion 21,twiga kupelekwa nje,poleni manyumbu,wamezoeshwa kupewa tsheti,kofia,kanga,skafu,na, 2000 kupakiwa kwenye malori,manyumbu hayajui kwamba,yana fanya nini juu ya mstakabali wao na watoto wao,ama kweli huyu ndio nyumbu,
 
Kwa hiyo Mbowe anasema watashinda kirahisi kwa sababu ya sera ya Majimbo?

Majimbo ndio "muarubaini" wa matatizo yetu?

Hivi hajajifunza kitu kutoka kwa Mrema?

Kwamba Watanzania hata kama una resonate nao kutokana na uozo wa CCM, hawapendi kuwa taken for granted na matatizo yao kuwa downplayed?

Hivi Mbowe kawa misquoted au ndo kweli anataka tuamini majimbo ndo jibu la matatizo yetu?
 
Very interesting topic. Let me add my two cents into the discussion.

Kama mkuu Mchambuzi alivyo sema hapo juu kuna a lot of rhetoric coming out of Chadema na hata ukiangalia washabiki wengi wa Chadema humu ndani (kama kweli ni washabiki wa Chadema maishani au mitandaoni tu) utakuta kauli nyingi ziko based on emotions (hisia). Mwaka 2010 kuna wanaJF wengi walio kuwa wakii support Chadema (at least humu ndani, sijui mchango wao kiuhalisia) ambao walikua wana apa humu kwamba lazima Chadema itashinda 2010. Sisi ambao hatukua emotional about it tukasema its a premature declaration tuka tukanwa na kuitwa "mamluki", "mafisadi", nk. Matokeo yake Chadema ikashindwa 2010 na kwa sababu walisha jiaminisha kwamba ushindi ulikua must badala ya kujichunguza baada ya uchaguzi what went wrong kimbilio ikawa kwamba kulikua na uchakachuaje nk. Niwakumbushe tu watu kuhusu uchaguzi wa uraisi wa mwaka wa jana Marekani. Kambi ya mpinzani wa Obama, Mitt Romney na chama chake walisha jiaminisha ushindi na kujilisha data zisizo za ukweli kiasi kwamba matokeo ya uchaguzi yalipo anza kutiririka walishikwa na butwa.

Kitu kimoja nilicho gundua kuhusu siasa za Tanzania, na hii ni kwa vyama vyote, ni kwamba siasa zetu ni za kienyeji. Kwa wenzetu kama Marekani kuna kuwa na wanasiasa ambao kazi yao ni kutoa rhetoric na topic points lakini nyuma yao kuna wataalamu haswa wawe wa kukusanya data (research), wa communications (speech) nk. Kwa hiyo unakuta mgombea ndiyo mwanasiasa lakini behind him kuna team of professionals. Sisi kwenye chaguzi zetu kila mtu ni mwanasiasa kwa hiyo unakuta they has been no research done what so ever. Sijui kwa upande wa Chadema ila mimi ningekua na cheo Chadema baada ya 2010 ningetaka status report ya what went wrong. Ningetaka uchunguzi ufanyike na wataalamu siyo wanasiasa waangalie je ujumbe wetu ulipokelewaje na different groups of people (wa mjini/vijijini, wanaume/wanawake, wazee/vijana nk.). Pia ningeagiza kwamba kila baada ya muda fulani ifanyike polls kuangalia uhalisia wa kukubalika kwetu. Kumbuka kujaza watu kwenye mikutano haimaanishi kukubalika kwenye sanduku la kupigia kura. Sidhani kama kume wahi tokea mashabiki wa chama passionate kama wa CUF lakini leo chama kikoapi.

Kwa hiyo ushauri wangu kwa vyama vyote, especially CCM na Chadema kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 ningeomba wafanye professional research na kujipima uhalisia wa kukubalika kwao. Watu wanasahau Tanzania ni nchi ya watu milioni 45 na wengi wanaishi mjini lakini watu wakiona kwenye tv mikutano ya kivyama ya mjini imejaa watu wao wana chukulia kama ishara ya chama kukubalika kiasi hicho nchini kote na hii ina tokana na too much emotions and lack of professionalism. Mfano ni huu wa Mbowe kusema ujumbe wao wa kimajimbo unakubalika na ndiyo utawafikisha ikulu 2015. Hajaonyesha any study or research kuprove so which means kauli ni either rhetoric as usual au its based on emotions.

mkuu unanichekesha. viongozi wa chedama wamewaaminisha wafuasi wao kuwa walishinda, lakini ukiangalia wao wana wabunge 20 na ccm zaidi ya 200. huo ushindi ungewezekana Tanzania tu na si mahali pengine popote duniani.
 
Back
Top Bottom