Mbowe: Tutashika dola kirahisi 2015

Mbowe: Tutashika dola kirahisi 2015

mwanakijiji ameshakuwa mmarekani,anarusha smart bombs tokea cleveland,ohio,anaogopa vita ya ardhini!!

Hauwezi ukajipa jukumu la kuangalia wenzako wanafanya nini alafu ukakosa cha kukosoa.
 
Mchambuzi:
Unapotoka unaposema Chadema inavuna wanachama 5Mil wa CCM, kwani wanachama na mashabiki wengi wa Chadema, hawaijuhi na wala hawajawahi kuwa CCM na kwa mpango ni kuwa Chadema ina Recruit vijana waleo, kizazi cha 90's ambacho hakijuhi CCM ni nini zaidi ya kuwa CCM ni Janga.
Labda cha kuwashahuri Chadema ni kuhakikisha elimu ya kutosha inafika kwa hawa vijana kwa ajili kuhakikisha siku ya kupiga kura wote wanajitokeza kupiga na kulinda.
 
Kwanini watu ambao tayari wana nyadhifa ndani ya chama wanapewa nafasi nyingine za kuongoza kwenye kanda?

Mzee Mwanakijiji najua kuwa wewe si mvivu wa kufikiri, kwa msingi huo, tohoa tafadhali kwa ulinganifu wa matukio kufikia hatua ya kuaminiwa ama kutokuaminiwa ya wamarekani/kimarekani na yetu nitakayoyateua:-
1) Ni baada ya Gen. Collin Powel "mwafrika" kuwathibitishia pasipo shaka "wazungu" wa marekani kwamba waafrika wanaweza alipoweza kwa mafanikio makubwa kuwa rubani mahiri hatimaye kukabidhiwa na Bush senior kuchora raketi ya vita vya ghuba,

2) harakati za kuzingua zilizofanywa na shonza, mwampamba & co. ndani ya harakati wakiwa miongoni mwa wanaharakati kuudai uhuru unaohitajika zaidi sasa kuliko wakati mwingine, huku wakifanya kazi za malware kuderail move ya ukombozi wakiwa embeded fighter wa jeshi la upinzani (ccm)

kama umenielewa vizuri mifano yangu ukiisha kuijadili tupe fikara zako, ni muda gani tuutumie kumchunguza askari wetu kabla ya kumuamini kumkabidhi Arsenal ama angalau B52 ashambulie kwa mfano kanda ya kati.

n.b adui (ccm) ana majeshi ya kukodi nayo ameyatapakaza haiyumkini miongoni mwetu.
 
Last edited by a moderator:
Katika wakati mgumu kama huu cdm inabidi kuangalia ni jinsi gani inapunguza madaraka toka kwa viongozi waliopo kama kina Mnyika. Wakati huo huo ijipange kuona ni jinsi gani inatafuta viongozi wapya na wakaandaliwa kwa namna ambayo hawatakuwa na madhara katika mchakato wa kuendea kushika Dola.

Wako wanachama ndani ya chama na ni wa muda mrefu tu. Hao wapikwe kwa kozi kwa maandalizi ya kufikia lengo. Hii tayari imeshakuwa ni pigo kwa ccm hivyo umakini ni muhimu mno.
 
Very interesting topic. Let me add my two cents into the discussion.

Kama mkuu Mchambuzi alivyo sema hapo juu kuna a lot of rhetoric coming out of Chadema na hata ukiangalia washabiki wengi wa Chadema humu ndani (kama kweli ni washabiki wa Chadema maishani au mitandaoni tu) utakuta kauli nyingi ziko based on emotions (hisia). ...

Mchango mzuri sana, CHADEMA, CCM chukueni hii mjenge juu yake. Hapo tutakuwa na kampeni nzuri sana
 
Na George Ramadhan|21st February 2013


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema sera mpya ya majimbo itakiwezesha chama hicho kushika dola na kuongoza nchi kwa urahisi zaidi.

Akifungua kikao cha kazi za Chadema kilichofanyika jijini hapa jana, Mbowe alisema sera ya majimbo ni mkakati uliobuniwa na chama hicho kwa lengo la kusogeza madaraka kwa wananchi ili kushiriki kufanya maamuzi ya jinsi ya kuongoza nchi....
ndiyomkuusana naomba tofauti ya sera za majimbo na sera za CCM za upelekaji madaraka mikoani; uanzishwaji wa serikali za mitaa na kitu wanachoita "D by D"
 
Na
George
Ramadhan|21st February 2013


Mwenyekiti wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema sera mpya ya
majimbo itakiwezesha chama hicho kushika dola na kuongoza nchi kwa
urahisi zaidi.

Akifungua kikao cha kazi za Chadema kilichofanyika jijini hapa jana,
Mbowe alisema sera ya majimbo ni mkakati uliobuniwa na chama hicho kwa
lengo la kusogeza madaraka kwa wananchi ili kushiriki kufanya maamuzi ya
jinsi ya kuongoza nchi....

Ukisoma gazeti la Mtanzania la Jana utabaini propagander inayopigwa na watu wa CCM dhidi ya Serikali inayotawala ni kali zaidi ya inachoweza kufanya CDM, the war within CCM kwa sasa imefika kwenye hatua mbaya, hii inaifanya CDM kushika nchi huku wanakunywa chai
 
Hizi kauli wanasiasa wa Afrika wamezoea sana kuzitumia ili baada ya uchaguzi wapate justification ya kusema wameibiwa kura. Yaani leo anatoa kauli kuwa ana uhakika wa ushindi halafu baada ya uchaguzi akishashindwa anatumia yake ya awali kuthibitisha kuwa alishinda ila ameibiwa kura. Kwa vile wafuasi wengi hawakai chini kuchuja, wanabeba maneno hayo na kuamini kuwa chama chao kimedhurumiwa.
Hii ni sawa na wale fanatics wanaoamini kuwa Wilbroad Slaa alishinda uchaguzi wa mwaka 2010, ukiuliza vigezo wanatumia kauli za huyohuyo mwanasiasa!!!!
 
nyie ccm mjiulize kama 2010 mligawana kura na wapinzani tena hazikutosha nye kwa hii miaka mitano mmeboreshaje maisha ya watanzania mpaka muje kukubalika tena..? nyi mkishindwa uchaguzi hamtakubali kuachia madaraka kwa fikra zenu mgando mlizonazo!
 
wanachofanya cdm ni sahihi kabisa, bado mapema, baadhi ya watu hawaaminiki na kadiri muda unavyokwenda ndivyo watu watazidi kujuana zaidi. Hebu fikiria wangekuwa wameshapewa nafasi nzito akina shonza ingekuwaje mbele ya safari? Na akina shonza wako wengi tu ndani ya upinzani. Hatua kwa hatua tutafika.
 
Vyeo vinavyotolewa kwa kujuana kuna vetting gani?Yale yale ya rubbe stamp tu.
Wakati mwingine watu msiishie tu kulalamika na kupiga majungu mitandaoni.
Mtu hajaonesha jitihada zozote za kukipigania chama, naye anataka apewe madaraka from nowhere.
Ndo yale yale ya akina Shonzi et al.
 
Kwanini watu ambao tayari wana nyadhifa ndani ya chama wanapewa nafasi nyingine za kuongoza kwenye kanda?

MM ni heri hao wenye nyadhifa tayari wanajulikana kuliko kuweka watu wapya,unaweza kuta umejaza
wasaliti"
 
Siku chache zilizopita, asha dii alikuja na mjadala mzuri juu ya kwanini yeye binafsi anadhania CCM itashinda uchaguzi mkuu wa 2015; Mwendelezo wa kauli kama hizi kutoka kwa Mbowe (ukiachilia ile ya mwaka jana kwamba CCM ikishinda 2015 atajiuzulu siasa), inaonyesha kwamba aidha kwa kujua au kutojua, kuelekea 2015, kutakuwa na more rhetoric (from chadema leaders) kuaminisha wananchi kwamba CCM itaanguka, kuliko effective practice/action ya kushirikiana na wananchi mapema kufanikisha hilo, hasa kwa Chadema kuachana na strategy ya kuvua wanachama milioni tano wa CCM and recruit them kuongezea idadi yao (chadema) ya wanachama takribani milioni mbili - tatu, na badala yake kujikita na swing voters bila ya kuhangaika kuwageuza kwanza kuwa wapiga kura wenye political affilitions na chadema; Kwa mujibu wa takwimu za wapiga kura 2010 ambao ilikuwa ni watanzania millioni kumi na nane, ukitoa wanachama wa CCM milioni tano, na wa chadema na vyama vingine vya siasa ambao sidhani kama wanazidi milioni tatu in total, it means column ya swing voters ni zaidi ya idadi ya wanachama wa vyama vyote vya siasa Tanzania, na hawa ndio watakuwa key to victory ya chama chochote baina ya hivi viwili iwapo turn out itakuwa ni kubwa 2015;

Unless chadema imefanya utafiti na kubaini kwamba ili kupigiwa kura na watanzania, ni lazima kwanza watanzania hao wawe wanachama wa Chadema; vinginevyo mimi kama mwanachama wa CCM pamoja na wengine wengi, tulipigia kura mgombea wa Chadema jimbo la Kawe - Halima Mdee kwani tuliona anatosha zaidi ya wagombea wa CCM na NCCR, huku kura yetu ya urais ikienda CCM kwa Kikwete kwani tulikuwa na imani nae kwamba atatekeleza mambo mengi kwa kasi zaidi baada ya serikali kuanguka 2008; mwenendo wetu wa kupiga kura kwa chadema 2010 (ubunge) means Chadema ina kura nyingi zaidi katika column ya swing voters (let alone ccm members) hata kama hawatakuwa wanachama wa Chadema by 2015; all Chadema needs is to engage them kisaikologia na kuwahamisha wajitokeze 2015, hasa kwa kuwa na rekodi zao ili wawe in constant communication kuliko kuhangaika kukusanya kadi za CCM; isitoshe, enzi za mass - based political parties zimeshapitwa na wakati, it no longer works for CCM, so Chadema should stop copying something which is already obsolete;

Vinginevyo, kama ya 2010 yatajirudia ambapo zaidi ya nusu ya wapiga kura hawakujitokeza kupiga kura, Chadema wasisahau kwamba a low voter turn out 2015 itakuwa ni ushindi wa CCM kwenda ikulu;
Mkuu Mchambuzi you are right in one way, wrong in another.

Kampeni zote, yaani ku-recruit wanachama wapya (ikiwemo kuchukua wale wa ccm ili kuidhoofisha) na kuelimisha wale swing voters ili waiamini chadema inabidi ziende sambamba. Na nina imani ndicho wanachokifanya chadema kwa sasa.

Kwa muda uliobaki sasa kufikia 2014/2015 huwezi ukaenda na kampeni moja moja kwani muda utakuwa hautoshi. Afterall unapofanya mkutano mahali popote unakuwa na watu wa aina zote hizo mbili ulizozitaja kwa hiyo ni vema kupiga ndege wawili kwa jiwe moja.

Kuchukua wanachama wa ccm ni muhimu kwani ni mahesabu ya ki-accounting yaani una credit kwako na ku-debit kwa adui yako. Wakati huo huo unabeba na wale wanachama ambao ni swing voters. Hii ni muhimu sana.

Unapokuwa na wanachama wengi unakuwa umeongeza wigo wa watu wa kukusemea, yaani kutangaza itikadi yako kwa wengine ambao ni "undecided". Hili ni muhimu sana.

Unapofika uchaguzi unakuwa na kazi ya ku-brush kidogo tu kwani kazi kubwa inakuwa imeshafanyika huko mitaani.

Kutegemea ku deal na swing voters pekee ni hatari kwani hawa wengi wao huwa wanabadilika kutegemea na upepo unavyovuma.
 
Ni vizuri kujua nia ma dhumuni ya chama chochote cha siasa Duniyani ni kutaka kuchukua au kuongoza Doula. Hivyo Mbowe ana haki zote kutamka hivyo kwani ndio dhumuni lao la kuunda chama chao.

lakin uhalisia inabidi ajipime je itawezekana?

Tombe mola tuone 2015.
 
Ni kweli dola siku hizi zinashikwa kirahisi
$1 , $10, $100 zote zinapatikana kirahisi .
 
MM ni heri hao wenye nyadhifa tayari wanajulikana kuliko kuweka watu wapya,unaweza kuta umejaza
wasaliti"

Mpaka lini?
Kila mzazi anapenda mtoto wake wa kike abaki bikira mpaka wakati anaolewa, sio rahisi kiivyo. Jukumu la kukilinda chama lipo mikononi mwa wanachama na si viongozi peke yao ni vizuri kuwa na imani na wenye chama kuwa hawawezi yumbishwa na mamluki.
 
Back
Top Bottom