Mbowe: SMG bastola zilitumika Arusha

Mbowe: SMG bastola zilitumika Arusha

Tupo pamoja nanyi Kamanda. Huu ni msiba mkubwa kwa taifa zima kwa wote wanaopenda demokrasia. Kitendo kilichofanywa Arusha si UGAIDI dhidi ya CHADEMA bali ni UGAIDI dhidi ya DEMOKRASIA. Ninaamini Watanzania walio wengi - wawe ni wafuasi wa CCM, CDM, CUF, TLP, na wasiojinasibisha na vyama - wangependa kuona DEMOKRASIA inakua. kama hivyo ndivyo, basi huu ni msiba wetu wote. Tuoneshe mshikamano kama taifa kwa kulaani vikali vitendo kama hivi vinavyokusudia ku-terrorize wananchi wasiwe huru kujumuika katika mijumuiko ya kisiasa kuunga mkono itikadi yo yote wanayochagua au kidini kushiriki katika imani walizochagua. Nasema tena huu ni UGAIDI DHIDI YA DEMOKRASIA na ulaaniwe na kila mpenda demokrasia. Waliotangulia RIP na waliojeruhiwa tunawaombea Muumba awarejeshee afya zenu mapema.
 
Jii tume ni funoka kombe mwanaharamu apite,
tumuulize huyo Chagonja, tipoti ua yale mauaji ya mwanzo Arusha yako wapi!.Na nihatua gano zilichukuliwa naada ya kuikabidhi, zaidi ya kusikia mkwr wake sasa ni staff one?? Tuamini sasa anakuja kupandisha byeo wengone au kaja kutenda kazi lwa mujibu wa kiapo cjake?

Maneno ya Mchrmba na Mwanri yangekuwa yamesemwa napinzani wangekuwa Kisomgo, Pia kauli ya Nape jana ingekuwa motu wa upinzami kaitoa asinge kuwa uraiani,
Ila kwa vile ni vionhozi wa ccm wanapeta.
 
yaani kauli inachunguzwa vipi....mbona wanatufanya sisi watnzania wajinga...unachunguza kauli kivipi...?
 
Sijui lini vituko vitaisha nchini kwetu. Maana kabla hili halijaisha linatokea jengine lol. R.I.P wote waliopteza maisha Arusha
 
Mwigulu kauli yake inachunguzwa vp? Mimi naona wangesema akamatwe then aeleze alikuwa na dhamila ipi. Acheni porojo kwenye uhai wa watu, i wish avute kigogo mmoja ili tuone nalo kama mtachukulia poa maana hawa wengine mnaona kama kuku tu. MNATIA HASIRA SANA
 
Uchaguzi wa Madiwani wa Kata nne za Jiji la Arusha uliokua ufanyike leo umeairishwa hadi tarehe 30/06/2013 mwaka huu,uchaguzi huo umeahirishwa kufuatia shambulio la kigaidi lililotokea jana katika Mkutano wa kufunga kampeni ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Akizungumza na Habarimpya.com jijini Arusha Mkurugenzi wa Jiji hilo Sipora Liana amesema uchaguzi huo umeairishwa kutokana na sababu za Kiusalama,na kwamba utafanyika katika tarehe hiyo endapo hali itatulia.
"Tumelazimika kuahirisha uchaguzi huo kwa sababu za kiusalama, hatuwezi kuendelea na uchaguzi katika hali kama hii, hali si shwari katika Jiji la Arusha na hata tarehe hiyo iliyopangwa pia inaweza ikaahirishwa endapo hali haitakuwa shwari"alisema Liana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema katika tukio hilo watu wawili mwanamke na mwanamume wamepoteza maisha, huku akidai kwamba bado wanafuatlia idadi ya majeruhi waliotawanywa katika Hospitali mbalimbali -mkoani humo.
Hilo ni tukio la pili la bomu kulipuka katika mkusanyiko wa watu wengi mkoani humo, Mei 5 mwaka huu bomu lililipuka katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasit mjini Arusha na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.


HIYO milipuko ilipangwa kabisa na MWIGULU,RPC wa ARUSHA pamoja na MKUU WA MKOA WA ARUSHA ili Arusha ionekane hakuna amani uchaguzi upigwe dana dana
 
muuaji ni ccm na polisi, polisi wanajua hilo sasa wanachunguza nini....
 
Haki ya Mungu wauaji wa Padri, moshi,Mwangosi, waliomjeruhi Padri Ambross, waliolipua bomu katika ziara ya balozi wa papa, watekaji na kutesa Dr-Ulimboka, Kibanda na huu ulipuaji wa bomu jana ni genge lile lile linalopokea amri kutoka kwa Master mind yule yule mmoja. Don't go far, MWIGULU IS ONE OF THEM!! I swear!!!
.
 
Sijui lini vituko vitaisha nchini kwetu. Maana kabla hili halijaisha linatokea jengine lol. R.I.P wote waliopteza maisha Arusha
Ni wakati sasa wa kuheshimu uniform alovaa Said Mwema na kumwambia ajifanyie yeye uchunguzi lakini hatumtaki wala hatutaki majibu. Tutapigana na Mungu atawalipa. Wasitugeuze wajinga na danganya toto yao
 
Tupo pamoja nanyi Kamanda. Huu ni msiba mkubwa kwa taifa zima kwa wote wanaopenda demokrasia. Kitendo kilichofanywa Arusha si UGAIDI dhidi ya CHADEMA bali ni UGAIDI dhidi ya DEMOKRASIA. Ninaamini Watanzania walio wengi - wawe ni wafuasi wa CCM, CDM, CUF, TLP, na wasiojinasibisha na vyama - wangependa kuona DEMOKRASIA inakua. kama hivyo ndivyo, basi huu ni msiba wetu wote. Tuoneshe mshikamano kama taifa kwa kulaani vikali vitendo kama hivi vinavyokusudia ku-terrorize wananchi wasiwe huru kujumuika katika mijumuiko ya kisiasa kuunga mkono itikadi yo yote wanayochagua au kidini kushiriki katika imani walizochagua. Nasema tena huu ni UGAIDI DHIDI YA DEMOKRASIA na ulaaniwe na kila mpenda demokrasia. Waliotangulia RIP na waliojeruhiwa tunawaombea Muumba awarejeshee afya zenu mapema.
Broda,
Uko sahihi sana mkuu, na umetuliza kichwa.

Kimsingi ilibidi mhimili wa Bunge ambao ni mhimili ma wananchi utambue hilo na walipaswa kuahirisha shughuli zote za leo ili kuungana na Watanzania kuomboleza.
 
Hizo SMG ndizo alifauta china ili magharibi wasiwe na serial number?Wachina watatuua sana ili magamba wahonge nchi ili wabaki madarakani.Na uatajiri uliopo unawaumiza sana roho CCM.
​nani?
 
Kutoa kauli ya kutishia maisha ya mwenzako ni kosa kisheria. Mwigulu ameachiwa sana na Policcm, alianza kupiga watu, kumwagia acid na sasa anatumia mabomu. Polepole anajitengenezea uungu mtu, mwishoni atawageuka CCM na kuleta maafa mengi
 
Hiyo kauli ya Mwema ni ya kisiasa,na hata hiyo namba ya simu aliyotoa kwa kumwomba yeyote mwenye taarifa,zinaweza kufanikisha kuwakamata walioratibu mauaji ya Arusha,nayo ni danganya Tito.

Kama yeye mwenyewe IGP,amethibitisha bila shaka yoyote kuwa Mwigulu Nchemba,alitamka kwenye mkutano wa kampeni huko Arusha kuwa kama wakazi wa huko,hawataki kuichagua CCM,hakika watakufa,na imetokea kweli wamekufa.

Sasa swali tunalomuuliza IGP Mwema,anafanya uchunguzi gani mwingine,wakati imethibitika,maneno hayo aliyatamka Mwigulu Lameck Nchemba?!!

Ikiwa ile clip ya kuchongwa na Mwigulu,iliweza kumsotesha ndani Lwakatare miezi mitatu,ni kitu gani kinampa kigugumizi IGP Mwema,kumkamata Mwigulu Nchemba?!

Watanzania tunasubiri kuona baada ya ushahidi wote huo wa wazi unaomuhusisha Mwigulu,kabla siku ya leo haijaisha,Mwigulu awe ametiwa mbaroni,
.
Kama hilo halitafanyika,waTZ tutakuwa tumepata ushahidi mwingine usio na shaka yeyote kuwa jeshi la polisi,ni kitengo cha CCM,na mpango wa mauaji ya Arusha,uliratibiwa na CC ya chama tawala,ikiingozwa na amiri jeshi mkuu,ambaye ndiye mkuu wa nchi yetu!!!!!
 
Waliosema nchi haitatawalika mbona hawakamatwi na vitendo vyao tunaona madhara yake?
 
IGP aunda timu Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Mwema ameunda timu
ya kuongeza nguvu ya uchunguzi itakayoongozwa
na makamishna wawili ambao ni Paul Chagonja
kutoka idara ya operesheni na Isaya Mngulu kutoka
ofisi ya upelelezi makao makuu..

Paul Chagonja? .. Anaenda kufanya nini? Kuhalalisha unyama huu?... Heri hata angeokotwa teja au kibaka mtaani na kupewa kazi hii kuliko huyu jamaa.
 
Mwigulu, Nchimbi, Mwema, Chagonja, Mngulu ndio wakandarasi wakuu wa mauaji hayo. Tunategemea wajikamate?
 
Waliosema nchi haitatawalika mbona hawakamatwi na vitendo vyao tunaona madhara yake?

We mama fika mahali jali utu kuliko ushabiki wa udini na ukabila. Hivi angekuwa nduguyo kauawa ungeleta upuuzi huu?.
 
General mwigulu nchemba a.k.a. Jasusi

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom