Mbowe, Lema, Lissu kwanini hamkemei yanayoendelea nchini?

Elitwege

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
5,154
10,809
Kweli tumefikia hatua ya kupanga foleni kununua umeme?

Yaani kwa wakati mmoja mfumo wa TRA unasumbua, mfumo wa bandari unasumbua, mfumo wa LUKU unasumbua na TFF nao wamekula hela za wananchi.

Hapa hutaona Lissu, Lema wala Mbowe wakilaani shughuli za wananchi kusimama na kupanga foleni ya kununua umeme!

Hamuoni vitu vilivyopanda bei kiholela?
 
L
IMG_20210519_204613.jpg
 
Uhai wa mti ni mizizi yake na sio majani yake

Kama serikali iliyopo madarakani mizizi yake ni dhaifu tegemea uhai na uimara wa huo mti utakuwa mashakani

Tunaweka tegemeo kwenye mizizi dhaifu na tunajaribu kuficha ukweli

Kwa kweli huu ni unafiki, namna Rais wa awamu ya tano alivyokosolewa kwenye utendaji wake na hivyo hivyo tusiyafumbie macho hizi changamoto tunazokumbana nazo kwenye hii awamu ya sita.
 
Bado wanasubiri teuzi ziishe labda wanaweza wakapata.Wakikosa utaona rangi zao halisi
 
Kulaani sio lazima Lissu na Lema. Mbona usimtaje Kalemani? Hao uliowataja hata wasipolalamika,wewe ushalalamika inatosha na sisi tunachangia.

Au hata Lisu huko aliko Tanesco pia malipo yanasumbua?
Au unadhani amekaatu anafuatilia mapungufu ya huku?

Waache wachape kazi huko ughaibuni bwana maana pia huko kazi inaendelea
 
Back
Top Bottom