mama Chiku Abwao ameongelea mambo mengi sana, la kwanza maandamano amesisitiza kuwa maandamano ya CDM yanaungwa mkono na watu wa rika lote kwa kuwa yanawaamusha na kuwasemea wanyonge. akaonya kuhusu kejeli ya magamba kuhusu maandamano na kusema mbona na nyie mmeunga tela kwa kuandamana Mbeya na sisi CDM hatujawakejeli?ameonya serikali kuwa iliridhia mfumo wa vyama vingi ila inaongoza nchi kwa watisha wananchi hasa wa upinzani na akasema ndo sbb leo wabunge wa upinzani walokuwepo bungeni mwaka 1995 pamoja naye hawapo,wamekata tamaa na kurudi ccm na wachache walobaki ni mawakala wa ccm kama Mzee mrema(akaonywa na m/kiti asitaje majina) ila ujumbe ulikuwa umeshafika. akairudia rudia hotuba ya Mh Lema(soma thread ya hotuba ya lema) na kuitia nguvu zaidi. Akawaonya magamba kuwa nchi haitatawalika kama CDM wakikosa uvumilivu na akawaonya tena viongozi kuwa kama wataendelea hivi wananchi watawazomea popote wapitapo na maandamano yatazidi zaidi na wananchi wameamka ndo maana wanawaunga mkono. kuhusu wabunge wa ccm kusimama na kusema wananchi watawahukumu 2015, akasisitiza hakika watawahukumu ktk haki ya kuwatetea wanyonge na katu hawataogopa wala kukata tamaa kama hao walorudi ccm. kuhusu mauaji ya polisi akasema hawalaumu polisi kwa kuwa wanatii amri haramu ya viongozi wa ccm na akasema yeye na wenzake hawatacha kuwasemea wanyonge kama polisi imeua ndivyo watakavyosema bila kumung'unya maneno. kuhusu amani akasema hakuna amani palipo na udhalimu na umasikini na akampinga waziri nahodha aliyesema kuwa maandamano yanaleta umaskini, akampasha kuwa mbona maandamano yameanza juzi tu na miaka 49 mbona hamkuwapa maendeleo????ki ukweli ameongea with authority ya hali ya juu sana mpaka mawaziri walionyeshwa wanavyosisimkwa na kupigwa ganzi kwa kila sentensi aloongea.<br />
CDM ina hazina kubwa sana...sikuwahi kumjua huyu mama kuwa ni strong that much.