Mulangila Mukuru
JF-Expert Member
- Feb 24, 2010
- 1,945
- 724
<br />Wakuu,<br />
<br />
Naona kila dalili kwamba wabunge wa CHADEMA na wale wa NCCR - Mageuzi wapo pamoja na naona ushirikiano wao ni mzuri sana bungeni. Kinacholeta tatizo ni huyu mwenyekiti wa NCCR - Mageuzi ndugu <b>Mbatia</b> ambaye bado ana donge la kushidwa ubunge wa kawe na Mh. Halima Mdee kiasi kwamba hata kesi aliyofungua dhidi yake <b>amegoma</b> kuifuta.<br />ukiondoa CDM Chama kingine cha upinzani TZ ni NCCR CUF na vyama vilivyobakia ni wachumia tumbo
<br />
Ukimwondoa <b>Mbatia katika NCCR - Mageuzi </b>wanaobaki ni wapiganaji na wanatetea maslahi ya watanzania kama walivyo CHADEMA. Naomba ushirikiano huu uendelee hata huko Igunga ambako tunajiandaa kuchukua Jimbo basi tuite " CHADEMA & NCCR MAGEUZI OPERATION CHUKUA JIMBO". Pongezi zangu ziende kwa wabunge wote wa NCCR - Mageuzi kweli nyie ni wapiganaji wenzetu. Sisi wananchi wanyonge tunafarijika sana tukiona mnakuwa kitu kimoja. <br />
<br />
ref: Hotuba ya Mbuge kijana wa NCCR (jina limenitoka) alivyoguswa kwa kutolewa bungeni kiuonevu kwa Mh. Wenje jana.
<br />