KipimaPembe
JF-Expert Member
- Aug 5, 2007
- 1,285
- 699
Siasa za majukwaani zina wakati wake. Vipindi kama hivi siasa zinapigwa bungeni. Kama mmeshindwa kwenye uchaguzi na wabunge wenu ni wachache hakika hamtafurukuta. Inatakiwa kipindi hiki kitumiwe kujipanga upya kimfumo ndani ya chama. Hizi siasa za kudandia hoja za vikashfa vya hapa na pale si endelevu. CHADEMA mtajifunza hili lini? Tunataka tuone chama chenye mfumo unaoeleweka, siyo chama cha mikutano mikubwa ya kisiasa. Toka uchaguzi upite, hakuna hoja coherent iliyokwishasimamiwa na CHADEMA ikasimama. Sana sana imekuwa ni kucheza ngoma ya Magufuli na CCM; Magufuli kafanya vile, CHADEMA inapinga! Magufuli katumbua majipu CHADEMA inapinga. Magufuli hasafiri nje, CHADEMA inapinga, lazima asafiri taifa lisitengwe. Serikali imenyimwa misaada, CHADEMA ikashangilia. Wale wale walionyima misaada wamegeuka wanatangaza misaada mingi zaidi - CHADEMA in hoja gani?
Hizo siasa za matukio hazifiki mbali. CHADEMA imeteua katibu mkuu ambaye amebaki kwenye mashubaka. Hoja ni Lowasa na Sumaye?? ....... .... hao wote ni X CCM. Wana jipya gani? Halijaonekana mbali na yale yale ya kulalamikia kashfa za hapa na pale!
Hizo siasa za matukio hazifiki mbali. CHADEMA imeteua katibu mkuu ambaye amebaki kwenye mashubaka. Hoja ni Lowasa na Sumaye?? ....... .... hao wote ni X CCM. Wana jipya gani? Halijaonekana mbali na yale yale ya kulalamikia kashfa za hapa na pale!