MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,255
- 8,027
Bonjour wanabodi!
MBOWE CHANZO CHA YANAYOENDELEA CHADEMA.
Pamoja na miaka yote aliyoifumia kukijenga CHADEMA kwa jasho na damu ingawa si peke yake maana kuna ambao walipoteza maisha, wapo waliopotezwa mpaka sasa hawajulikani walipo, wapo walioumizwa sana na kuachiwa vilema vya kudumu hadi leo.
Yeye alikua kiongozi mkuu wa chama aliyeongoza jahazi kwenye mapambano dhidi ya CCM ingawa alishafikia Compromise (kulamba asali) kwa lugha laini ya 4Rs. Mzee Baba alikuwa mtu wa kelele nyingi, watawala ikimuita wayamalize analegea analamba halua anatulia huku nje utamsikia "No hate, No fear".
KWANINI MBOWE ANASTAHILI LAWAMA?
•Hakuna asiyejua vuguvugu la hawa G-55 kuondoka CHADEMA chanzo ni Uchaguzi ndani ya chama ambapo kundi la Waliokua wakimuunga mkono Mbowe baada ya kushindwa kuamua kutokwenda pamoja na uongozi uliopo chini ya Mwenyekiti mpya Wakili Tundu Lissu.
•Mh Mbowe alijua kabisa mwaka 2024 ilikua lazima kuwepo na Uchaguzi wa ndani ya Chama, kama mwenyekiti alipaswa kufanya maandalizi mapema. Nia ya yeye kugombea au kutogombea ilitakiwa ijulikane na mifumo ya ndani ya taasisi.
Hii ni kutokana na nguvu yake ndani ya chama na ambaye angejitokeza kugombea naye ikiwa naye ana nguvu, maana yake ni lazima yangetokea makundi mawili ndani ya chama. Kama kweli Mwamba ana akili na kama alikua na dhamira yakweli ya kukijenga chama alipaswa alijue hili mapema ili kukilinda chama.
MBOWE Vs LISSU KABLA YA UCHAGUZI WA CHAMA.
•Sote tunakumbuka jinsi yalivyoibuka mashambulio makali baina ya magwiji hawa wawili wa kisiasa kupitia media mbalimbali kabla ya uchaguzi kwa maana ya kampeni kwa kila upande. Kama siyo wao wenyewe kushambuliana basi ni makundi yao ya ushawishi ndani ya chama yalishambuliana. Katika hali ya kawaida, baada ya uchaguzi ilikua ni lazima uhasama na visasi viendelee ikiwa tahadhari haitachukuliwa mapema na wajibu huu ulikua ni wa mwenyekiti mwemye na baraza lake la wazee wa kumshauri.
Unaweza kuhisi ni uzembe wa uongozi uliopo kushindwa kuyaweka makundi haya pamoja lakini si kazi rahisi hivyo kwa jinsi walivyojeruhiana, ni kazi ambayo pengine ingechukua hata mwaka mzima kukaa sawa. Imagine Uchaguzi umeisha tar 22/01/2025 kisha baada ya miezi 3 baadaye Chief Comforter wa Chama ambaye ni mwenyekiti akakamatwa kwa kesi kubwa ya uhaini, hapo hapo agenda NRNE inahitaji kutembea, mabadiliko ya mifumo ya uendeshaji ndani ya chama yaendane na uongozi mpya yalihitajika. Hivyo kuzuia hili kundi lililoshindwa kuanza kuonesha hisia zake mapema hivi isingewezekana. Kumlaumu Mhe Lissu ni kosa kubwa sana labda uwe na akili ya kulimia bamia na mchicha tu.
BADO NAMLAUMU MBOWE
•Mhe Mbowe mpaka miezi 3 kabla ya Uchaguzi alikua bado hajaonesha nia ya kurudi kugombea tena nafasi hii ya juu ya uenyekiti wa Chama lakini aliyekua Makamu wake Mh Lissu alikua ameshaonesha nia ya kugombea tena nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama. Hii hali ya ukimya wa Mbowe hata alipoulizwa hakujibu ulikua Ujuha na usaliti wa hali ya juu ndani ya chama.
Ilikua lazima Watu makini ndani ya Chama waanze kujiuliza ikiwa Mwamba hatagombea anayekuja kugombea ni nani? Ana ushawishi ndani ya chama? Falsafa na tamaduni za chama ameiva nazo? Kwa sababu ndani ya CHADEMA ukimtoa Mhe Mbowe kwenye Ushawishi anayefuata ni Mhe Lissu. Hii hali pia ilipelekea watu kuanza kumfikiria Lissu ikiwa Mbowe hatagombea na walianza kujijengea hivyo mapema na ndio maana haikua ngumu kumshawishi agombee baadaye hata Mbowe aliposema familia yake imemshauri agombee.
•Ikumbukwe kuna hadi viongozi wa dini walihusika kuwakutanisha hawa mafahali wawili ili mmoja wao agombee uenyekiti na mwingine baadaye Urais wa nchi hapo baadaye. Lakini Mbowe alikataa kata kata kuonesha nia yake ya kugombea either nafasi ya uwenyekiti ndani ya chama au Urais baadaye. Muda huu wote Mhe Lissu alikua tayari kwa nafasi yeyote ambayo mwenyekiti Mbowe hataigombea, tatizo Mbowe hakua muwazi na ndiko ugumu wa mambo ulipoanza na ndio matokeo yake haya yanayoendelea leo kwenye Chama. Hivi kwa hali hii alaumiwe Lissu kwa lipi kama si Mbowe?
•Katika mgawanyiko wowote unapotokea ndipo adui hupenyeza, hapa ndio paliikuwa patamu kwa CCM kujipigia wanavyotaka.Wewe umekutwa upo katika hali ya majonzi ya kushindwa unapoozwa unapewa pole ya pesa, unaahidiwa cheo na maisha mazuri baadaye, hivi kwa misimamo ya hao wanaume ambao baadhi wake zao ni miongoni mwa COVID-19 wangekataa hizo ofa za adui?
•Yote tisa, kumi Mhe Mbowe alikua na uwezo wa kuepusha haya yote lakini mzee Baba kala jiwe mtajuana wenyewe dadadeki.
NINI KILIMSUKUMA LISSU KUGOMBEA UWENYEKITI CHADEMA?
•Hili liko wazi hata yeye alibainisha. Ilikua ni Utashi wake yeye pamoja na ushawishi wa wanachama baada ya Princess kupelekwa nyumbani kwake na moja ya maofisa wa juu wa chama na kumtaka apunguze volume ya sauti yake kwenye Public ili apate kumneemesha kwa vitu vitamu vitamu na laini, hii ilimtia wasi wasi mhe Lissu kama chama kitakua salama.
Mbaya zaidi aliyempeleka Princess Abdallah nyumbani kwake ni huyu anayetaka nafasi yake ya umakamu mwemyekiti. Mhe Tundu kwa jinsi anavyokipenda chama na hapendi hongo aliona moja kwa moja kwamba chama hakipo salama na huyo Afisa wa juu wa chama anayeutaka umakamu mwemyekiti na amempeleka Princess nyumbani kwake, moja kwa moja Mhe Mwemyekiti aliyekuwepo madarakani lazima atakua kamtuma na ulikuwa ndio mpango wake na yawezekana yeye kula vitamu vitamu alishaanza kitambo.
Hivyo kwa hali hii ilikua ni sababu tosha kwa mhe Lissu kugombea uwenyekiti na nafsi iliyokua agombee awali ya umakamu mwemyekiti agombee Mhe Heche ambaye kidogo kwa sifa wanakaeibiana na ushawishi pia anao kwa kuzingatia historia yake ya uongozi ndani ya chama.
HITIMISHO
Unaweza kuhisi siyo sawa kumlaumu Mhe Mbowe kwa kazi aliyoifanya ya kukijenga CHADEMA lakini yeye pia ndio chanzo cha yanayoendelea. Alikua na uwezo kabisa wa kuita kambi yake na kuwaelekeza kuunga mkono Mwemyekiti mpyq katika kukijenga Chama zaidi kua pamoja katika ajenda yao kuu ya NRNE kwa sasa.
Kukaa kwake kimya lazima alaumiwe na ni tafsiri ya kwamba yupo nyuma ya yanayoendelea. Kama hayupo nyuma ya yanayoendelea kama kiongozi mstaafu na mjumbe wa kudumu wa kamati kuu alikua uwezo wa kukinusuru na kukilinda Chama chake pendwa. Yawezekana kwa sasa amekichukia Chama kwa sababu tu ya kushindwa uchaguzi wala hakuna kingine.
MBOWE CHANZO CHA YANAYOENDELEA CHADEMA.
Pamoja na miaka yote aliyoifumia kukijenga CHADEMA kwa jasho na damu ingawa si peke yake maana kuna ambao walipoteza maisha, wapo waliopotezwa mpaka sasa hawajulikani walipo, wapo walioumizwa sana na kuachiwa vilema vya kudumu hadi leo.
Yeye alikua kiongozi mkuu wa chama aliyeongoza jahazi kwenye mapambano dhidi ya CCM ingawa alishafikia Compromise (kulamba asali) kwa lugha laini ya 4Rs. Mzee Baba alikuwa mtu wa kelele nyingi, watawala ikimuita wayamalize analegea analamba halua anatulia huku nje utamsikia "No hate, No fear".
KWANINI MBOWE ANASTAHILI LAWAMA?
•Hakuna asiyejua vuguvugu la hawa G-55 kuondoka CHADEMA chanzo ni Uchaguzi ndani ya chama ambapo kundi la Waliokua wakimuunga mkono Mbowe baada ya kushindwa kuamua kutokwenda pamoja na uongozi uliopo chini ya Mwenyekiti mpya Wakili Tundu Lissu.
•Mh Mbowe alijua kabisa mwaka 2024 ilikua lazima kuwepo na Uchaguzi wa ndani ya Chama, kama mwenyekiti alipaswa kufanya maandalizi mapema. Nia ya yeye kugombea au kutogombea ilitakiwa ijulikane na mifumo ya ndani ya taasisi.
Hii ni kutokana na nguvu yake ndani ya chama na ambaye angejitokeza kugombea naye ikiwa naye ana nguvu, maana yake ni lazima yangetokea makundi mawili ndani ya chama. Kama kweli Mwamba ana akili na kama alikua na dhamira yakweli ya kukijenga chama alipaswa alijue hili mapema ili kukilinda chama.
MBOWE Vs LISSU KABLA YA UCHAGUZI WA CHAMA.
•Sote tunakumbuka jinsi yalivyoibuka mashambulio makali baina ya magwiji hawa wawili wa kisiasa kupitia media mbalimbali kabla ya uchaguzi kwa maana ya kampeni kwa kila upande. Kama siyo wao wenyewe kushambuliana basi ni makundi yao ya ushawishi ndani ya chama yalishambuliana. Katika hali ya kawaida, baada ya uchaguzi ilikua ni lazima uhasama na visasi viendelee ikiwa tahadhari haitachukuliwa mapema na wajibu huu ulikua ni wa mwenyekiti mwemye na baraza lake la wazee wa kumshauri.
Unaweza kuhisi ni uzembe wa uongozi uliopo kushindwa kuyaweka makundi haya pamoja lakini si kazi rahisi hivyo kwa jinsi walivyojeruhiana, ni kazi ambayo pengine ingechukua hata mwaka mzima kukaa sawa. Imagine Uchaguzi umeisha tar 22/01/2025 kisha baada ya miezi 3 baadaye Chief Comforter wa Chama ambaye ni mwenyekiti akakamatwa kwa kesi kubwa ya uhaini, hapo hapo agenda NRNE inahitaji kutembea, mabadiliko ya mifumo ya uendeshaji ndani ya chama yaendane na uongozi mpya yalihitajika. Hivyo kuzuia hili kundi lililoshindwa kuanza kuonesha hisia zake mapema hivi isingewezekana. Kumlaumu Mhe Lissu ni kosa kubwa sana labda uwe na akili ya kulimia bamia na mchicha tu.
BADO NAMLAUMU MBOWE
•Mhe Mbowe mpaka miezi 3 kabla ya Uchaguzi alikua bado hajaonesha nia ya kurudi kugombea tena nafasi hii ya juu ya uenyekiti wa Chama lakini aliyekua Makamu wake Mh Lissu alikua ameshaonesha nia ya kugombea tena nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama. Hii hali ya ukimya wa Mbowe hata alipoulizwa hakujibu ulikua Ujuha na usaliti wa hali ya juu ndani ya chama.
Ilikua lazima Watu makini ndani ya Chama waanze kujiuliza ikiwa Mwamba hatagombea anayekuja kugombea ni nani? Ana ushawishi ndani ya chama? Falsafa na tamaduni za chama ameiva nazo? Kwa sababu ndani ya CHADEMA ukimtoa Mhe Mbowe kwenye Ushawishi anayefuata ni Mhe Lissu. Hii hali pia ilipelekea watu kuanza kumfikiria Lissu ikiwa Mbowe hatagombea na walianza kujijengea hivyo mapema na ndio maana haikua ngumu kumshawishi agombee baadaye hata Mbowe aliposema familia yake imemshauri agombee.
•Ikumbukwe kuna hadi viongozi wa dini walihusika kuwakutanisha hawa mafahali wawili ili mmoja wao agombee uenyekiti na mwingine baadaye Urais wa nchi hapo baadaye. Lakini Mbowe alikataa kata kata kuonesha nia yake ya kugombea either nafasi ya uwenyekiti ndani ya chama au Urais baadaye. Muda huu wote Mhe Lissu alikua tayari kwa nafasi yeyote ambayo mwenyekiti Mbowe hataigombea, tatizo Mbowe hakua muwazi na ndiko ugumu wa mambo ulipoanza na ndio matokeo yake haya yanayoendelea leo kwenye Chama. Hivi kwa hali hii alaumiwe Lissu kwa lipi kama si Mbowe?
•Katika mgawanyiko wowote unapotokea ndipo adui hupenyeza, hapa ndio paliikuwa patamu kwa CCM kujipigia wanavyotaka.Wewe umekutwa upo katika hali ya majonzi ya kushindwa unapoozwa unapewa pole ya pesa, unaahidiwa cheo na maisha mazuri baadaye, hivi kwa misimamo ya hao wanaume ambao baadhi wake zao ni miongoni mwa COVID-19 wangekataa hizo ofa za adui?
•Yote tisa, kumi Mhe Mbowe alikua na uwezo wa kuepusha haya yote lakini mzee Baba kala jiwe mtajuana wenyewe dadadeki.
NINI KILIMSUKUMA LISSU KUGOMBEA UWENYEKITI CHADEMA?
•Hili liko wazi hata yeye alibainisha. Ilikua ni Utashi wake yeye pamoja na ushawishi wa wanachama baada ya Princess kupelekwa nyumbani kwake na moja ya maofisa wa juu wa chama na kumtaka apunguze volume ya sauti yake kwenye Public ili apate kumneemesha kwa vitu vitamu vitamu na laini, hii ilimtia wasi wasi mhe Lissu kama chama kitakua salama.
Mbaya zaidi aliyempeleka Princess Abdallah nyumbani kwake ni huyu anayetaka nafasi yake ya umakamu mwemyekiti. Mhe Tundu kwa jinsi anavyokipenda chama na hapendi hongo aliona moja kwa moja kwamba chama hakipo salama na huyo Afisa wa juu wa chama anayeutaka umakamu mwemyekiti na amempeleka Princess nyumbani kwake, moja kwa moja Mhe Mwemyekiti aliyekuwepo madarakani lazima atakua kamtuma na ulikuwa ndio mpango wake na yawezekana yeye kula vitamu vitamu alishaanza kitambo.
Hivyo kwa hali hii ilikua ni sababu tosha kwa mhe Lissu kugombea uwenyekiti na nafsi iliyokua agombee awali ya umakamu mwemyekiti agombee Mhe Heche ambaye kidogo kwa sifa wanakaeibiana na ushawishi pia anao kwa kuzingatia historia yake ya uongozi ndani ya chama.
HITIMISHO
Unaweza kuhisi siyo sawa kumlaumu Mhe Mbowe kwa kazi aliyoifanya ya kukijenga CHADEMA lakini yeye pia ndio chanzo cha yanayoendelea. Alikua na uwezo kabisa wa kuita kambi yake na kuwaelekeza kuunga mkono Mwemyekiti mpyq katika kukijenga Chama zaidi kua pamoja katika ajenda yao kuu ya NRNE kwa sasa.
Kukaa kwake kimya lazima alaumiwe na ni tafsiri ya kwamba yupo nyuma ya yanayoendelea. Kama hayupo nyuma ya yanayoendelea kama kiongozi mstaafu na mjumbe wa kudumu wa kamati kuu alikua uwezo wa kukinusuru na kukilinda Chama chake pendwa. Yawezekana kwa sasa amekichukia Chama kwa sababu tu ya kushindwa uchaguzi wala hakuna kingine.
