Babu we ndio unazinduka leo. Mbona umechelewa. Sisi wengine tulikumbwa na Dr Slaa mitaani na tukafanya maamuzi magumu kupitia ushawishi wake tukaaamua kuvaa magwanda. Lakini leo hii aliyetushawishi AMEKATWA.! unadhani na sisi wafuasi tufanye maamuzi gani magumu.
Huyu Lowasa tulikuwa tunazunguka nchi nzima kuwaaminisha wananchi kwamba ni mwizi na fisadi. Na tuhuma hizi za wizi na ufisadi sio siasa, ni tuhuma ambazo ni kweli na tulikuwa tukiaminisha wananchi kwamba na ushahidi tunao. Sasa leo Mbowe na Mbatia kwa tamaa ya pesa za kuhongwa wamwamua kukumbatia fisadi hilo na jizi. Unadhani sasa sisi tuliokuwa wafuasi tufanye maamuzi gani.? NASHAURI KWANZA TUWE WAAMINIFU KWA VIONGOZI WETU WALIOJITOA KWA SABABU KUJITOA KWAO WANAMAANISHA KUNA UCHAFU UMEFANYWA.
PILI, KWA KUWAKOMESHA HAWA KINA MBOWE NA MBATIA, NA SISI TUWAKATE. TUCHAGUE CCM WALAU DR MAGUFULI AMETUONYESHA MSIMAMO ULIONYOOKA.
TATU, TUTAFUTE NAMNA YA KUWAREJESHA VIONGOZI WETU DR SLAA NA PROF LIPUMBA KUPITIA VYAMA VINGINE LAKINI SIO CHADEMA. IKIWEZEKANA HATA TURUDI CCM KWANZA AU TWENDE ACT.
NNE SHIDA YETU NI MAENDELEO YA KWELI. TWENDE POPOTE TUNAPOIMANI NAPO. MAMBO YA VYAMA SASA YAMEPITWA NA WAKATI.
TANO, TUONYESHE MSHIKAMANO KWA HILI NA NASEMA MBOWE NA MAFISADI WENZAKE WATAISOMA NAMBA