Mods naomba msiunganishe uzi huu na mwingine.
Kuna mambo mengi mazuri yanayoanzishwa lakini ghafla yanazimika.
Tumeshuhudia kampeni za usafi mwisho wa mwezi, usafiri bure kwa waalimu Dar, kupanda miti Dar na mazoezi yanayoongozwa na makamu wa rais Samia Suluhu.
Je, TRA kusoma mapato ilikuwa mojawapo ya 'kiki' hizi za kuanza na kuzima?
Swala la TRA kutusomea mapato na matumizi lilikuwa linatupa mwanga, japo hali ilikuwa ngumu kitaa lakini ukisikia fedha zimeelekezwa kwenye ujenzi wa airport Chato na hostel za Magufuli nyingine kwenye fly over atleast moyo unafarijika kuwa hatujapigwa.
Lakini ghafla.... hakuna taarifa ya mapato na matumizi, wasiwasi unawapata raia maana bajeti iliyopitishwa bungeni haifuatwi sasa hela zinakwenda wapi.
Au ndo hizo biashara zisizoeleweka kati ya TZ na North Korea?
Je, TRA kufungua branch Rwanda kuna kilichoongezeka au tunabeba mzigo wa kuwasaidia warwanda.
Wito: Tusomeeni mapato na matumizi labda italeta faraja katika kipindi hiki kigumu.