Mbona foleni zimezidi?

Mbona foleni zimezidi?

Nahisi ni huu ujenzi unaoendelea maeneo mengi ya katikati ya mji pale Ubungo kuelekea Kibaha, Mwenge kuelekea Posta, SGR pale Buguruni, na maeneo ya Shaurimoyo, Ujenzi unaoendelea pale mbagala..

Lakini pia kuna tatizo la mipango miji kwenye jiji la Dar es salaam, Shughuli nyingi za uzarishaji mali na maofisi yapo sehemu moja kwa maana ya Posta na Kariakoo hivyo hupelekea watu wote asubuhi kuelekea huko na jioni kuondoka..
Jiji la Dar es salaam linatakiwa liwe funzo kwetu katika kuijenga miji mingine inayokua kama DODOMA, MWANZA NA ARUSHA..
 
Tatizo la foleni dar halitanisha kama tamroad hawata badili ujenzi wa barabara.

Barabara wanazo jenga tanroad hazisaidii kupunguza folenj bali kupitisha magari.

Hawaweki solution za kusaidia magari kupita bila kusababisha foleni

Mfano niliwahi pita kanjia ka chuo udsm kutokea msewe.

Pale junction ya changanyieni wangeweka round about , kisha pale nbc napo waweke round about.. kisha wahamishe vile vituo viwili vya daladala, njia ya chuo foleni mtasahau.

Pale mlimani upande wa chini kuelekea ardhi kuna foleni sana.. solution ni kufanya njia ya chini iwe ni ya kuingia tuu na waondoe kile kituo cha daladala.


Njia ya bafamoyo hadi tegeta wanatakiwa kupunguza njia za kuingia na kutoka , pia wajenga under pass au over pass pale mwenge.
 
Mkuu kitambi siyo sifa ni ugonjwa unaokumaliza taratibu bila ya wewe kujua, hebu jitahidi kufanya chchote iwavyo ili ukiondoe hicho kitambi mkuu kabla hakijakugharimu. Ila siyo lazima kuufuata ushauri wangu.
Tokea nimehama huo mji nimegundua kuwa kumbe hata mimi nilikuwa na kitambi lakini kutokana na hekaheka za kugombea madaladala kilikuwa kimejificha,sasa hivi kametuna hadi raha...
 
Back
Top Bottom